Nipo tayari kuikomboa wilaya ya kilosa.

Mkomawatu

JF-Expert Member
Oct 13, 2012
267
118
Habari zenu ndugu wadau wa JF,nikiwa kama kijana mzalendo wa nchi hii na ambaye ninakereketwa na maendeleo duni ya wilaya yangu ya Kilosa,mkoani Morogoro na wilaya nyinginezo zilizo nyuma kimaendeleo nchini,natangaza rasmi kuwa nipo tayari kutoa mchango wangu wa mawazo na hata vitendo kwa wananchi wenzangu,viongozi wa vyama vya siasa na hata asasi za kiraia ili kuona mabadiliko yanapatikana,nawahakikishia kuwa nipo tayari kwa lolote na atakayetaka kuungana nami awe na dhamira ya uzalendo kwa umma na si vinginevyo.Naomba kuwasilisha hoja.
 
Huku tutakusaidiaje labda?ni maeneo gani ambayo mnadhani unataka kuungana na sie kuhakikisha unaleta maendeleo wilayani kwako, au unataka Ubunge hivyo unataka tuangalie namna ya kuku-support
 
Binafsi nategemea msaada wenu wa kuandaa makongamano ya kujadili mustakabali wa wilaya,kushirikiana katika uanzishwaji wa Jumuiya ya vijana wa kilosa,suala la ubunge itategemea na tathimini yenu kwangu kuangalia ujengaji hoja wangu na utendaji wangu kama mtatniona nafaa kuwaongoza nipo tayari,lakini ni vyema mkafahamu kuwa mimi ni muumini wa siasa za upinzani.
 
Back
Top Bottom