Nitajuaje gari inachemsha?

Shukarani saaaaana kwa Maelezo ya Mazuri na ya Kina Mkuu. Ngoja nichek Kesho nifanye hilo zoezi la Mwisho kwenye maelezo yako Mkuu.. Ila kwenye Dashboard hakuna taa yeyote kwa maana ya gari kuchemsha.


Suala la pili ni hili la Kuongeza Maji, kiukweli Asubuhi ninapotaka Kuiwasha huwa naangalia Maji, naona kupungua kiasi cha kama Nusu Lita hivi huwa Naongeza ndiyo yanakuwa yamejaa kabisa pale Juu, sioni Kuvuja kokote ila kesho tena hata kama sijatembelea nakuta hayaonekani juu. Na huwa najaza kweli asubuhi kabla ya kuwasha.
Ila hakuna Kuvuja chini, vinginevyo nimejaza zaidi yanayovujia kwa kutoka juu hayo ndiyo nayaona kabisaaa.
Naomba kama kuna Maelezo ya ziada na tahadhali zozote ninazotakiwa Kuchukuwa.
Ahsante saana Mkuu.
Nimekuelewa mkuu. Ukikuta maji yameshuka na huyaoni jaribu kuingiza kidole chako kirefu kuliko vyote na ukiyagusa usiongeze, tembea hivyo hivyo siku nzima kesho yake pima tena kwa kidole usipoyagusa jua iko shida kwenye gasket au pipe ikiwa hamna leakage yeyote uloipata.
 
Nimekuelewa mkuu. Ukikuta maji yameshuka na huyaoni jaribu kuingiza kidole chako kirefu kuliko vyote na ukiyagusa usiongeze, tembea hivyo hivyo siku nzima kesho yake pima tena kwa kidole usipoyagusa jua iko shida kwenye gasket au pipe ikiwa hamna leakage yeyote uloipata.
Basi kuna Shida Mkuu.
Maana siyafikii Maji yalipo. Na shida inaweza kutatulika vipi Mtaalam?
 
Hizo zote 2 ni hali za kawaida sana wala zisikuumize kichwa.. Iko hivi

1. Unapojaza maji gari ikiwa imezimwa (imetulia) yanajaa kweny tank za radiator na kutulia ila unapowasha gari tayari yanaanza mzunguko wa kupooza engine hapo lazima yapungue sababu yametembea kweny engine yaan yapo kwen mzunguko. Unaweza kugundua kama gari inavuja kwa kukagua mwenyew upande wa chini wa radiator km inadongosha maji pia unaweza kuijaza full ikiwa ingine inatembea ili kujaza mfumo mzima wa kupooza, au unaweza kuangalia kiwango unachoongeza maji kila siku.. ukiona unaongeza maji kila siku au kila mara hapo kuna tatizo.

2. Suala la mfuniko kutoa sauti na kamvuke hapo tambua mfuniko wako uko sawa na unaifanya kazi yake ipasavyo.. Mifuniko ya radiator huwa ina act kama pressure release valve ambayo imesetiwa kweny kiwango flan cha joto na likifika hapo huwa inaachia mvuke wa moto kutoka nje ya radiator ukiangalia mfuniko huo kwa ndani una kitu kama spring na ruber ndo vinavyoruhusu huo mvuke unaouona.

Ikiwa umejaza maji yako kweny radiator gari ikiwa on kabla hujafunga mfuniko wa radiator kwanza angalia maji kama yametulia jua gasket iko sawa ila ukiona kama puvo au babbles zinapanda kutoka kweny radiator na kupasuka zikifika juu jua gasket yako huenda imeshaungua au ina cracks kadhaa.
Nakazia hapo kwenye point namba 2..
Akiona bubbles wakati amefungua mfuniko wa radiator, kuna mawili.
1...head gasket imeungua au
2...Wakati wa kujaza maji/coolant kwenye radiator, mjazaji hakujaza kitaalamu hivyo akaruhusu hewa kuwepo ndani ha mfumo wa upoozaji...hii hutokea kama radiator inajazwa upya..

hali hii ya kuwepo kwa hewa kwenye mfumo wa upoozaji, pia hisababisha bubbles ambazo mafundi ambao si wataalamu, huwaambia wateja head gasket imekufa na kuwataka wanunue mpya...

Kuna watu watu wengi wameshawahi kukumbwa na hii kadhia ya kubadilisha head gasket,kumbe mafundi wao ndiyo hawajui..

Pia kuna njia ya kienyeji ya kupima na kundua kama kuna cylinder ambayo inapoteza comprehension kuelekea kwenye cooling system
 
Nakazia hapo kwenye point namba 2..
Akiona bubbles wakati amefungua mfuniko wa radiator, kuna mawili.
1...head gasket imeungua au
2...Wakati wa kujaza maji/coolant kwenye radiator, mjazaji hakujaza kitaalamu hivyo akaruhusu hewa kuwepo ndani ha mfumo wa upoozaji...hii hutokea kama radiator inajazwa upya..

hali hii ya kuwepo kwa hewa kwenye mfumo wa upoozaji, pia hisababisha bubbles ambazo mafundi ambao si wataalamu, huwaambia wateja head gasket imekufa na kuwataka wanunue mpya...

Kuna watu watu wengi wameshawahi kukumbwa na hii kadhia ya kubadilisha head gasket,kumbe mafundi wao ndiyo hawajui..

Pia kuna njia ya kienyeji ya kupima na kundua kama kuna cylinder ambayo inapoteza comprehension kuelekea kwenye cooling system
Nakubaliana na wewe japo bubbles za hewa upandaji wake huwa tofauti ni zile zinazoashiria gasket head kuungua.. Very similar but not the same.
 
Habari ya Majukumu humu Ndani.

Naomba kusaidiwa hiyo hoja. Je, nitajuaje gari yangu inachemsha?

Gari yangu nimeona haya, Je ndiyo Kuchemsha au mwanzo wa Kuchemsha?

1.Maji nikiweka yemejaa Mpaka Juu, nikiwasha gari baada ya muda nikazima nakufungua Radiotor naona maji hayaonekani.

2.Nimetembea na gari Umbali wa kama 5KM, nikafungua Bonet, natazama tena kwenye Mfuniko wa Radiator nasikia ile mfoko wa "fuuuuu" na mvuke kiasi unatoka.

Naomba msaada tafadhali kujua shida kama ipo hapa.

JituMirabaMinne.

Ahsanteni.
Linachemsha hilo wahi kwa fundi!
 
Kama inakuteza kuchemsah mnk hata ujataja aina ya gar yenyewe bas Kama inakusubumbua sna funga feni direct yaani kitendo Cha kuweka switch on bas feni inaanza kuzungusha apo Apo na mshale hauwezi kupanda ovyo na itasahau maswala ya kuchemsha kwa gari ikiwa unatka kufany hvyo mtafute fundi waya afunge feni direct gari haiwez kuchemsha ovyo ovyo
mkuu hii haina madhara kwenye feni? kuna mtu niliwahi msikia akisema kuna vibrush kwenye mota ya feni huwa vinawahi kusagika mapema kama itakuwa inafanya kazi mara tu uwakapo switch on sasa sijui hii kama ni kweli au uongo
 
Unachotakiwa kujua ni je head gasket ina leakage au la..kitu cha kwanza ni kuweka hayo maji au coolant halafu haufungi mfuniko wa radiator halafu unawasha gari wakati mfuniko upo wazi unachezea throttle ile kwa ku rev ukiona maji yanatoa mapovu na yanapanda juu kwenye radiator jua chuma kinachemsha
 
Unachotakiwa kujua ni je head gasket ina leakage au la..kitu cha kwanza ni kuweka hayo maji au coolant halafu haufungi mfuniko wa radiator halafu unawasha gari wakati mfuniko upo wazi unachezea throttle ile kwa ku rev ukiona maji yanatoa mapovu na yanapanda juu kwenye radiator jua chuma kinachemsha
Ahsante kwa Elimu.
Ila tafadhali ufafanuzi zaidi, inatakiwa yasionekane Maji kabisa, maana huwa maji siyoni kwa macho ya kawaida?

Concern yangu nyingine ni kuwa je Maji napaswa kuyaona pale juu au hata nisipoyaona kwa Macho ni sawa? Naomba msaada Maelezo ya Kina maana napata Knowledge hapa Mkuu!
 
Una watu wanakutegemea?

Maana ni kama umejichoka hivi.

Hivi unaendeshaje gari na kwenda kufungua mfuniko wa Radiator?

Kuchemsha kwa gari unaangalia kwenye dashboard na siyo huko kwenye engine.
Anataka apake karolite
 
Ahsante kwa Elimu.
Ila tafadhali ufafanuzi zaidi, inatakiwa yasionekane Maji kabisa, maana huwa maji siyoni kwa macho ya kawaida?

Concern yangu nyingine ni kuwa je Maji napaswa kuyaona pale juu au hata nisipoyaona kwa Macho ni sawa? Naomba msaada Maelezo ya Kina maana napata Knowledge hapa Mkuu!
Maji yanatakiwa yaonekane kimtindo maana unapokua una rev maji yanakua yanazunguka kwenye vile vinjia vyake kwaionwalau unatakiwa uyaone yakiwa yanapita kama ukiweka maji ila haujayoni kuna possibility kubwa ya leakage kwenye cooling system mimi niliwahi kutumia gari nikiweka coolant asubuhi nikienda mizunguko maji yanapungua nikajakufanya uchunguzi nikakuta kwenye oil cooler kuna kutu na hio kutu inasababisha hewa kupita na maji yanatoka kwaio kukiwa na joto yanapotea unatumia gari yenye engine gani mkuu?
 
Maji yanatakiwa yaonekane kimtindo maana unapokua una rev maji yanakua yanazunguka kwenye vile vinjia vyake kwaionwalau unatakiwa uyaone yakiwa yanapita kama ukiweka maji ila haujayoni kuna possibility kubwa ya leakage kwenye cooling system mimi niliwahi kutumia gari nikiweka coolant asubuhi nikienda mizunguko maji yanapungua nikajakufanya uchunguzi nikakuta kwenye oil cooler kuna kutu na hio kutu inasababisha hewa kupita na maji yanatoka kwaio kukiwa na joto yanapotea unatumia gari yenye engine gani mkuu?
Ni IST CC1500 Mkuu.
 
Habari ya Majukumu humu Ndani.

Naomba kusaidiwa hiyo hoja. Je, nitajuaje gari yangu inachemsha?

Gari yangu nimeona haya, Je ndiyo Kuchemsha au mwanzo wa Kuchemsha?

1.Maji nikiweka yemejaa Mpaka Juu, nikiwasha gari baada ya muda nikazima nakufungua Radiotor naona maji hayaonekani.

2.Nimetembea na gari Umbali wa kama 5KM, nikafungua Bonet, natazama tena kwenye Mfuniko wa Radiator nasikia ile mfoko wa "fuuuuu" na mvuke kiasi unatoka.

Naomba msaada tafadhali kujua shida kama ipo hapa.

JituMirabaMinne.

Ahsanteni.
gari yako aina gani mzee?
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom