Nisaidieni kuhusu huyu celeb wetu mkongwe

SHIEKA

JF-Expert Member
Dec 20, 2011
8,244
4,258
WanaJF, ninaomba mnipe jina halisi la Bi Kidude na kwa nini alipewa jina hili la Bi Kidude?
 
Anaitwa Fatuma binti Baraka, jina la Kidude ni la kisanii.
Wakati mwingine make use of Google na uache kusumbua watu humu.
Sawasawa?
 
WanaJF, ninaomba mnipe jina halisi la Bi Kidude na kwa nini alipewa jina hili la Bi Kidude?

Huyu ni celebrity tunaemuheshimu sana kutokana na umri wake pamoja na kazi zake. Kwa vijana walio wengi hulitafsiri hili jina katika negative perception na hivyo kumvunjia heshima bibi wa watu.
 
Anaitwa Fatuma binti Baraka, jina la Kidude ni la kisanii.
Wakati mwingine make use of Google na uache kusumbua watu humu.
Sawasawa?
Kuna raha yake kupata info kutoka kwa wanaJF wenyewe kuliko kupambana na google. Asante kwa hilo jina.
 
Kuna raha yake kupata info kutoka kwa wanaJF wenyewe kuliko kupambana na google. Asante kwa hilo jina.

wewe nawe?
Sasa hizi taarifa nilizokupa mimi nimezitoa Wikipedia via Google.
Halafu hao wana-JF wana 'u-wenyewe' gani mpaka uwaweke juu hivyo?
 
nadhani ingekuwa vyema kama ungeenda Zanzibar ukamuuliza mwenyewe. nadhani eyey atakupa jibu zuri
 
nadhani ingekuwa vyema kama ungeenda Zanzibar ukamuuliza mwenyewe. nadhani eyey atakupa jibu zuri
Mtumeeee Young_Master! Kwa nini unanitolea kali hivyo? Yaani nivuke bahari kisa kutafuta jina la mtu? Hata hivyo namshukuru Mphamvu keshanipa jina.
 
wewe nawe?
Sasa hizi taarifa nilizokupa mimi nimezitoa Wikipedia via Google.
Halafu hao wana-JF wana 'u-wenyewe' gani mpaka uwaweke juu hivyo?
WanaJF kubadilishana habari naona ndiyo 'essence' ya JF. Ulivyoingia Google na wikipedia kunisaidia umeonyesha moyo wa kiJF unaotakiwa! Nashukuru ndugu
 
Back
Top Bottom