Nisikilizeni CHADEMA: Tatizo ni UKAWA, Hili ndilo chaguo langu la rais wa 5

Ni kweli kuwaachia CUF au NCCR lakini unadhani ni yupi atasimama watu wakavutika labda kama mnataka wabunge nao tupoteze fikirini mara mbili jamani Lipumba au Mbatia? Sijui!!
 
Chadema wanachekesha,hivi hawajui Lipumba anaivuruga Ukawa makusudi.?
Lipumba ameshahongwa pesa nyingi sana na JK aivuruge Ukawa. Lipumba sio mjinga ,anajua wazi kabisa hawezi kushinda uchaguzi, Anachofanya ni kuivuruga tu Ukawa
 
Hayo ni Mawazo Mazuri sana!; Ambayo ni Nccr na Nld tu, Wanaweza Kuyaafiki!; Cuf hawawezi kuyaafiki! Hivyo basi wapelekee hii Ajenda kwa walio Tayari, kwa ajili ya utekelezaji! Muda si rafiki tena kwa kusubiri!

Kamwe Lipumba hawezi kukubali kumwachia Slaa agombee Urais, Ameshakula hela za ccm.., subiri hiyo tarehe 25 watapiga tu dana dana ili kuwakatisha tamaa Ukawa,, Hakuna maamuzi yoyote watakayofanya. Teh trh teh,, Huu mvurugano umepangwa kiustadi sana na ccm.. Chadema wameingia kwenye mtego
 
Chadema wanachekesha,hivi hawajui Lipumba anaivuruga Ukawa makusudi.?
Lipumba ameshahongwa pesa nyingi sana na JK aivuruge Ukawa. Lipumba sio mjinga ,anajua wazi kabisa hawezi kushinda uchaguzi, Anachofanya ni kuivuruga tu Ukawa
Kumbe unalijua hilo kua chama chako nichakuhonga honga?
 
Mkuu unaweza kuwa sahihi kwa upande mmoja lakini kwa upande wa pili usiwe sahihi

Kama kwa namna yoyote ile cuf wanajaribu kwa makusudi mazima kuchelewesha na kuja kuukwamisha ukawa hapo mbeleni basi mada yako itakua na mantiki kubwa sana

Lakini kama mantiki yako ni ukubwa wa cdm na hawakuhitaji ukawa kufanikisha malengo yao hapo utakua unakosea sana

Kimahesabu ni majimbo mangapi ambayo ukijumlisha kura za wapinza na jumla ya kura alizoshinda mgombea wa ccm na ikawa kura za wapinzani ni nyingi ndio utajua hoja yako inakosa mantiki
Na ukichukua kura za Dr na Prof ukizijumlisha pamoja unaweza kuona ni jinsi gani ushirikiano huu unaweza kuwa na mntiki kubwa zaidi kuliko wakienda mmoja mmoja kivyake

Mnapotaka kushirikiana na mmoja akaanza kujiona yeye ni muhimu kuliko mwenzake basi hapo hakuna ushirikiano tena
 
Kamwe Lipumba hawezi kukubali kumwachia Slaa agombee Urais, Ameshakula hela za ccm.., subiri hiyo tarehe 25 watapiga tu dana dana ili kuwakatisha tamaa Ukawa,, Hakuna maamuzi yoyote watakayofanya. Teh trh teh,, Huu mvurugano umepangwa kiustadi sana na ccm.. Chadema wameingia kwenye mtego


Swali ni CDM watafanya nini?
 
Mkuu M.M Mwanakijiji, mimi nadhani huyu jamaa wa CUF hajaelewa vizuri siasa zinavyokwenda kwa sasa hivi. Uimara wa CUF anaoongelea kwa upande wa huku bara ni upi? Pamoja na ujio wa ACT bado CHADEMA kimezidi kuimarika zaidi. Tena mimi nikiangalia kwa makini, ninaona kama kufukuzwa kwa Zitto Kabwe na genge lake kumeifanya CHADEMA iwe imara zaidi kuliko kipindi kile walipokuwemo CHADEMA. Utagundua kuwa wakati Zitto Kabwe bado yuko CHADEMA na kundi lake, kulikuwa na CHADEMA mbili ndani ya chama kimoja. Kufukuzwa kwa Zitto Kabwe a.k.a Supreme Leader au Ayatollaaah na genge lake kumeifanya CHADEMA ibaki na viongozi ama wanachama ambao ni waaminifu na wafia chama. Zitto Kabwe na genge lake walipofukuzwa CHADEMA, waliondoka na wale watu wote ambao walikuwepo CHADEMA si kwa sababu ya kuamini katika itikadi, falsafa na sera za CHADEMA, bali katika mtu binafsi ambaye ni Zitto Kabwe. Na kwa sehemu kubwa Zitto Kabwe alitumia muda wake mwingi kujijenga yeye binafsi kuliko kujenga chama.

Aidha, kitu kinachoipa nguvu CHADEMA sasa hivi, ni kujijenga kitaasisi zaidi na kutokutegemea sana viongozi wakuu au watu maarufu katika kuendesha mambo yao ikiwemo mikutano ya hadhara, na ufunguzi wa matawi. Ni kipindi hiki cha mwaka 2010-2015 ambacho tumeshuhudia CHADEMA ikijipanua zaidi kutoka mijini hadi vijijini, na kuanza kujenga mashina na matawi katika ngazi za chini kabisa kule vijijini. Hali hii imeifanya CHADEMA ianze kung'oa ile mizizi ya mashina vijijini ambayo ilikuwa inategemewa sana na CCM nyakati za uchaguzi. Kutokana na mambo kama hayo tunashuhudia CHADEMA, angalau kwa mwaka huu imekuwa na watia nia wengi sana tofauti na miaka ya nyuma. Mfano, juzi niliona kwenye tovuti yao watia nia wa Ubunge wakiwa wanafika takribani 900, na bado wanaendelea kuchukua fomu. Mwaka 2010 ambapo CHADEMA ilifanya vizuri idadi ya wagombea wa Ubunge ilikuwa 186 tu. Ina maana hawakusimamisha wagombea wa Ubunge majimbo yote, achilia mbali watu waliorubuniwa. Kwa mara ya kwanza CHADEMA wataenda kufanya kura za maoni km CCM ili kupata wagombea wa Ubunge na Udiwani nchi nzima.

Kwa maana hiyo, mwaka huu haturajii CCM wapite bila kupingwa katika majimbo yote, labda kutokee mapingamizi ya kisheria zaidi. Sasa hao CUF anaosema wako imara, bado msemaji wao alikuwa anahamasisha watu waendelee kuchukua form za kugombea. Majimbo mengi hawataweza kusimamisha wagombea wa nafasi za Ubunge na Udiwani. Mimi bado ninaamini CHADEMA wameshafanya harakati za kutosha sana mijini na vijijini. Uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka jana ulitupa picha kidogo tu ya matokeo halisi ya mwaka huu. Ndio maana binafsi ninaungana na ushauri wako ulioutoa kwa sababu CHADEMA wasipokuwa makini watapoteza zaidi kwa kujifunga katika zimwi hili la UKAWA, ilhali wana uwezo wa kusonga mbele.

Kuhusu ACT uimara wake ni wa bahati nasibu na kufikirika zaidi kuliko uhalisia. Kama ACT wataanza kutegemea zaidi wabunge wa CCM ambao wataachwa kwenye kura za maoni lazima tuhoji uimara wao. Hayo ni makosa ambayo CHADEMA walikuwa wanayafanya huko nyuma, mfano tuliona John Shibuda alivyowasumbua CHADEMA. Pia, wagombea wengi wa CCM kwa mwaka huu wanaweza wasiwe na mvuto wa kuchagulika sana na wapiga kura. Wengi wao wataangushwa mwaka huu kwa sbb wananchi wamewachoka kutokana na style yao ndiooooooo! bungeni na wanahitaji mabadiliko. Kuwachukua wagombea kama hawo kunaweza kusiwe na maana sana katika kujenga chama imara. Isipokuwa, wale wagombea ambao wataamua wenyewe kuhama kwa hiari kabla ya kura za maoni.

Umeongea vyema sana, hongera.
 
Kamwe Lipumba hawezi kukubali kumwachia Slaa agombee Urais, Ameshakula hela za ccm.., subiri hiyo tarehe 25 watapiga tu dana dana ili kuwakatisha tamaa Ukawa,, Hakuna maamuzi yoyote watakayofanya. Teh trh teh,, Huu mvurugano umepangwa kiustadi sana na ccm.. Chadema wameingia kwenye mtego

Let me assure you CDM will break through this na kila jicho halitaamini...,

Some of us are determined and have set the course none shall make it different!
 
Mzee Mwanakijiji ktk vita MTU kma wwe huchelei kuitwa mhaini huu ni muda wa watu kuwa wamoja na sio kukatishana tamaa. Ukawa km ukawa wana nafas kubwa ya kushinda ni kuwasihi tu waache ubinafsi muungano huu ni muhim na mbowe pamoja na wanacdm wengine wameyajua haya sio kweli cdm in chama kinakubalika kanda zote LA hasha, Bali yapo maeneo ambayo yana kura nyingi kwa vyama vingine washirika na ccm ndio wanataka mfarakano wafanikiwe.

Ccm kwa sasa anatafuta turufu kubwa kwa hali na Mali na hana jinsi zaidi ya kutumia turufu ya udini (uislam na ukristo) hii unajua madhara yake hasa kwa taifa ambalo liko nusu kwa nusu na kura zote hzo zinahitajika. Na ukweli ni kwamba ukawa tu ndio wanaoushawishi wa kufanya hayo. Uwepo wa cuf na cdm ni alama kubwa na tosha ya kuua propaganda ya udini ambyo tukubali tukatae vyama hivi vinaonekana kusmamia pande flani za kidini kwa maono ya watu wengi sana. Hvo huna sababu ya kuona cdm anaweza kusmama peke , mathalan kama umemqoute lipumba kwa kuwaambia masheikh hakuna jinsi kwa 2010 kwa kumsaidia kikwete basi kama mtamuacha sa hv atatumia mbinu hyo hyo je huoni kama ana ushawishi kwa jamii Fulani.

Ukawa ni muhimu sasa kwa kuwa wanapambana na magufuli. Huyu ni kiongozi ambaye sio mwepesi mwepesi ana nguvu na anatajuka kwa wannachi sote ni mashahidi jamani na jua fika cdm katika moja ya ngome zake imara ni kanda ya ziwa na ujio was magufuli unaenda kugawa hyo kanda hakuna jinsi, na inafahamika kuwa kanda ya ziwa ina kura nyingi na hamasa za kikabila lzma zichukue nafas hizo ndio ghilba za ccm. Je? Huoni umuhimu wa kuungana utasaidia kucover kanda ya ziwa. Mathalani vyama washirika wana nguvu kanda ya kusini, magharibi,pwani na visiwani je kanda kama hzi kuwa moja huoni hata nguvu ya magufuli achukue kanda ya ziwa yote bado itakuwa imekula kwa ccm?

Ccm iko scattered kwa sasa i.e lowassa team na nguvu pekee ya upinzani ambao umejenga imani kwwenye katiba na sasa uchaguzi ndio sulihisho kuna wanachama wengi na wapigakura hawajielewi lkn nguvu ya umoja utasomba sana hizo undecided vote hasa zile kura 20m.

LA mwisho na la msingi Mzee mwanakijiji we haupo field unatanguliza sana hisia baadala ya ukweli kaka acha fununu fununu hawa akina mbowe c wapumbavu kuona hakuna njia mbadala zaidi ya umoja huuu na ukweli ni kwamba ccm ni mwamba mgumu bila ya haya kwa ghilba zao hakuendeki.

Cdm ni chama chenye wafuasi wengi na ushawishi kwa upinzani lkn bila ukawa nchi hii ni kitendawili, nawasihi wanaukawa wamentain umoja wao na kuomba wasiwe vipande vipande, mtafika ccm furaha yao ni kupasuka kwenu maana hata waliondani na wanataka kutoka wanaangalia nguvu yenu kwanza.
 
Last edited by a moderator:

Afadhali wewe umeona mbali kidogo!
CHADEMA haina turufu hata moja ya kuviburuza vyama vingine vinavyounda UKAWA kwasababu uwanja wa kisiasa nchini, 2015, ni tofauti sana na ule wa2010 na hata ikisema isimame yenyewe ni wazi kuwa ina mengi ya kupoteza kuliko kufaidika (haitaki shahada ya uzamili kuliona hili!)
CUF inaogopa kupoteza maslahi yake, endapo haitaweka mgombea, na kwakua CHADEMA imechukua majimbo mengi ya Ubunge kwanini isiwaachie NCCR au CUF kusimamisha mgombea uraus?
KWA KIFUPI, NAFIKIRI ULE MUDA WA KUMWAGA UGALI NA MBOGA UMEFIKA, KAMA SIO CHADEMA KUJIREKEBISHA NA KUHESHIMU VYAMA VINGINE NDANI YA UKAWA!



















Sijui kama wenzetu hata mnaangalia haya mambo kwa kina kinachostahili. Kwanza, hakuna mgombea wa "UKAWA" kwa sababu moja tu nimeeleza huko juu; UKAWA siyo chama cha siasa na hakina uwezo au hata haki ya kusimamisha mgombea yeyote hata wa kijiji. Mgombea wa Urais atatoka kwenye chama; na kwa vile Rais wa Tanzania ni mtendaji hawezi kutoka tu alimradi ametoka kwenye chama chochote. Rais lazima atoke kwenye chama ambacho kinaonekana kwa kiasi kikubwa kukubaliwa na wananchi wengi zaidi na ambacho sera zake zinakubaliwa na wananchi wengi (hili linaonekana kwenye uchaguzi). Sasa ukimchukua mgombea kutoka NLD au NCCR unafanya kwa msingi gani? Kwamba " kwa vile wenzetu wamesimamisha wagombea wengi basi na sisi tupewe Urais? Hivi ndivyo mnavyoona?

Lakini kubwa zaidi ambalo hamtaki hata kulipa nafasi ni ukweli kuwa Rais anatawala akisimamishwa na Chama cha Siasa. Sasa ukiwa na RAis ambaye chama chake kina wabunge watano tu; halafu chama kingine kina wabunge hamsingi au mia; huyo Rais atasimamiwa na chama gani? Atajadiliana na chama gani? Si unajikuta unamlazimisha kutokuwa huru kutekeleza sera. Vipi akiamua kutekeleza sera za chama chake kidogo utamwajibisha vipi?
 

Cdm ni chama chenye wafuasi wengi na ushawishi kwa upinzani lkn bila ukawa nchi hii ni kitendawili, nawasihi wanaukawa wamentain umoja wao na kuomba wasiwe vipande vipande, mtafika ccm furaha yao ni kupasuka kwenu maana hata waliondani na wanataka kutoka wanaangalia nguvu yenu kwanza.

Hivi hata kabla sijakujibu labda unisaidie jambo moja. Ni kwanini unafikiria UKAWA ni Muungano wa vyama vya upinzani Tanzania au inawakilisha "Umoja" wa vyama vya upinzani? Maana hayo mengine yote unayasema inaonekana yamejengwa katika msingi potofu - kwamba UKAWA ni umoja wa vyama vya upinzani.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Kimahesabu ni majimbo mangapi ambayo ukijumlisha kura za wapinza na jumla ya kura alizoshinda mgombea wa ccm na ikawa kura za wapinzani ni nyingi ndio utajua hoja yako inakosa mantiki
Na ukichukua kura za Dr na Prof ukizijumlisha pamoja unaweza kuona ni jinsi gani ushirikiano huu unaweza kuwa na mntiki kubwa zaidi kuliko wakienda mmoja mmoja kivyake

Mnapotaka kushirikiana na mmoja akaanza kujiona yeye ni muhimu kuliko mwenzake basi hapo hakuna ushirikiano tena

Unajua Lipumba alipata kura ngapi 2010 kulinganisha na kura alizopata 2005 na kwanini?
 
Hivi hata kabla sijakujibu labda unisaidie jambo moja. Ni kwanini unafikiria UKAWA ni Muungano wa vyama vya upinzani Tanzania au inawakilisha "Umoja" wa vyama vya upinzani? Maana hayo mengine yote unayasema inaonekana yamejengwa katika msingi potofu - kwamba UKAWA ni umoja wa vyama vya upinzani.

Kama unachukulia ukawa kwa muktadha unaotaka ww ni umoja wa katiba ya wananchi lkn kma tutachukua kwa dhamira nzr basi ukawa utakuwa kwa umoja wa vyama vya upinzani tanzania. Hoja ndio za kujadili na lzma tukubali ukweli kuwa mwenyekiti na associates wake hawakukosea kuingiza cdm ukawa wao wako kwenye field na wanajua zaidi nini umuhim wa huo unaoitwa umoja.
 
CUF wabinafsi sana, tamaa za wanachama wa CUF zinazoofisha UKAWA
Ata wakjitoa watz tutawaona hawakua na lengo la dhati ktk kuleta mabadiliko nchi....

Naiman wabunge wa CDM watazidi kuwa wengi zaid mwaka huu
 
Back
Top Bottom