Jamani nina kaka angu ameishi na mwanamke mpaka wanawatoto wawili hajafunga ndoa, mwezi uliopita kaka akasema anataka kufunga ndoa na mkewe tukaenda kwao na wifi kutoa mahari. Juzi wifi kapata habari kuna dada ambaye ni x-girlfriend wa kaka anamimba ya kaka. wifi amekata tamaa siku mbili tu namuona amekonda nahisi ataondoka jamani wifi yangu nampenda hivi hata mama presha zimepanda kwa kile alichokifanya kaka baba yeye kamwambia tu kaka hilo balaa silitaki katika familia yangu,namtambua mke mmoja tuliyemtolea mahari hao malaya wako sitaki kuwasikia.wifi yangu ni mke jamani hata kaka aliwahi kukiri, alafu huyo mdada mwenye mimba ni mcharuko balaa. tumemuuliza kaka amekili alichofanya ila haonyeshi kujuta wala kumuhurumia mkewe na watoto anajibu jeuri na dharau kama hawezi kuvumilia mwache aende,aniachie watoto wangu.anafikiri akiondoka ndo atapata mwanaume mtakatifu.yaani huyu kaka kama kachanganyikiwa mpaka aibu mwezi uliopita tu tulipeleka mahari tukitegemea mwezi wa pili mwakani wafunge ndoa . tuwasaidieje hawa watu jamani wifi ni mcheshi lakini toka juzi hata haongei jana nimeshinda huko kwa kaka wifi hata kula shida.leo namuuliza kaka anajibu bado jeuri wifi yako atakufa kwa wivu usiku kakesha anafanya kazi kafua, kadeki kaosha vyombo,kanyoosha nguo mpaka asubuhi,atakuwa anajiandaa kwenda kwao.naona kaka hajui anachokifanya atapoteza mke.nisaidieni nimsaidie kaka angu.