Nisome nini ili niwe miongoni mwa "white hackers" hatari duniani kwenye suala la computer na mitandao kiujumla?

Nominee

JF-Expert Member
Sep 5, 2017
459
1,240
Habarini wakuu. Mimi ni kijana "age below 35". Napenda sana siku zijazo nije kuwa miongoni mwa watu wenye uwezo mkubwa wa kuamrisha internet kufanya kile ninachotaka. Hizi 'Search engines' zote kuanzia google hadi yahoo nizikosoe kwa namna moja ama nyingine. Hizi facebook, whatsap, instagram, tweeter etc nizivuruge kwa kuongeza vitu unique au nizikosoe kwa namna moja ama nyingine. Nisome course ipi ili nifanye hayo yote?.

NB: Mimi ni msomi wa kawaida tu (First degree holder).Bachelor of science with education "Chemistry+Biology".

Natanguliza shukrani.
 
We unaishi Afrika..hakikisha unakua mkulima mkubwa sana ndo kitu itakutoa..achana na mambo ya wazungu maana hayatakusaidia wewe wala kizazi chako,utajikuta unazama ulaya maisha yako yote na kuishi kama mtumwa tu
 
We unaishi Afrika..hakikisha unakua mkulima mkubwa sana ndo kitu itakutoa..achana na mambo ya wazungu maana hayatakusaidia wewe wala kizazi chako,utajikuta unazama ulaya maisha yako yote na kuishi kama mtumwa tu
Nitaishi Afrika na nitawekeza hapa.Afrika inajengwa na sisi wenyewe wa-Afrika.Nahitaji kuonyesha njia kuwa hata sisi tunaweza.
 
Kuwa hacker mzuri hauitaji usome hata... ni kitu ambacho kinakuwa ndani ya damu.. hacker wengi wa kusomea ni watupu sanaaaaa
Nahitaji tu kupata msingi.Baada ya hapo nitajiongeza mwenyewe kwa kupekua pekua makabrasha mbalimbali.Niko siriaz mkuu.Naamini kipaji ninacho
 
Sasa mkuu kuna usemi unasema "Hata m'buyu ulianza kama mchicha". Iko hivi kuhack kuingiza password tu hapo kuna kujifunza namna ya programming, codes writting na makolokolo kibao sio kipaji tu hapo kuna elimu kubwa kuweza kufanya hiyo hacking unayoitaka. U msomi fuata taratibu za ki elimu ndo njia rahisi zaid au tafuta mwl mtaan akufundishe ila itakua ghali na ngumu labda uwe Genius.
 
Sasa mkuu kuna usemi unasema "Hata m'buyu ulianza kama mchicha". Iko hivi kuhack kuingiza password tu hapo kuna kujifunza namna ya programming, codes writting na makolokolo kibao sio kipaji tu hapo kuna elimu kubwa kuweza kufanya hiyo hacking unayoitaka. U msomi fuata taratibu za ki elimu ndo njia rahisi zaid au tafuta mwl mtaan akufundishe ila itakua ghali na ngumu labda uwe Genius.
Ahsante sana kwa ushauri wako mzuri mkuu, nitaufanyia kazi. I'm a Genius indeed.Pia nina nia ya dhati ya kutimiza hili lengo.
 
Hauwezi kuwa haka mzuri kwa kupekua makabrasha mkuu, utapoteza mda wako bureee
Nisaidie basi maufundi/mbinu zote unazohisi zitanisaidia kutimiza lengo langu.Hizo ulizonitajia mwanzoni nazo nitazifanyia kazi
 
Google Kuna materials kibao kuhusu hacking. Ukiweza inalipa Sana ukifanya kazi as systems security analyst. Bidii yako tu Mkuu ya kusoma na kupractise.
 
Kipaji kinaendana na msingi mzuri.Huwezi kusema una kipaji cha kuogelea wakati hata kisima hujawahi kukiona.Nahitaji nipate tu japo basic info ili nikionyeshe hicho kipaji.
Habarini wakuu. Mimi ni kijana "age below 35".Napenda sana siku zijazo nije kuwa miongoni mwa watu wenye uwezo mkubwa wa kuamrisha internet kufanya kile ninachotaka. Hizi 'Search engines' zote kuanzia google hadi yahoo nizikosoe kwa namna moja ama nyingine.Hizi facebook,whatsap,instagram,tweeter etc nizivuruge kwa kuongeza vitu unique au nizikosoe kwa namna moja ama nyingine.Nisome course ipi ili nifanye hayo yote?.

NB:Mimi ni msomi wa kawaida tu(First degree holder).Bachelor of science with education "Chemistry+Biology".

Natanguliza shukrani.
Tafuta jinsi ilivotengenezwa,itakusaidia kuvuruga mfumo wake
 
Nisaidie basi maufundi/mbinu zote unazohisi zitanisaidia kutimiza lengo langu.Hizo ulizonitajia mwanzoni nazo nitazifanyia kazi
Kafanye kuzi chunguza kwanza system au mfomu unaotaka ku hack, uelewe namna unavyo fanya kazi in and out.. hapo unakuwa umemaliza kazi.. huwezi kupotea njia unayo pita kila siku, sana sana utagundua chocho za kukufikisha mapema ( hacking )
 
9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom