Nisaidieni mawazo ndugu zangu

Baba Rayhaan

JF-Expert Member
Mar 24, 2011
615
418
Nilikua na mwanamke niliemuoa na nilikua nampenda kupita kiasi, ila tumeachana miaka miwili iliyopita baada ya kuhisi eti ninatembea na rafiki yake, kiukweli sikua kabisa na uhusiano na rafiki yake na alipochukua maamuzi ya kunisubiri nitoke nyumbani kisha asombe kila kitu ndani na kuondoka, iliniuma sana nilikonda sana kwa sababu nilikua nampenda mke wangu kupita maelezo, nilijitahidi sana kumshawishi arudi tuendeleze maisha lakini cha kustaajabisha wazazi wake walimpeleka kumsomesha hotel management huko Dar es Salaam bila hata kunitaarifu na sasa hivi anafanya kazi hoteli ya kitalii huko Zanzibar, ilinichukua muda mrefu sana kumuondoa kichwani na ilibidi nikapate msaada wa daktari ambae aliniandika anti depressants nikatumia kwa miezi sita angalau nikaanza kuzoea hali halisi kwamba sipo na mke wangu anymore, msaada ninaowaomba mnisaidie ni kwamba, kwann nikiona kila kitu kinachomuhusu yeye moyo unanilipuka na kuanza kwenda mbio? Kila kitu mpaka mtoto wetu nikimuangalia namuwaza sana mama yake, sijaingia tena ktk uhusiano kwani ninaogopa sana kwa sasa, nishaurini nifanyeje niwe angalau namuona wa kawaida na moyo usiniende mbio kiasi hiki.
 
Asante, yaan sijui ndio kupenda kwa namna gani huku jamani hata sijielewi, naogopa sana kuingia katika mahusiano kwa sasa nahisi kama kakidonda bado kapo moyoni

pole sana, hicho unachokisema nakielewa sana

suluhisho tafuta mtu akuliwaze
 
Una mapenzi ya kipekeee, sasa siku ukikutana naye uso kwa uso si ndio utakufa kabisa.
 
Kama una vitu kama picha, nguo vipo kwako unaweza kuviondoa ili isikufanye umkumbuke tena.

Kwa suala la mtoto unaweza kumpeleka kwa bibi yake akalelewe kwa mda mpaka hapo akili yako itakapo kaa sawa ( kumsahau mkeo ) ndio ukamchukue.
 
Kama una vitu kama picha, nguo vipo kwako unaweza kuviondoa ili isikufanye umkumbuke tena.

Kwa suala la mtoto unaweza kumpeleka kwa bibi yake akalelewe kwa mda mpaka hapo akili yako itakapo kaa sawa ( kumsahau mkeo ) ndio ukamchukue.
Mtoto yupo kwa shangazi yake huko, sijui tu ni kwanini moyo wangu hautaki kuzoea
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom