Nipo tayari kujiuzuru endapo itathibitika-waziri wa miundombinu

Bajabiri

JF-Expert Member
Jan 1, 2011
9,730
1,201
Waziri wa miundombinu wa zanzibar hamad masud mh.Hamad Masudi amesema yupo tayari kujiuzuru
Sosi:bbc
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Amesema kuwa hatosubiri hadi rais amwambie.,,,,,,kama huo UTAMADUN HAUPO.........YEYE ATAUANZISHA,,,,,
SWALI:KWANIN HUYU WAZIRI YUPO HADI LEO?????
 
Bro,hatuna utamaduni huo,,,yeye kasema anasubiri TUME,na iwapo tu atatajwa kwenye taarifa ua TUME
Hana haja ya kusubiri tume. Kwa heshima heshima ya viumbe waliopoteza maisha bila hatia, anapaswa kuondoka. Kusubiri tume ni kusubiri huruma ambayo hastahiki. Aondoke!
<br />
<br />
 
Husninyooooo.....hahahaaa mimi hata nyumba niliyopanga sina hata ukiranja wa kukusanya LUKU&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;
<br />
<br />
hahahaha! Jeief hii, isije kuwa mheshimiwa sana bana!
Mheshimiwa usijiuzulu aisee.
 
Anasubiria tume ? nini maana ya kujiuzuru sasa ?
Kama tume ikionyesha ana kosa , huyo si wa kujiuzuru tena , bali wa KUFUKUZWA
 
Sasa ndio wakati wa kuwapima viongozi, hasa Mh. Shein na Maalim Seif Hamad kama kweli wanastahili sifa.
 
Sasa ndio wakati wa kuwapima viongozi, hasa Mh. Shein na Maalim Seif Hamad kama kweli wanastahili sifa.

Si vizuri kuwahukumu hawa tu kwani uzembe wa viongozi wetu wote ndio utamaduni wetu. List ya ajali za barabarani zilizotokea Tanzania tangu MV Bukoba ni ndefu sana lakini utaona kuwa zote zinajirudia kila kukicha. Tiba ya ugonjwa wetu siyo kunywa apsirini na kuendelea na shughuli za kila siku, bali tunahitaji operation na kulazwa wodini kwa muda wa siku kadhaa kabla hatujaanza shughuli zetu tena.
 
Si vizuri kuwahukumu hawa tu kwani uzembe wa viongozi wetu wote ndio utamaduni wetu. List ya ajali za barabarani zilizotokea Tanzania tangu MV Bukoba ni ndefu sana lakini utaona kuwa zote zinajirudia kila kukicha. Tiba ya ugonjwa wetu siyo kunywa apsirini na kuendelea na shughuli za kila siku, bali tunahitaji operation na kulazwa wodini kwa muda wa siku kadhaa kabla hatujaanza shughuli zetu tena.
Mkuu siwahukumu isipokuwa najua fika kwamba hakuna mtu atakaye jiuzulu bila shinikizo kutoka kwa hawa watu wawili. Na kutoka huku bara au niseme serikali ya Muungano, hakuna mtu anayeweza kuzungusha hata neno moja woote wana imani za kichawi zaidi...Nakumbuka enzi za mwalimu, Mzee Mwinyi Mzanzibar alikubali kuwajibishwa ktk swala lililotokea Shinyanga na hakuondoka peke yake...
 
Hayo mambo ya uwajibikaji tunayaona kwa wenzetu tu si Tanzania , waziri wa China alijiuzulu trenizilipo gongana lakini kwetu kilakitu siasa , kuna muhanga wa hiyoajali aliojiwa Jana na clouds anasema walipofika unguja Kama sikosei waliongeza mizigo na watu naodha akakataa kuendelea na safari sababu meli ilishaanza kulemea upande mmoja .Wafanya biashara waile mizigo wakamtafuta naodha mwingine wakampa hela akaondoa meli hapo sasa uchunguzi wa nini ?
 
Embu awaoneshe serikali ya magamba mfano wa kuwajibika, mana hawajui!
 
Maana halisi hasa ya kujiuzulu ni kuheshimu na kukubaliana na utawala wa sheria,hivyo timiza wajibu wako kwa maana halisi ya uwajibikaji. Kama dhamira yako inakusuta basi hapo inabidi ujiuzulu. Lakini kama utasubiri uchunguzi na halafu ukakutwa na hatia basi hapo si kujiuzulu tena ila itakuwa umewajibishwa kwa kufukuzwa kazi.

Mh waziri ni muda muafaka sana huu wa kujiuzulu na wala usingoje hadi ufanyike uchunguzi. Onyesha ukomavu wa kisiasa kwa chama chako cha CUF na serikali ya mseto (CCM + CUF). Chukua hatua mh waziri.

NOTE:
Usisahau kuacha kutumia huduma za vodacom, tena utangaze hadharani kwani wameidharau sana Zanzibar hawa jamaa wa vodacom. Nakuomba sana mh waziri paza sauti yako ya juu mataifa yoote yakusikie, hapo utakuwa umeacha angalau historia ya kufanya watu wa Zanzibar wakukumbuke kwa hilo. Paza sauti kubwa na unene kwa kuwaambia wazanzibar wakataeni vodacom kwa kitendo chao cha dharau. Kataeni kiabisa kutumia huduma zao.
 
Mkuu siwahukumu isipokuwa najua fika kwamba hakuna mtu atakaye jiuzulu bila shinikizo kutoka kwa hawa watu wawili. Na kutoka huku bara au niseme serikali ya Muungano, hakuna mtu anayeweza kuzungusha hata neno moja woote wana imani za kichawi zaidi...Nakumbuka enzi za mwalimu, Mzee Mwinyi Mzanzibar alikubali kuwajibishwa ktk swala lililotokea Shinyanga na hakuondoka peke yake...
Kwa kuweka rekodi sawa, Mwinyi hakuwajibishwa, aliwajibika. Na barua ya kujiuzulu ilisifika kwa kiswahili fasaha alichotumia. Ni aghalabu sana viongozi wa Afrika kuwajibika kwa kujiuzulu, Mwinyi aliweka mfano Tanzania.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom