Jhung tiao
Member
- Mar 27, 2012
- 82
- 15
Mimi ni kijana mwenye umri wa 27 mnamo mwaka 2010 nilikutana na binti ambaye nilitokea kumpenda sana, ila kwake ilikua ngumu kunielewa lengo langu, siku zilivo zidi kwenda akawa ananielewa, 2011 akaniambia hayuko tayari kushea sex kwan alikua chuo mpaka malengo yake yatime, kwangu haikua ngum kwani nilimpenda sana tukaendelea vizuri 2012 akahitimu cheti chake cha ualimu, kwa kipindi chote tulikua tunachati vizuri na mhudumia kadri ya uwezo wangu,baada ya kuhitimu mwaka jana akawa home kwao tuliendelea vizur bila mgegedo wowote nilijitahid kua mwaminifu sana coz yeye mwenye aliniambia bado yuko bikra so kama na malengo na yeye niwe mvumilivu, tatizo ilianza matokeo yalipo toka mwenzangu akapangiwa mwanza alipo ondoka nikawa nampa sapoti ya kifedha kidogo na mawasiliano yalikua mazuri ila baada ya miez miwili mambo yakabadilika nikipiga simu anakata then anatuma text nipo na wenzangu subiri nifike home ntakutafuta hii hali ikazidi ikaanza kunipa wasi wasi nikimuuliza inakuaje hupokei simu ukiwa na wenzako anakua mkali wakati mwingine nikimtext hajibu chochote nikimwambia neno I LOVE U anasema POA nikimuuliza inakuaje umebadilika anajibu kwani wewe UNAONAJE nikimuuliza nini tatizo hataki kuniambia anasema namchosha na maneno hayo hayo yani neno I LOVE U wakati mwingine anani-text I LOVE U DADY kweli na stress sana ilifika mahali nikamwambia tuachane kwenye simu alilia sana akesema nimempotezea mda na bado ananipenda sana nikarudisha moyo, lakina bado hiyo tabia inaendelea mpaka sasa nimemsaidia sana kwa kila kitu, kuna wakati naelewa kabisa yuko home alikopanga nikimpigia anapokea anaongea kidogo anakata nikipiga ana-text niko bize mara niko saloon siwezi ongea na simu mbele za watu sasa hii kitu inanitatiza sana maana usiku tu ndo huwa tunaweza ongea kuanzia saa tatu mpaka hata saa sita usiku na asubuhi huwa namuamsha mapema kwa kwenda kazini, yeye ni binti wa miaka 22 na maelezo yake nikuja kuishi na mimi coz nimemvumilia na mimi ndo chaguo lake na anataka niwe mwanaume wa kwanza kuutoa usichana wake jamani nipo njia panda naombeni msaada wenu na konda kwa mawazo kila siku niliomba nimtambulishe home kwetu akakataa kwamba yeye bado mdogo so nisuburi after 3 yrs atakua tayari coz anajipanga kwanza, wakati mwingine nikipiga simu anasema masikio yana muuma so tuongee baadae baada ya hapo nikimpigia simu yake inakua bize hata nusu saa nikimuuliza anasema anaongea namarafiki zake mara mama yake, jamani nisaidieni nifanyaje coz mimi mwenyewe niko mkoa mwingine na nampenda sana sijawahi saliti penzi lake hata cku moja na usiku ananihimiza sana kusali kabla ya kulala, na maswali mengi yasio na majibu kichwani mwangu. MSAADA NDUGU ZANGU