The Burning Spear
JF-Expert Member
- Dec 23, 2011
- 3,436
- 8,276
Ndugu zangu, Uraisi siyo kazi ya kitoto. Urais siyo lelemama. Hata Nyerere alilitambua hilo hadi akasema mtu anayetumia nguvu au fedha kuingia ikulu ni wa kuogopwa kama ukoma.
Tafasiri ya haraka haraka ni kwamba mpaka Dakika hii Samia nchi imeshamshinda, hakuna nchi ngumu kuongoza kama Tanzania ukizingatia ni Mzanzibar hata jiografia ya bara inampiga chenga.
Iko hivi, kuna maeneo watu wanajipigia bila uoga wala aibu kwa sababu wote ni wezi kuanzia TAKUKURU, Polisi hadi mawaziri Hakuna wa kumchunguza mwenzake. Huko kwenye halmashuri hali ya wizi ni mbaya sana.
Kikwete mwenyewe alishawahi kukiri. Nanukuu, "Nawaletea chuma hiki maana mlikuwa mnasema Mimi ni mpole, sasa anakuja mkali". Mwisho wa kunukuu.
Watanzania hawatakiwi kudekezwa utavuna mabua, nchi ilipokuwa imefikia kipindi cha kikwete Magufuli alikuwa hakwepeki that is why Hayati alipitishwa. Sawa?
Je, mlimsikia Mzee Makamba kipindi hicho? Nanukuu, "Huyu atawabatiza Kwa moto siyo maji tena" Walimtabua Kuwa alikuwa mtu sahihi kwa Watanzania.
Sasa nakuja kwa mama Samia ni hivi, Maza hana meno wahuni wa mjini wanamdhalilisha hajui afanye nini. Muda utafika wanachi hawatataka Hata kusikia jina lake.
Maana hawezi kubatiza Kwa moto wa siyo mkali, upole wake umezidi wa Kikwete. Kwa Mwenendo huu ubadhilifu wa kodi zetu kutumiwa na watu binafsi upo pale pale ndiyo maana kila kukichwa wanampaka mafuta kwa mgongo wa chupa.
Kama wewe unalipa Kodi PAYE, afu mwisho wa SIku unasikia watu wamepiga pesa afu wanaishia kusutwa tu badala ya kurudisha hela inauma sana. Aiseee tunafanyia KAZI watu. Mishahara yetu inakatwa kodi ili watu wale badala ya kuleta maendeleo.
Busara ilikuwa ni kukamilisha miaka 10 ya Awamu ya tano akae pembeni kwa heshima Tofauti na hapo atapata tabu sana. Pia kama taifa tutakuwa tumepata hasara kubwa mno.
Nawasilisha.
Tafasiri ya haraka haraka ni kwamba mpaka Dakika hii Samia nchi imeshamshinda, hakuna nchi ngumu kuongoza kama Tanzania ukizingatia ni Mzanzibar hata jiografia ya bara inampiga chenga.
Iko hivi, kuna maeneo watu wanajipigia bila uoga wala aibu kwa sababu wote ni wezi kuanzia TAKUKURU, Polisi hadi mawaziri Hakuna wa kumchunguza mwenzake. Huko kwenye halmashuri hali ya wizi ni mbaya sana.
Kikwete mwenyewe alishawahi kukiri. Nanukuu, "Nawaletea chuma hiki maana mlikuwa mnasema Mimi ni mpole, sasa anakuja mkali". Mwisho wa kunukuu.
Watanzania hawatakiwi kudekezwa utavuna mabua, nchi ilipokuwa imefikia kipindi cha kikwete Magufuli alikuwa hakwepeki that is why Hayati alipitishwa. Sawa?
Je, mlimsikia Mzee Makamba kipindi hicho? Nanukuu, "Huyu atawabatiza Kwa moto siyo maji tena" Walimtabua Kuwa alikuwa mtu sahihi kwa Watanzania.
Sasa nakuja kwa mama Samia ni hivi, Maza hana meno wahuni wa mjini wanamdhalilisha hajui afanye nini. Muda utafika wanachi hawatataka Hata kusikia jina lake.
Maana hawezi kubatiza Kwa moto wa siyo mkali, upole wake umezidi wa Kikwete. Kwa Mwenendo huu ubadhilifu wa kodi zetu kutumiwa na watu binafsi upo pale pale ndiyo maana kila kukichwa wanampaka mafuta kwa mgongo wa chupa.
Kama wewe unalipa Kodi PAYE, afu mwisho wa SIku unasikia watu wamepiga pesa afu wanaishia kusutwa tu badala ya kurudisha hela inauma sana. Aiseee tunafanyia KAZI watu. Mishahara yetu inakatwa kodi ili watu wale badala ya kuleta maendeleo.
Busara ilikuwa ni kukamilisha miaka 10 ya Awamu ya tano akae pembeni kwa heshima Tofauti na hapo atapata tabu sana. Pia kama taifa tutakuwa tumepata hasara kubwa mno.
Nawasilisha.