Nisaidieni nikoe ndoa hii.

tundatamu

Member
Nov 26, 2012
12
8
Jamani nina kaka angu ameishi na mwanamke mpaka wanawatoto wawili hajafunga ndoa, mwezi uliopita kaka akasema anataka kufunga ndoa na mkewe tukaenda kwao na wifi kutoa mahari. Juzi wifi kapata habari kuna dada ambaye ni x-girlfriend wa kaka anamimba ya kaka. wifi amekata tamaa siku mbili tu namuona amekonda nahisi ataondoka jamani wifi yangu nampenda hivi hata mama presha zimepanda kwa kile alichokifanya kaka baba yeye kamwambia tu kaka hilo balaa silitaki katika familia yangu,namtambua mke mmoja tuliyemtolea mahari hao malaya wako sitaki kuwasikia.wifi yangu ni mke jamani hata kaka aliwahi kukiri, alafu huyo mdada mwenye mimba ni mcharuko balaa. tumemuuliza kaka amekili alichofanya ila haonyeshi kujuta wala kumuhurumia mkewe na watoto anajibu jeuri na dharau kama hawezi kuvumilia mwache aende,aniachie watoto wangu.anafikiri akiondoka ndo atapata mwanaume mtakatifu.yaani huyu kaka kama kachanganyikiwa mpaka aibu mwezi uliopita tu tulipeleka mahari tukitegemea mwezi wa pili mwakani wafunge ndoa . tuwasaidieje hawa watu jamani wifi ni mcheshi lakini toka juzi hata haongei jana nimeshinda huko kwa kaka wifi hata kula shida.leo namuuliza kaka anajibu bado jeuri wifi yako atakufa kwa wivu usiku kakesha anafanya kazi kafua, kadeki kaosha vyombo,kanyoosha nguo mpaka asubuhi,atakuwa anajiandaa kwenda kwao.naona kaka hajui anachokifanya atapoteza mke.nisaidieni nimsaidie kaka angu.
 
ama kweli wewe wajua maana ya tundatamu. nakupenda manake wajua utamu wa tunda la mke mzuri alonalo kaka yako ingawa yeye halioni.

kwangu mm mkataa pema pabaya pana mwita, na waswahili husema mtoto akililia wembe mpe.

najua kaka yako anatumia nguvu ya kiume tu kwamba ni mwanaume kesha zaa hana jinsi, ni kweli kwani maji yakisha mwagika hayazoleki lkn amesahau kwamba anatakiwa kuyarekebisha makosa yake, kwa kumwonyesha mkewe kwamba anajuta alolifanya na yuo tayari kulirekenbisha kosa hili ili kulinda ndoa na penzi kwa mkewe.

wifi yako, anatakiwa aangalie kama mume hana mapenzi nae na wala hajali kama kakosea ni wazi ata akibaki atazidi kunyanyasika tu la msingi b4 its late aanze maisha mapya na Mungu atamasaidia. ni bora akaish alone pasi iyo ndoa kuliko kuish na cheater ambae hajutii wala haoni kama anakosea tena asiye thamani mapenzi ya mwenzie.
 
Last edited by a moderator:
Dawa chungu huwa inaponyesha. Mpe support huyo wifi yako, muambie unaheshimu maamuzi yake. Ila wifi yako angeondoka tu ili kakako ajifunze. Na kiboko cha Mungu hakipo mbali, ujue saa hizi kinainuliwa juu na kinashuka soon. Muache dada wa watu aondoke, nobody notices what you do unless you stop!
 
Dahh,...pole sana dada. Mpe pole wifi.

Hv, huyo ex-girlfriend si walishindwana na kuachana? Sasa iweje kaka aende KUM-MIMBA tena?

Mzungumze na huyo wifi kwa sababu akiondoka, watoto watayumba na kukosa mapenzi ya wazazi wawili.

Na huyo kaka yako aache ngede zake na akubali kosa, alaahh!
 
ndoa huwa ni ya wawili
nyie wngine ni washauri tu

wenye maamuzi ya kuendeleza ama kuvunja ndoa ni wao.

Kama mnatambua mchango wa wifi yenu msaidieni kukabialiana na kipindi anachokipitia sasa.
 
muulizeni kaka yenu msimamo wake ni upi msilazimishe mambo kwa sababu huo hautakuwa mwisho wa matatizo
 
Me naona hata kwenda kutoa mahari huyo kaka yenu mmemlazimisha ndio maana hajutii kitendo alicho kifanya, na ni dhahiri hampendi huo unaye muita ni wifi yako!

Pia uzuri wa hao wanawake ana wajua huyo kaka yako kwa hiyo muache afanye maamuzi, wewe unamuona malaya,mcharuko yeye ana muona ndio anafaa, ni bora muache achague mwenyewe baadae asije kuwalahumu nyinyi!

Ndoa si kitu cha mchezo,muacheni aoe anaye mpenda yeye!
 
Huyo kaka yako keshanasa, chakufanya hapo mwite uongee naye umsikie tatizo liko wapi vinginevyo ndo anatokomea hivyo!!!!!!! poleni
 
:a s 11::a s 11:
ama kweli wewe wajua maana ya tundatamu. Nakupenda manake wajua utamu wa tunda la mke mzuri alonalo kaka yako ingawa yeye halioni.

Kwangu mm mkataa pema pabaya pana mwita, na waswahili husema mtoto akililia wembe mpe.

Najua kaka yako anatumia nguvu ya kiume tu kwamba ni mwanaume kesha zaa hana jinsi, ni kweli kwani maji yakisha mwagika hayazoleki lkn amesahau kwamba anatakiwa kuyarekebisha makosa yake, kwa kumwonyesha mkewe kwamba anajuta alolifanya na yuo tayari kulirekenbisha kosa hili ili kulinda ndoa na penzi kwa mkewe.

Wifi yako, anatakiwa aangalie kama mume hana mapenzi nae na wala hajali kama kakosea ni wazi ata akibaki atazidi kunyanyasika tu la msingi b4 its late aanze maisha mapya na mungu atamasaidia. Ni bora akaish alone pasi iyo ndoa kuliko kuish na cheater ambae hajutii wala haoni kama anakosea tena asiye thamani mapenzi ya mwenzie.
 
Muache aondoke ili kaka yako akili zimsogelee.Kwa matendo kama haya wanaume tunaangushana kwa kweli.
 
Dawa chungu huwa
inaponyesha. Mpe support huyo wifi yako, muambie unaheshimu maamuzi
yake. Ila wifi yako angeondoka tu ili kakako ajifunze. Na kiboko cha
Mungu hakipo mbali, ujue saa hizi kinainuliwa juu na kinashuka soon.
Muache dada wa watu aondoke, nobody notices what you do unless you
stop!

i totaly agree with you,kuna mmoja aliamua kuondoka kwa mume na Mungu aliposhusha fimbo jamaa aliona dunia chungu.
 
Jamani nina kaka angu ameishi na mwanamke mpaka wanawatoto wawili hajafunga ndoa, mwezi uliopita kaka akasema anataka kufunga ndoa na mkewe tukaenda kwao na wifi kutoa mahari. Juzi wifi kapata habari kuna dada ambaye ni x-girlfriend wa kaka anamimba ya kaka. wifi amekata tamaa siku mbili tu namuona amekonda nahisi ataondoka jamani wifi yangu nampenda hivi hata mama presha zimepanda kwa kile alichokifanya kaka baba yeye kamwambia tu kaka hilo balaa silitaki katika familia yangu,namtambua mke mmoja tuliyemtolea mahari hao malaya wako sitaki kuwasikia.wifi yangu ni mke jamani hata kaka aliwahi kukiri, alafu huyo mdada mwenye mimba ni mcharuko balaa. tumemuuliza kaka amekili alichofanya ila haonyeshi kujuta wala kumuhurumia mkewe na watoto anajibu jeuri na dharau kama hawezi kuvumilia mwache aende,aniachie watoto wangu.anafikiri akiondoka ndo atapata mwanaume mtakatifu.yaani huyu kaka kama kachanganyikiwa mpaka aibu mwezi uliopita tu tulipeleka mahari tukitegemea mwezi wa pili mwakani wafunge ndoa . tuwasaidieje hawa watu jamani wifi ni mcheshi lakini toka juzi hata haongei jana nimeshinda huko kwa kaka wifi hata kula shida.leo namuuliza kaka anajibu bado jeuri wifi yako atakufa kwa wivu usiku kakesha anafanya kazi kafua, kadeki kaosha vyombo,kanyoosha nguo mpaka asubuhi,atakuwa anajiandaa kwenda kwao.naona kaka hajui anachokifanya atapoteza mke.nisaidieni nimsaidie kaka angu.

kwanza kabisa wewe na wazazi wenu wote wazushi tuu...mnajidai kumkandia mshikaji kuwa hamkubali huyo mcharuko...kama nyie ni watu wa maadili kwa nini hamkukemea tabia hake ya kuishi na huyu wifi yako ikiwa hawajaoana?
sasa u pay fof ur double standards..mmenyamaza mwezenu akaona sawa tuu kugegeda na kutia mimba wanawake.
huyo wifi yako nae kajitakia haya. mnaambiwa wanawake kila leo ukishaishi na mwanaume kabla ya kuilewa mwabaume atakudharau tuuu mnabisha haya mfano hai huo hapa.
 
kwani kuosha rungu kuna kosa gani? mwacheni kaka yenu ale vile vitu roho inataka! au kama vipi mushaurini wifi yenu aweke tego kama la temeke ili wanasane na huyo hawara labda kaka yenu atajifunza kitu kama kweli mnataka kumsaidia aendelee na huyo mnayemtaka...
 
ama kweli wewe wajua maana ya tundatamu. nakupenda manake wajua utamu wa tunda la mke mzuri alonalo kaka yako ingawa yeye halioni.

kwangu mm mkataa pema pabaya pana mwita, na waswahili husema mtoto akililia wembe mpe.

najua kaka yako anatumia nguvu ya kiume tu kwamba ni mwanaume kesha zaa hana jinsi, ni kweli kwani maji yakisha mwagika hayazoleki lkn amesahau kwamba anatakiwa kuyarekebisha makosa yake, kwa kumwonyesha mkewe kwamba anajuta alolifanya na yuo tayari kulirekenbisha kosa hili ili kulinda ndoa na penzi kwa mkewe.

wifi yako, anatakiwa aangalie kama mume hana mapenzi nae na wala hajali kama kakosea ni wazi ata akibaki atazidi kunyanyasika tu la msingi b4 its late aanze maisha mapya na Mungu atamasaidia. ni bora akaish alone pasi iyo ndoa kuliko kuish na cheater ambae hajutii wala haoni kama anakosea tena asiye thamani mapenzi ya mwenzie.

Nitamtafuta huyo mwanamke akiachika hata kama kanizidi miaka 30. Ukimuudhi anakesha anafua na kuosha vyombo, hakuna haja ya kuajiri mmasai.
 

Similar Discussions

4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom