Ugonjwa wa Kisonono (Gonorhea): Dalili, kinga na tiba yake

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,319
33,125
Kisonono (gonorrhea) ni nini?
Kisonono ni ugonjwa kati ya magonjwa ya zinaa unaosababishwa na bakteria aina ya Neisseria gonorrhoeae, bakteria ambao hukuwa na kuzaliana kwa haraka katika sehemu zenye unyevunyevu na joto mwilini kama kwenye shingo ya kizazi kwa wanawake (cervix), mirija ya kupitisha mkojo au shahawa (urethra), mdomoni na kwenye puru. Maambukizi mengi kwa wanawake hutokea kwenye shingo ya kizazi (cervix). Asilimia 75 ya ugonjwa wa gono hutokea kwa watu wenye umri wa miaka 15-19 wanawake walio katika umri wa miaka 15 -19 na wanaume walio katika umri wa miaka 20 -wako kwenye hatari zaidi ya kupata ugonjwa huu.

Ugonjwa huu huambukizwa vipi?
Ugonjwa huu huambukizwa kupitia vitendo vya ngono kupitia uke, njia ya haja kubwa (anus), kupitia mdomoni (oral sex). Ugonjwa unaweza kujitokeza kwenye sehemu za kujamiana, kwenye mdomo na kwenye puru (rectum). Ugonjwa wa gono huonekana sana kwa vijana, watu wenye maisha duni kiuchumi, watu wanaoishi mijini, watu weusi na watumiaji madawa ya kulevya.Dalili za ugonjwa wa kisonono
Dalili za ugonjwa wa kisonono huanza kujitokeza kuanzia siku ya 2 hadi ya 7 baada ya mtu kupata maambukizi na huweza kuchelewa kwa wanawake. Dalili ni kama zifuatazo;


Kwa wanaume:
  • Kuhisi kama kichomi wakati wa kukojoa (burning sensation)
  • Kutokwa na majimaji ya njano au meupe au ya kijani kutoka kwenye uume yanayoambatana na maumivu makali sana
  • Wakati mwengine maumivu au kuvimba kwa korodani (swollen testicles)
  • Maambukizi yakiwa kwenye puru (rectum) huambatana na maumivu wakati wa kujisaidia haja kubwa, kuwashwa sehemu za haja kubwa, na hata haja kubwa inaweza kutoka ikiambatana na damu, hii inatokea kwa wanaume na wanawake.

Kwa wanawake:
  • Dalili kwa wanawake huwa si nyingi lakini wanawake wengi hawaonyeshi dalili zozote
  • Maumivu au kuhisi kama kichomi wakati wa kukojoa
  • Kuongezeka kwa kutoka majimaji kutoka kwenye tupu ya mwanamke ambayo ni ya njano au yamechanganyika na damu
  • Kutokwa na damu kupitia tupu ya mwanamke kabla ya hedhi kufika.
  • Kutokwa na damu baada ya kujamiana au baada ya tendo la ndoa
  • Kichefuchefu
  • Homa (fever)
  • Kutapika

Vipimo vya ugonjwa wa kisonono
  • Swab for culture Kipimo hiki hufanyika maabara kwa kupandikiza bakteria baada ya kufuta sehemu za siri kwa kutumia swab ili kuona kama kuna bakteria wanaosababisha gono.
  • Polymerase Chain Reaction (PCR) Kipimo cha kuangalia vina saba (DNA) ya bakteria, ni ghali sana.

Tiba ya ugonjwa wa kisonono ni nini?
Tiba ya gono inahusisha na tiba ya ugonjwa wa Chlamydia kwani mara nyingi magonjwa haya huambatana kwa pamoja.Tiba hutegemea na umri wa mgonjwa na kama mtu ni mjamzito au la. Tiba ya gono ambayo sio sugu iliyo kwenye shingo ya kizazi (cervix), urethra na

puru, dawa zinazotumika ni aina za cephalosporin dozi moja pamoja na dawa za aina ya macrolide antibiotics (mfano azithromycin) na za jamii ya penicillin (mfano doxycyclin) ili kutibu ugonjwa wa chlamydia. Mara nyingi kwa wale chini ya miaka 18 na wanawake wajawazito, hutibiwa kwa kuchomwa sindano. Fuata ushauri wa daktari kabla ya kutumia dawa hizi kwani dawa nyingi zina madhara kwa wajawazito (mfano doxycyclin). Ushauri nasaha hutolewa kwa wapenzi wote wawili na ni vizuri wapenzi wote wawili kutibiwa hata kama mmoja hana dalili za ugonjwa huu.Madhara ya ugonjwa wa kisonono

  • Kutoweza kuzaa kwa mwanamke (tasa) au kutoweza kutungisha mimba kwa mwanamume (infertility)
  • Huweza kuathiri moyo (heart valves), ubongo,ngozi nk ambayo ni hatari sana kwa mtu yoyote.
  • Madhara kwenye sehemu za maungio au jointi (joint inflammation)
  • Kwa wanawake wale ambao hawajatibiwa wanaweza kupata ugonjwa wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) ambao huongeza asilimia ya mwanamke kuwa tasa.
  • Wale wanawake ambao ni wajawazito na wameambukizwa gono wako kwenye hatari ya mimba kutoka au kuzaa mapema kabla mimba haijatimiza umri wake (preterm labor).
  • Kwa wale wanaoambukizwa gono kipindi cha kukaribia kujifungua, wanaweza kuwaambukiza watoto wao na hivyo watoto kupata ugonjwa wa uti wa mgongo (meningitis), kuwa kipofu (blindness), homa ya mapafu (pneumonia) na ugonjwa wa mifupa (septic arthritis).

Kinga ya kisonono
  • Kutumia kondomu wakati wa kujamiana
  • Kuwa na mpenzi mmoja mwaminifu
  • Kuacha vitendo vya ngono kama matumizi ya vifaa vya ngono hasa kwa wanawake mfano vibrators nk.
  • Kwa wanawake wajawazito Hakikisha unahudhuria kliniki mapema ili upate kuchunguzwa na kupatiwa tiba muafaka kama utagundulika na ugonjwa wa gono au ugonjwa mwengine wowote.
  • Wanawake wajawazito wanashauriwa kujifungulia hospitali ili kama mtoto ameathirika na gono apate matibabu ya haraka baada ya kuzaliwa kuepusha kuwa kipofu.
  • Epuka kufanya ngono na mtu aliyeambukizwa gono.

"Kumbuka ya kwamba hakuna kitu kama ngono salama kwani huwezi kujua kama wewe au mwenzako wakati wa kujamiana ameathirika au la, au una michibuko au umekatika kwenye ngozi au la kwani michibuko mengine inaweza isionekane au kugundulika kwa urahisi. Njia pekee na nzuri ni kuacha au kujikinga na vitendo vya ngono". Mtu aliyepata gono awali anaweza kupata tena.
ummu kulthum Aende hospitali kupiga Sindano haraka iwezekanavyo.
 
Salam wakubwa,

Kuna jamaa yangu hii niki ya 3 kama 4 naona anameza dawa antibiotics (doxy na ingine nimeisahau). Kila nikimuuliza ananiyeyusha ila leo jioni ameniambia ukweli kuwa Gono inamsumbua. alienda hospital akapewa hizo dawa lakini bado inarudia rudia
wakati amesimama kabisa kamchezo.

swali Je tutamsaidiaje?
 
How to Treat Gonorrhea
One of the most common sexually transmitted diseases in the world, gonorrhea can cause potentially serious medical complications unless you treat it promptly and properly. It can be asymptomatic, so you should be screened for gonorrhea regularly if you are sexually active.
Instructions

Treat Gonorrhea
  1. Recognize that up to 60 percent of gonorrhea cases, in both men and women, do not show any symptoms of infection. Even if you seem perfectly healthy, you must take the initiative and ask your doctor for a gonorrhea screening.
  2. Know that the most common symptoms of gonorrhea, in both men and women, include difficult or painful urination and genital discharges. The disease has an incubation period of up to
  3. weeks, meaning a newly infected person will not experience symptoms until the incubation period has elapsed. Symptoms, when present, usually begin to show within about 5 days after incubation.
  4. Make an appointment with your physician or at a sexual health clinic to be screened for gonorrhea. There are three primary methods used to detect gonorrhea: direct staining tests for the presence of gonorrhea bacteria, DNA tests for gonorrhea in urine and a bacterial swab from which doctors will attempt to grow the bacteria in a laboratory.
  5. Realize that your doctor will be unable to tell you immediately whether or not you have gonorrhea. If you are found to be infected with the disease, your doctor will set up another appointment to advise you on its treatment. Tell your doctor if you have any known allergies to antibiotic medications. Antibiotics are the primary treatment method used to treat cases of gonorrhea.
  6. Take the antibiotic medications your doctor prescribes as directed by your pharmacist. Continue to take the medication, if advised, even after symptoms begin to clear up. It is very important that you abstain from sexual activity during your treatment period.
  7. Submit to re-testing after your antibiotics have been used up. Your doctor will be able to tell you whether or not the infection has cleared up.

Source: How to Treat Gonorrhea | eHow.com

Tips & Warnings

  • People infected with gonorrhea are at increased risk of contracting or passing on the HIV virus. It is essential that you practice safe sex at all times. Abstain from sexual intercourse if you become infected with gonorrhea.
  • Bear in mind that gonorrhea is beginning to show signs of resistance to antibiotics. In particular, tetracycline has been less and less effective against it. The worst-case scenario is that you have contracted a resistant strain and will have to manage rather than cure the disease.
Read more: How to Treat Gonorrhea | eHow.com How to Treat Gonorrhea | eHow.com


Kwa Ushauri wangu aende Hospitali kuu kama yupo hapo Dar mwambie aende Hospitali ya Rufaa muhimbili kuna wataalam wa hayo Maradhi ikishindikana mwambie aje hapa tutampa

Dawa za Mitishamba kujaribu kutumia. mimi mwenyewe katika ujana wangu wakati nina Umri wa miaka 24 niliwahi kushikwa na huo ugonjwa aliniambukiza Mwanamke wangu nikaenda nae

hospitalini kutibiwa tukapona wote wawili nakumbuka tulipigwa sindano ya PPF kwa muda wa siku tatu mfulululizo nakutumia vidonge sikumbuki ni vidonge vipi tukapona Gono linauma wakati wa kukojowa hutowa usaha mweupe mpe pole sana huyo jamaa.
 
Kisonono ni maradhi ya zinaa ambayo husababishwa na bakteria zinazofahamika kisayansi kama Neisseria gonorrhoeae. Bakteria hizo hushambulia utandotelezi unaozunguka sehemu za siri.

Ingawa kwa makisio maambukizi 360,000 ya kisonono huripotiwa kila mwaka nchini Marekani, wataalamu wamekisia kuwa watu karibia 650,000 huambukizwa kwa mwaka.

Kama ilivyo klamidia, kisonono nayo huwa haionyeshi dalili. Kisonono ikiwepo huwa na dalili kama zile za klamidia ambazo huhusisha mauvimu wakati wa kukojoa na kutokwa kwa maji yanayonuka au usaha katika uke au uume.

Kisonono huonekana kwa urahisi kwa wanaume ambao hutoa usaha kutoka katika mfereji wa mkojo (urethra). Huanza kidogo, lakini huongezeka na huwa mwingi na kusababisha kusikia haja ya kukojoa mara kwa mara huku kukiwa na maumivu.

Kisonono ikisambaa na kufikia prostate, mfereji wa mkojo huziba kwa kiasi fulani. Kwa wanawake maambuki hutokea katika urethra, uke au mlango wa uzazi (cervix). Ingawa mwasho unaotokana na majimaji katika uke unaweza kuwa mkubwa, mara nyingi dalili hizi huwa ni chache au hamna kabisa katika hatua za awali.

Kisonono isiyotibiwa inaweza kusababisha PID kwa wanawake. Watoto wanaozaliwa na mama wenye kisonono huwa na hatari ya kuambukizwa wakati wa kuzaliwa; maambukizo haya yanaweza kusababisha magonjwa ya meno kwa wachanga.

Uchunguzi wa ugonjwa hufanywa kwa kuchungunza usaha kutoka katika uke au uume au mkojo kwa uwepo wa Neisseria gonorrhoeae.
Kisonono iliongezeka kwa kiasi kikubwa Marekani mnamo miaka ya 1970 na mwanzoni mwa miaka ya 1980, hadi kukaribia kufikia kiwango cha magonjwa ya mlipuko (epidemic proportions) kwa vijana wanaobalehe na watu wa umri wa kati.

Kisonono hutibiwa kwa antibaotiki kadhaa, ingawa maambukizi yamekuwa na ukinzani juu ya tiba ya baadhi ya madawa katika miongo ya nyuma. Moja kati ya mambo magumu katika kupambana na kisonono ni kutafuta mahusiano yote ya kimapenzi ya nyuma ya aliyeambukizwa ili kuweza kuzuia usambaaji zaidi wa ugonjwa.
 
Mh. Kicharo, kwa kuwa hujataja dalili alizonazo napenda kwanza ieleweke kuwa Kama ni Gonorrhea (Kisonono) atakuwa anatokwa na usaa kwenye njia ya mkojo, kama si hivyo itakuwa ni STD aina nyingine, km ana dalili hizo basi TIBA SAHIHI nashauri nakili prescription hii akamwonyeshe mganga wake wake amwandikie tiba kwa usahihi.

kwa kuwa usaa ktk njia ya mkojo inaweza kusababishwa na GONORRHEA au CHLAMYDIA au vyote, basi anatakiwa achanganye dawa mbili kama ifuatavyo,

  1. Inj SPECTINOMYCIN 2g intramuscular single dose (atachomwa matakoni sindano moja)
  2. Tabs AZITHROMYCIN 1g single dose (atakunywa vidonge 8 kwa mpigo kama vitakuwa na kiwango cha 250mg Tembe)
kwa tiba hii, ndani ya masaa 48 atapata matokeo chanya, unless awe amerogwa au dawa alizopata ni za kuigiza

NB
  • Tiba hii lazima aandikiwe na daktari/tabibu baada ya kujiridhisha kuwa ni Gonorrhea, Mini kama mwana JF Sitahusika kwa lolote kama mhusika ataamua kujinunulia dawa na kutibiwa na watu wasio na mamlaka na ujuzi wa tiba.
  • Inashauriwa pia afanye kipimo cha kaswende (VDRL test) kwa kuwa anaweza kuwa alipata co-infection (syphilis inachelwa kuonyesha dalili) na pia ni busara kupima VVU sasa na baada ya miezi mitatu kama matokeo ya kwanza yatakuwa ni hasi.
 
Visenti umejitahdi kutoa utaalamu ila mwishoni umenichefua! Kwa dunia ya sasa na mtaalamu kama wewe hupaswi kutoa ushauri wa nadharia kwamba mgonjwa amelogwa! dk. unaamini uchawi??!
 
Visenti umejitahdi kutoa utaalamu ila mwishoni umenichefua! Kwa dunia ya sasa na mtaalamu kama wewe hupaswi kutoa ushauri wa nadharia kwamba mgonjwa amelogwa! dk. unaamini uchawi??![/QUO

Mh. Kisima nakiri kwa hilo nimewapotosha wanainji kwa jinsi nilivyoliweka, ilikuwa ni mchanganyiko na kautani kumbe si mahala pake, nimeliona hilo na nashukuru kwa kulikemea.
 
mkuu visenti mimi sioni kama umekosea inaonyesha jamaa ni mlokole(kisima) kwani ni nani asie jua uchawi ee bwana we acha uchawi upo uliza mitaa ya manzese unaweza ukala dawa kumbe ni majambozi kitaani
Conquest-kitaani usile pilau usiku kipigo eti umekula vizuri:A S angry:
 
Hongela dr, kwa kujitolea kuielimisha jamii ktk maswala mhimu kama afya. Ni vema pia ukaweka bayana ni jinsi gani ya kujikinga nayo. Asante, Nimrod, Mwanza
 
Mi napenda nimshauri angeenda kupima kabla ya kuanza kujichukulia uamuzi wa kumeza dawa, magonjwa ya zinaa mengi yana stage zake, matibabu yanatolewa kwa stage vilevile.
 
Mh. Kicharo, kwa kuwa hujataja dalili alizonazo napenda kwanza ieleweke kuwa Kama ni Gonorrhea (Kisonono) atakuwa anatokwa na usaa kwenye njia ya mkojo, kama si hivyo itakuwa ni STD aina nyingine, km ana dalili hizo basi TIBA SAHIHI nashauri nakili prescription hii akamwonyeshe mganga wake wake amwandikie tiba kwa usahihi.
kwa kuwa usaa ktk njia ya mkojo inaweza kusababishwa na GONORRHEA au CHLAMYDIA au vyote, basi anatakiwa achanganye dawa mbili kama ifuatavyo,

  1. Inj SPECTINOMYCIN 2g intramuscular single dose (atachomwa matakoni sindano moja)
  2. Tabs AZITHROMYCIN 1g single dose (atakunywa vidonge 8 kwa mpigo kama vitakuwa na kiwango cha 250mg @tembe)
kwa tiba hii, ndani ya masaa 48 atapata matokeo chanya, unless awe amerogwa au dawa alizopata ni za kuigiza

NB

  • Tiba hii lazima aandikiwe na daktari/tabibu baada ya kujiridhisha kuwa ni Gonorrhea, Mini kama mwana JF Sitahusika kwa lolote kama mhusika ataamua kujinunulia dawa na kutibiwa na watu wasio na mamlaka na ujuzi wa tiba.
  • Inashauriwa pia afanye kipimo cha kaswende (VDRL test) kwa kuwa anaweza kuwa alipata co-infection (syphilis inachelwa kuonyesha dalili) na pia ni busara kupima VVU sasa na baada ya miezi mitatu kama matokeo ya kwanza yatakuwa ni hasi.
Dozi hiyo ya Azthromycin
una huhakika nayo?are u medical profession?unajua hizo dawa zinakuja kny strenght gni? Zipo za 250mg na 500mg kma akimeza 250mg ni vidonge 4 na km ni 500mg ni vidonge 2,pls kwa tiba zaidi nenda hosp kwa hajili ya vipimo.
 
Wakubwa habari za kazi natumai mu wazima.Naombe msaada wenu kwa wanaoijua dawa ya kutibu ugonjwa huu.
 
Dr bora umemtibu kaka wa watu,lol!

Hivi hakuna tiba m'badala ya magonjwa haya?
Usisahau kumuambia asione soo, kwani kuugua kisonono ni dalili kuwa ukimwi hauchezi mbali naye.
 
Dr bora umemtibu kaka wa watu,lol!

Hivi hakuna tiba m'badala ya magonjwa haya?
Usisahau kumuambia asione soo, kwani kuugua kisonono ni dalili kuwa ukimwi hauchezi mbali naye.
Dawa ya Kienyeji ya Kisonono ya Tiba Mbadala Apate Mizizi ya Mvule na Mizizi ya Mbono uchemshe kwenye maji unywe kutwa mara 3 kwa muda wa wiki 3 inshallah atapona.@KIBURUDISH Mkuu.@King'asti
 
Nilijua tu hukosi maarifa. Asante boss. Manake na mgomo huu, mweeh! Ataishia kuzodolewa na dr kwa ngono nzembe kuliko kusaidiwa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom