Nissan Ad Van 2005

Ngisibara

JF-Expert Member
Jan 2, 2009
3,301
2,076
Wana JF naomba kuelimishwa kidogo kuhusu bei ya magari katika mtandao wa Tradecar view kabla sijamnunulia dada/shemeji yenu, katika pitapita yangu ndani ya mtandao kuna kitu kimenishangaza sana kwani nimegundua gari nyingi za Nissan Ad Van ni bei chini sana tena kama ya mwaka 2005 ina uzwa kwa US$ 447 (FOB price) na baada ya kuunganisha mahesabu yote ya Inspection fee, Insuarance na fleight charges nikapata CIF US$ 1847, nikatumia GariYangu.com kukokotoa mahesabu ya TRA ili kujua gharama halisi mpaka kulitoa nikawa nimepata US$ 3.222 ambayo ni sawa na Tsh 4,188,285.00, kiujumla bei hiyo ni chini ya bei ya pikipiki inayouzwa ndani ya mtandao huo kwa US$112, sasa nabaki kujiuliza kulikoni? kunanini ndani yake kwani ukiiangalia inavutia na engine inaonekana sio complicated kama BMW, Ningependa kumchukulia BMW lakini naogopa kwani nasikia Dar hawana mafundi na hata wangekuwapo hawana computerised diagnostic equipment kwa gari kama hizo, tafadhali wakuu mnipe mwanga kwa hilo
 
Watu watupu kama wewe mwenyewe. Mi ushauri wangu ni huu "Cheap is expensive" Akili kumkichwa mkubwa.
 
mkuu unatoka kwenye BMW all the way down to $447 NISSAN AD VAN??hapo katikati hujaona gari ingine yoyote kama x-trail hivi?rav 4?harrier?
BTW bmw bongo zipo nyingi tu na mafundi wapo,mji umejaa x5s kibao zinatengenezwa wapi??
 
Kaka kwa bei hiyo achana na hilo gari, uatadanganywa lakini ukweli unabaki palepale, aliyepanga bei anajua quality ya gari!! The higher the price the better the quality! Nissan hiyo hiyo inapatikana kwenye mitandao mingine kwa $4500 FOB.....

Kuhusu BMW anayesema hakuna mafundi ni nani? Ipeleke pale Diamond Motors au au CMC nadhani...ila kila unapoipeleka kwa diagnosis uwe na 100,000/= mambo ya ufundi hapo hayapo!!

Ukiacha hao...mafundi wapo kibao na yanatengenezeka, kama una hela sioni sababu ya nibi kuhofia..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom