Nishauri Kwa nini Nirudi Kuishi Tanzania?

Mtanganyika

JF-Expert Member
Jul 18, 2007
1,601
945
Kushughulikia mafisadi ni kazi ngumu - Pinda

2008-04-10 10:35:14
Na Joseph Mwendapole na John Ngunge, Dodoma


Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda, amesema kuwashughulikia mafisadi ni kazi ngumu inayohitaji umakini wa hali ya juu.

Aliyasema hayo mjini Dodoma jana wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu masuala mbalimbali.

Bw. Pinda alikuwa akijibu swali aliloulizwa namna anavyowashughulikia waliohusika na wizi katika akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya BoT.

Alitetea uamuzi wa serikali wa kuendelea kupokea fedha zinazorejeshwa na mafisadi hao bila kuwataja majina kuwa unamanufaa makubwa.

Aidha, alisema serikali inachotaka kwa sasa ni fedha na kwamba baada ya hapo ndipo itaangalia namna ya kuwashtaki waliohusika.

Alisema hata majina yao yatatangazwa baada ya shughuli ya kurejesha fedha hizo na uchunguzi kukamilika.

``Usipojipanga vizuri unaweza kukurupuka kuwashtaki na wakakushinda, hivyo utapoteza vyote, kesi umeshindwa na fedha hujapata, sasa serikali kwanza inaona cha muhimu ni kupata fedha zake, mambo mengine baadae,`` alisisitiza Bw. Pinda.

Alisisitiza kuwa kutaja majina ya waliochota fedha hizo ni kuvuruga uchunguzi unaoendelea.

Alisema hata yeye binafsi ana shauku ya kujua majina ya watu waliohusika katika sakata hilo lakini aliomba wananchi kuendelea kuvuta subira.

Bw. Pinda alisema atajitahidi kwenda na kasi aliyokuwa nayo Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Bw. Edward Lowassa.

Alimsifu Bw. Lowassa kuwa alikuwa na kasi kubwa katika kusukuma mambo mbele na kwamba atajitahidi kufuata nyayo hizo.

``Na ndiyo maana nimemua kubaki na watu waliokuwa karibu na Bw. Lowassa ili wanisaidie kazi, wao wanajua mipango yote, watanisaidia kusonga mbele. Sitaki kuanza upya,`` alisema.


Pinda: Govt mulls measures against Richmond culprits

2008-04-10 10:05:15
By Lydia Shekighenda, Dodoma


Prime Minister Mizengo Pinda yesterday appealed for more patience as the government considered appropriate disciplinary measures to be taken against senior government officials implicated in the Richmond corruption scandal.

The officials include Attorney General Johson Mwanyika and Prevention and Combating of Corruption Bureau (PCCB) Director General Edward Hosea.

The premier, who was responding to calls for resignation of all those linked to the scam at a press conference here, said the government needed patience in dealing with ``the complicated and complex`` scandal.

``Resignation of these officials may not be a solution to corruption problems in state organs.``

Spika akasirika

Habari Zinazoshabihiana
• Wabunge waanza kufundishwa sheria 15.08.2006 [Soma]
• Zitto akana kulikejeli Bunge, Spika 01.01.2008 [Soma]
• Cheyo awasilisha ushahidi kwa Spika 14.07.2006 [Soma]

*Awajia juu wanaomzushia tuhuma kumchafua
*Asikitishwa bintiye kuandikiwa SMS chafu
*Rostam Aziz leo kuwekwa kitimoto bungeni

Na John Daniel, Dodoma

SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Bw. Samwel Sitta, amewajia juu wanaomzushia tuhuma na kuwaita kuwa ni wanasiasa wa kiwango cha chini na majitaka huku akiwahakikishia wabunge kwamba ataendelea kuendesha Bunge kwa kasi na spidi inayotakiwa kwa maslahi ya Taifa bila kurudi nyuma.

Spika ambaye alionesha wazi kuhuzunishwa na tuhuma hizo, aliwapasha wabaya wake hao kuwa yuko tayari kujibu mashambulizi yoyote watakayoelekeza kwake, kwa kuwa ana uwezo wa kufanya hivyo.

Akizungumza muda mfupi baada ya muda wa maswali na majibu kumalizika bungeni jana, Bw. Sitta aliwataka watu hao kuacha mara moja kuwashambulia watoto wake na kuwajulisha rasmi kwamba aliyewakosea ni yeye na si Watoto wake, hivyo hakuna sababu ya kuwasumbua kwa maneno machafu kama walivyofanya kwa kumtumia ujumbe bintiye ambaye ameolewa.

"Waheshimiwa wabunge napenda kutumia nafasi hii kuwashukuru wote walionipa pole kwa yale yanayonipata, hata hivyo napenda kuwahakikishia kwamba nitaendelea kuimarisha Bunge hadi hatua inayotakiwa, hawa ni wanasiasa wa kiwango cha chini, ni wanasiasa wa majitaka," alisema Bw. Sitta na kuongeza:

"Ninachowaomba tafadhali wasishambulie Watoto wangu, binti yangu aliyeolewa anatumiwa meseji chafu, wanishambulie mimi, mimi ndiye nimewakosea si watoto wangu, ila niwahakikishie tu kwamba nina uwezo wa kuyakabili vizuri," alisema Bw. Sitta.

Conclusion:
Kila ninapojaribu kuperuzi news za Tanzania ni vioja juu ya vioja, scandal juu ya scandal. Sasa swali ni moja tuu, jee ni kwanini walio ughaibuni warudi kuishi Tanzania? Nadhani huu ni muda wa kuchukua kinyago aka mkoba aka gamba la nchi uliyokuwepo. Kwani haito kuuma sana sababu hiyo nchi huna root nayo. Kurudi home unaweza jiingiza kwenye maamuzi mabaya bure, mfano kuingi msituni ukawa muasi.
 
Kwani unataka kuingia kwenye siasa?? Kama sio wewe rudi tuu..fungua kampuni yako huku feki au ya kweli..rudi bongo kama investor..uanze ulaji!!
 
Tanzania is land of oppatunities we rudi kama una viji $ tafuta na mzungu mmoja muwe partner mie ukija nitakuunganisha na top wa govt utachota mijihela zaidi ya EPA utakuwa tajiri kisha utaogopewa kufilisiwa, utashitakiwa tutacheza na mahakama kesi haitasikika mwisho itafutwa situtakuwa na pesa?we usikhofu njoo mzee tufanye mambo!
 
Kwani unataka kuingia kwenye siasa?? Kama sio wewe rudi tuu..fungua kampuni yako huku feki au ya kweli..rudi bongo kama investor..uanze ulaji!!

Nataka kuridi kama investor, lakini kama unakuja na mainvestor watakao wekeza kwenye dollar, kumbuka kuna kitu kinaitwa foreign exchange risk, pesa ya Tanzania in flactuate more than anything, haiko stable kwenye exchange market.Yaani kwa lugha raisi, naweza kuwekeza dolla 1000 leo, ni sawa na shilling 1,200,000 na nikapiga hesabu zangu kwamba nitapata return ya 10%, sawa na dolla 100. so mwisho wa siku nategemea kurudisha dolla 1100, lakini kama exchange rate itajump mpaka 1400tsh kwa one dolla, unajua how much nitapata? Dolla 945. Actual nimeloose money baada ya kugain money, that is the risk associate kuwekeza katika unstable currency.

Kuwekeza na political risk jee? Kama hupatani na CCM expect masive taxation kwenye kampuni yako, illegal alligations na mengine mengi sana.

Investment ni neno nyeti sana, nyumba zinapanda bei sababu ya speculator walio iba pesa za EPA, leo hii dar kuna nyumba ya 3 bedroom inayocost dolla 3000 kwa mwezi, sawa na bei nyumba ya kifahari kwenye hood ya Royal Oaks in uptown Dallas.

Watu wachache wameweza kuinfluance bidhaa nyeti kuwa na unrealistic price, kwa wale tunacheza na investment we call it bubble it just the matter of time litapasuka
 
Tanzania is land of oppatunities we rudi kama una viji $ tafuta na mzungu mmoja muwe partner mie ukija nitakuunganisha na top wa govt utachota mijihela zaidi ya EPA utakuwa tajiri kisha utaogopewa kufilisiwa, utashitakiwa tutacheza na mahakama kesi haitasikika mwisho itafutwa situtakuwa na pesa?we usikhofu njoo mzee tufanye mambo!

Sasa kiongozi wa government pia unaomba abaki kwenye kila serikali mpya ya CCM. Maana kama alikuwa mshikaji wako ni Pius Mangula na JK baada ya kuingia kamuweka Makamba, now tell me?

I think that is not a good idea, i wanna hear more
 
Sasa kiongozi wa government pia unaomba abaki kwenye kila serikali mpya ya CCM. Maana kama alikuwa mshikaji wako ni Pius Mangula na JK baada ya kuingia kamuweka Makamba, now tell me?

I think that is not a good idea, i wanna hear more

Ukiwa mjanja unaangalia upande gani wa mkate umepakwa siagi.Hamkumbuki ya mama zakhia megji?mwanzo hakuwa mwanamtandao lakini baadae akastukia deal na akaukwaa uwaziri wa fedha. Siasa za bongo hazina maadui wa muda mrefu wala marafiki wa muda mrefu unawakuna migongongo yao na wao wanakukuna mgongo wao.
 
Wewe kama unataka kurudi rudi ni maamuzi yako na akili yako.Sasa hata nikuambia urudi na wakati maamuzi yako ni kutokurudi huoni kama itakuwa ni upuuzi mtupu?.

Hapa kama huna akili ya huwezi ishi endelea kubeba box tu huko maswali mengine jijibu mwenyewe unatumalizia kurasa za JF
 
Sasa wewe kwa akili yako unadhani ni jukumu la nani kurekebisha hali iliyopo tanzania??? Yaani wewe unataka kuishi kwenye nyumba safi wakati huo huo hutaki kufanya usafi???
 
Sasa wewe kwa akili yako unadhani ni jukumu la nani kurekebisha hali iliyopo tanzania??? Yaani wewe unataka kuishi kwenye nyumba safi wakati huo huo hutaki kufanya usafi???

Nataka nyumba safi, lakini kama wapangaji wanaamani nyumba ni safi jee nitasafisha peke yangu?

I wanna walk that walk, but everybody talk that talk
 
Wewe kama unataka kurudi rudi ni maamuzi yako na akili yako.Sasa hata nikuambia urudi na wakati maamuzi yako ni kutokurudi huoni kama itakuwa ni upuuzi mtupu?.

Hapa kama huna akili ya huwezi ishi endelea kubeba box tu huko maswali mengine jijibu mwenyewe unatumalizia kurasa za JF

Wrong mentality kwamba kila aliye nje ya nchi ni mbeba box. As long as i can secure a bread and butter, and i have legal right of first ammendment then who cares what am i doing?
 
Nataka kuridi kama investor, lakini kama unakuja na mainvestor watakao wekeza kwenye dollar, kumbuka kuna kitu kinaitwa foreign exchange risk, pesa ya Tanzania in flactuate more than anything, haiko stable kwenye exchange market.Yaani kwa lugha raisi, naweza kuwekeza dolla 1000 leo, ni sawa na shilling 1,200,000 na nikapiga hesabu zangu kwamba nitapata return ya 10%, sawa na dolla 100. so mwisho wa siku nategemea kurudisha dolla 1100, lakini kama exchange rate itajump mpaka 1400tsh kwa one dolla, unajua how much nitapata? Dolla 945. Actual nimeloose money baada ya kugain money, that is the risk associate kuwekeza katika unstable currency.

Kuwekeza na political risk jee? Kama hupatani na CCM expect masive taxation kwenye kampuni yako, illegal alligations na mengine mengi sana.

Investment ni neno nyeti sana, nyumba zinapanda bei sababu ya speculator walio iba pesa za EPA, leo hii dar kuna nyumba ya 3 bedroom inayocost dolla 3000 kwa mwezi, sawa na bei nyumba ya kifahari kwenye hood ya Royal Oaks in uptown Dallas.

Watu wachache wameweza kuinfluance bidhaa nyeti kuwa na unrealistic price, kwa wale tunacheza na investment we call it bubble it just the matter of time litapasuka

Nikupe ushauri ndugu yangu kuhusu Exchange rate ni kuwa utaona kwenye biashara nyingi faida inapanda kutokana na exchange rate. Mfano mimi niko kwenye business ya trucks. Malipo yote yanafanyika kwa dollar. Dollar ikipanda thamani, mafuta yanapanda bei na matumizi pia yanapanda. Kwa kuwa nalipwa kwa dollar hiyo effect inaji cancel yenyewe.

Dollar ikishuka thamani, Na bei ya vitu inapungua. Profit haibadiliki sana kutokana na exchange rate. Sisemi uingie kwenye biashara ya Trucks ila jaribu kuingia kwenye biashara ambayo utalipwa kwa dollars. Pia mimi mishahara yote nalipa kwa dollar, kwenye account za dollar. Ikishuka thamani dollar wafanyakazi watajiju. Ikipanda pia heri kwao.
 
"Allah's Slave;172031]Nikupe ushauri ndugu yangu kuhusu Exchange rate ni kuwa utaona kwenye biashara nyingi faida inapanda kutokana na exchange rate. Mfano mimi niko kwenye business ya trucks. Malipo yote yanafanyika kwa dollar. Dollar ikipanda thamani, mafuta yanapanda bei na matumizi pia yanapanda. Kwa kuwa nalipwa kwa dollar hiyo effect inaji cancel yenyewe.

Dollar ikishuka thamani, Na bei ya vitu inapungua. Profit haibadiliki sana kutokana na exchange rate. Sisemi uingie kwenye biashara ya Trucks ila jaribu kuingia kwenye biashara ambayo utalipwa kwa dollars. Pia mimi mishahara yote nalipa kwa dollar, kwenye account za dollar. Ikishuka thamani dollar wafanyakazi watajiju. Ikipanda pia heri kwao."

LOL ..sawa boss..wats the name of 'YOUR' company again??
 
Mtanganyika, Do you really believe you have no reason to come back home? Do you really believe Tanzania is a wrong place for you in all walks of life? So you are convinced that you can not change the situation and you have nothing to contribute? So you feel that you have nothing to loose and you can live wherever you are peacefully and let whatever is happening there continue? Therefore you wish you were not born Tanzanian. Kama ni hivyo, don't come back, endelea kubeba ma-box. But Idon't want to believe umefikia hatua hiyo and perhaps thats why you call yourself Mtanganyika. Hebu acha mentality ya kitumwa hiyo! Tanzania is still one of the best places kuzidi hata huko mliko, nakushauri tu malizia mipango yako urudi home, our beautiful land!
 
mtanganyika rudi nyumbani bana wasikutishe mambo tambarare, mie nipo hapa najionea mwenyewe ! njoo twakusubiri !
 
mtanganyika rudi nyumbani bana wasikutishe mambo tambarare, mie nipo hapa najionea mwenyewe ! njoo twakusubiri !


Tumwambie ukweli ndugu yetu huyu. Kama unachannel rudi mambo yatakuwa tambarare kama huna Bongo ni kurudi kusalimia tu,
 
Mtanganyika,

Kule ni kwenu, ukikimbia moja kwa moja ndio furaha ya mafisadi. Hawataki
wanaojua na ambao hawako tayari kupakwa na uchafu wao. Wanafurahi kweli wengi wa watu wazuri wakizamia nje moja kwa moja.

Usiogope kurudi nyumbani, ila uwe tayari kwa mapambano. Kama unapandisha pressure basi anza kununua dawa toka siku unashuka maana utakutana na wafanyakazi wa serikali, TRA, na wajinga wengine wa serikali ambao wanajifanya wanajua kumbe ni Pumbavu namba moja.

Wakijua unajua haki zako, wanakuheshimu hata kama watakusema pembeni.
 
Tumwambie ukweli ndugu yetu huyu. Kama unachannel rudi mambo yatakuwa tambarare kama huna Bongo ni kurudi kusalimia tu,

nilisema vile sababu najua ntu kwao, na anayekataa kwao ntumwa ! yee arudi tu asiwe na wasi, kwani anasubiri akina nani wamjengee nchi then ndio arudi ?
 
Back
Top Bottom