Nisiposema hili kwa siku kama ya leo, nitapasuka hata moyo

Nisiposema hili kwa siku kama ya leo, nitapasuka hata moyo

Mopak

JF-Expert Member
Joined
Sep 19, 2024
Posts
1,719
Reaction score
3,574
JF wote wanajua kila kitu ni sawa. JF wote ni washauri wa kuanzia siasa, uchumi, michezo nk, jf wengi wanajiweza, its ok, JF wote ni mapro kwa kila sector, thats good.

=======
Kwa kawaida, mtu anayependa kusaidia huanzia kwa watu wake wa karibu kwanza kabla ya kuja JF kutoa ushauri wa namna mambo yanavyopaswa kufanyika. Kama kweli mnayosema ni sahihi, leo natamani kuona mtu akisimama hapa na kusema amewahi kumsaidia ndugu au rafiki yake akafanikiwa kupitia njia anayoishauri.

Kinachoshangaza ni kuona baadhi ya watu wakija hapa kueleza matatizo ya magari yao ilhali hata gari hawana. Mtu anakwambia viwanja vyote bora vya kula bata, lakini nyumbani kwao hali ni ngumu kiasi kwamba hata mahitaji ya msingi hayapatikani kwa urahisi. Tuache misifa na kujionyesha kusikokuwa na uhalisia.

Wengine mpo mjini mkijifanya maisha yamekaa sawa, wakati familia zenu vijijini zinategemea vibarua vya mashambani ili kupata chakula cha siku. Wapo pia wanaotumia Wi-Fi za watu wengine na kujenga picha ya maisha ya kifahari mtandaoni, wakisimulia kuhusu magari na vitu ambavyo havipo katika maisha yao halisi. Acheni ulimbukeni; tuwe wakweli kuhusu hali zetu. Na kabla mtu hajahisi kuguswa, niseme wazi tu kwamba sijamtaja mtu yeyote.​
 
Jf usiichukulie siriazi mwanetu,mbona utakuwa na stress na watu fake.

Fake I'D,fake life.
na ni ukweli lakini kuna haja gani kufake kila kitu ambacho hata karibia familia yenu nzima hawana mtoto wetu. Anaweza kukuambia kuwa marekani watu wanaishi hivi na hivi na yupo iringa kule hata mwanza mjin hajawahi kufka lakin life ya watu wa dar anaijua yote
 
1. Wanaume humu wote matajiri
2. Hawautaki broke women na hawajawahi kumiliki pisi maskini
3. Wote wanamiliki na wameoa bikra
4. Wote Wana vibesi ndani ya nyumba
5. Wanaume humu wote wako nje ya nchi
6. Wanamiliki magari makali makali
7 Hawajawahi kudate wala kumiliki single mama.
8. Mapenzi hayawayumbishi
9. Wengi humu account zinasoma kuanzia million hamsini kupanda juu
10. Wana akili na gpa kali
 
JF wote wanajua kila kitu ni sawa. JF wote ni washauri wa kuanzia siasa, uchumi, michezo nk, jf wengi wanajiweza, its ok, JF wote ni mapro kwa kila sector, thats good.

=======
Kwa kawaida, mtu anayependa kusaidia huanzia kwa watu wake wa karibu kwanza kabla ya kuja JF kutoa ushauri wa namna mambo yanavyopaswa kufanyika. Kama kweli mnayosema ni sahihi, leo natamani kuona mtu akisimama hapa na kusema amewahi kumsaidia ndugu au rafiki yake akafanikiwa kupitia njia anayoishauri.

Kinachoshangaza ni kuona baadhi ya watu wakija hapa kueleza matatizo ya magari yao ilhali hata gari hawana. Mtu anakwambia viwanja vyote bora vya kula bata, lakini nyumbani kwao hali ni ngumu kiasi kwamba hata mahitaji ya msingi hayapatikani kwa urahisi. Tuache misifa na kujionyesha kusikokuwa na uhalisia.

Wengine mpo mjini mkijifanya maisha yamekaa sawa, wakati familia zenu vijijini zinategemea vibarua vya mashambani ili kupata chakula cha siku. Wapo pia wanaotumia Wi-Fi za watu wengine na kujenga picha ya maisha ya kifahari mtandaoni, wakisimulia kuhusu magari na vitu ambavyo havipo katika maisha yao halisi. Acheni ulimbukeni; tuwe wakweli kuhusu hali zetu. Na kabla mtu hajahisi kuguswa, niseme wazi tu kwamba sijamtaja mtu yeyote.​
Umejuaje haya wakati JF wanatumia ID fake?
 
1. Wanaume humu wote matajiri
2. Hawautaki broke women na hawajawahi kumiliki pisi maskini
3. Wote wanamiliki na wameoa bikra
4. Wote Wana vibesi ndani ya nyumba
5. Wanaume humu wote wako nje ya nchi
6. Wanamiliki magari makali makali
7 Hawajawahi kudate wala kumiliki single mama.
8. Mapenzi hayawayumbishi
9. Wengi humu account zinasoma kuanzia million hamsini kupanda juu
10. Wana akili na gpa kali
Tuko perfect kwenye kila angle
 
na ni ukweli lakini kuna haja gani kufake kila kitu ambacho hata karibia familia yenu nzima hawana mtoto wetu. Anaweza kukuambia kuwa marekani watu wanaishi hivi na hivi na yupo iringa kule hata mwanza mjin hajawahi kufka lakin life ya watu wa dar anaijua yote
Mtu kama huyo ni wakuonewa huruma,maana anatamani na hapati,na hajui atavipataje.
 
Back
Top Bottom