Nazgur
JF-Expert Member
- Apr 19, 2020
- 3,730
- 2,850
Dar umeona picha leo hakuna mtu amehangaika na huyo mtu wako mpaka jioni sasa unapasemaje dar?Kila nikiangalia, mahesabu yangu yananiambia kwenye uchaguzi wa mwaka 2020 MAGUFULI anapigwa asubuhi na mapema tu
1. Kura za Kaskazini zitamkataa vibaya mno
2. Kura za kusini zitamkataa katakata
3. Kura za Waislamu ndiyo kabisaa maana teuzi zake nyingi wamezilalamikia
4.Kura za mji mikubwa kama Mbeya na Dar es salaam atazisikia katika bomba
5.Kura za Singida kwa Tundu Lissu na Nyalandu hizo asahau
6.Kura za wafanyakazi ambao hajawaongezea nyongeza za mishahara atazisikia katika bomba
7. Kura za Vijana wasio na ajira, Vijana wa vyuoni wanamwangalia wanasema hiiiiiii etc
8.Kura za Watanzania walioko kwenye social media wengi hawamkubali
9. Iringa atapigwa asubuhi na mapema tu
10.Kagera ndiyo kabisa wanasubiri wapitishe hukumu
11. Kule Kigoma kwa Mwami Zitto ndo asahau kabisa
12. Wafanyabiashara wanaosumbuliwa kodi na TRA wamenyuti hawana maneno mengi wanamsubiri kwa hamu wamsulubu
13. Wenye Magari waliogeuzwa ng'ombe wa kukamuliwa pesa na Matrafiki hawa wanamgojea kwa hamu kubwa wamuonyeshe kilichomnyoa kanga manyoya