Nipo kinyume na kwenda kasi kwenye kurudisha mahusiano na Kenya

Nyumisi

JF-Expert Member
Nov 10, 2010
13,404
19,051
Salaam JF,

Hivi karibuni Mhe. Rais Samia alifanya ziara nchini Kenya lengo likiwa kurejesha mahusiano ya kibiashara na kidiplomasia na kujenga zaidi ushirikiano baina ya hizi nchi ili kuipa uimara Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Kilichonishtua ni kuona namna haya mahusiano yanavyokwenda kwa kasi ukizingatia kenya wamekuwa na urafiki wa mashaka na kimaslahi zaidi na Tanzania hadi kufikia kutukejeli na Rais wetu kwenye suala la korona na kutuchongea kwa mabeberu ambao kihistoria wamekumbatiwa sana huko Kenya na kuendesha mambo ya uchumi na uwekezaji kwa kushirikiana na wafanyabiashara wakubwa na wanasiasa.

Kwa hulka hii ya kukumbatia mabeberu na ubeberu kenya waliunga mkono Serikali ya makaburu dhidi ya mtu mweusi.

Hivi karibuni Kenya wamepiga marufuku mahindi ambayo yalikuwa tayari kuingizwa kutoka Tanzania kwa kisingizio cha sumu kuvu huku hayo mahindi wakiwa wanayatumia kwa miaka lukuki. Utafiti ukionyesha kwamba huo msimamo umetokana na kutaka kuikomesha Tanzania kama njia ya kulipa kisasi kutokana na Tanzania kuja na njia mbadala za kuendesha uchumi wake na kukuza uwekezaji na ajira.

Hivyo, naomba chonde chonde Serikali ichukue tahadhari kubwa katika mashirikiano dhidi ya Kenya.
 
Watu kama nyinyi Mh. Suluhu amewaongelea kule bungeni. Watu kadhaa walio na choyo na fikra finyu za kuendeleza chuki baina ya wananchi wa pande zote mbili. Na hamtaweza kwani mwendo ni wa 5G sahi.

Urafiki, undugu, ushirikiano na ujirani mwema kwa pande zote mbili husika ndio jambo muhimu sahi na mbeleni ili kuimarisha uchumi na hali ya maisha kwenye ukanda huu. 🇹🇿 + 🇰🇪 = Prosperity
 
Sisi ndio tulikuwa miamba,mahodari na mashujaa wa huo urafiki wa mashaka,na kuwa geuza maadui wetu,sababu sisi ni wavivu na walk niwachapakazi said yetu ,unabisha angalia uwekezaji wao kwetu, hata tukanaribu kuwazuia.
 
Watu kama nyinyi Mh. Suluhu amewaongelea kule bungeni. Watu kadhaa walio na choyo na fikra finyu za kuendeleza chuki baina ya wananchi wa pande zote mbili. Na hamtaweza kwani mwendo ni ya 5G sahi. Urafiki, undugu, ushirikiano na ujirani mwema kwa pande zote mbili husika ndio jambo muhimu sahi na mbeleni ili kuimarisha uchumi na hali ya maisha kwenye ukanda huu. 🇹🇿 + 🇰🇪 = Prosperity
Lazima twende na hatua za kujilinda ukizingatia kutotabirika kwa mahusiano ya Tanzania na Kenya tangu enzi za Mwl. Nyerere na Jomo Kenyatta....ni hatari kubwa kuingiza watu wetu kwenye mahusiano yasiyo na break na kenya. Tunahitaji kujenga kwanza uwekezaji wa ndani na kuwaandaa watu wetu kwenye kupambania fursa katika eneo zima la afria mashariki..
 
Mama aboreshe uhusiano na Majirani zetu wote

Kisha tuwasainishe kuwa hakutakuwa ma agression baina ya Nchi zetu

Kisha Mama apunguze Jeshi na kulibakisha kidogo bajeti ya Ulinzi ipunguzwe

Tuboreshe huduma za Jamii na kuuondoa huu umasikini unaotutesa.
 
Lazima twende na hatua za kujilinda ukizingatia kutotabirika kwa mahusiano ya Tanzania na Kenya tangu enzi za Mwl. Nyerere na Jomo Kenyatta....ni hatari kubwa kuingiza watu wetu kwenye mahusiano yasiyo na break na kenya. Tunahitaji kujenga kwanza uwekezaji wa ndani na kuwaandaa watu wetu kwenye kupambania fursa katika eneo zima la afria mashariki..
Sidhani Kama ni hoja ya msingi, Tanzania sio kisiwa tunahitaji kufanya biashara na majirani zetu kwa namna zote. Mfano Congo wanategemea bidhaa kutoka kwetu, na sisi tunapaswa kuchukua baadhi ya bidhaa za congo kuzileta huku. Hali hiyo pia kwa kenya na nchi zingine. Ukisema tufunge Ili tuimarishe uchumi wa ndani ni akili za ajabuajabu tu.
 
Lazima twende na hatua za kujilinda ukizingatia kutotabirika kwa mahusiano ya Tanzania na Kenya tangu enzi za Mwl. Nyerere na Jomo Kenyatta....ni hatari kubwa kuingiza watu wetu kwenye mahusiano yasiyo na break na kenya. Tunahitaji kujenga kwanza uwekezaji wa ndani na kuwaandaa watu wetu kwenye kupambania fursa katika eneo zima la afria mashariki..
Mkuu, yaliyopita si ndwele, tugange yajayo. Lakini ka waona kubaki nyuma ndio muhimu kwako, uko huru kubaki na msimamo wako. Kazi iendelee!
 
Mama aboreshe uhusiano na Majirani zetu wote

Kisha tuwasainishe kuwa hakutakuwa ma agression baina ya Nchi zetu

Kisha Mama apunguze Jeshi na kulibakisha kidogo bajeti ya Ulinzi ipunguzwe

Tuboreshe huduma za Jamii na kuuondoa huu umasikini unaotutesa.
Hata mimi zamani nilijua jeshi linakula fedha bure.

Malawi wakijua jeshi letu limepunguzwa nguvu wanchukua ziwa nyasa na mikoa ya Songea ,Njombe na Mbeya asubui-asubuhi.

Kenya wanajichukulia Kilimanjaro yao mapema kabisa.

Sijui waganda ule mto Kagera kama watatuachia.

Umemsikia mmisri anavyomtisha muethiopia ili aache mradi wake wa umeme kwenye vyanzo vya mto Nile?

Wakati mataifa mbalimbali ikiwemo Uganda wanaimarisha jeshi lao halafu sisi tupunguze budget tutakuwa tumecheza pata potea.
 
Hata mimi zamani nilijua jeshi linakula fedha bure.
Malawi wakijua jeshi letu limepunguzwa nguvu wanchukua ziwa nyasa na mikoa ya Songea ,Njombe na Mbeya asubui-asubui...
Hoja nzuri, sasa ndio maana nilisema tunafanya makubaliano na Majirani zetu wote haswa Malawi.

Iddi Amini na madai yake ya Mto Kagera zilikuwa ni Propaganda za kutaka Obote afukuzwe na Nyerere.

Tukiunda jeshi dogo lenye mafunzo ya Kisasa na vifaa vya kisasa kama ilivyo kwa Israel inakuwa muruwaa.

Tufanye kama Nchi ya Uswiss.
 
Sidhani Kama ni hoja ya msingi, Tanzania sio kisiwa tunahitaji kufanya biashara na majirani zetu kwa namna zote. Mfano Congo wanategemea bidhaa kutoka kwetu, na sisi tunapaswa kuchukua baadhi ya bidhaa za congo kuzileta huku. Hali hiyo pia kwa kenya na nchi zingine. Ukisema tufunge Ili tuimarishe uchumi wa ndani ni akili za ajabuajabu tu.
Biashara kati ya Tanzania na Kenya mbona ipo miaka mingi mkuu, ninachohofia ni hizi moves zinazoharakishwa ambazo zitaipa kenya advantages zaidi za kiuwekezaji nchini kwao huku wakifaidika kwa kutengeneza ajira zaidi na kuifanya Tanzania kuwa soko tu la bidhaa zao jambao ambalo litaendelea kuua ajira za watu wetu.

Kenyatta anaposema watanzania wanaruhusiwa kufanya kazi na biashara kenya bila zuio lolote kuna mtego mkubwa ndani yake, ndo maana wengine tunatahadharisha kwamba haya mahusiano yaendelee kwa kasi iliyokuwepo au iliyozoeleka, maana kuna watu wanataka twende kwa kasi ya 5G kwenye integration na kenya, jambo ambalo haliwezi kukubalika kwa mustakabali wa nchi na watu wetu.
 
T
Salaam JF, hivi karibuni mh. rais alifanya ziara nchini kenya lengo likiwa kurejesha mahusiano ya kibiashara na kidiplomasia na kujenga zaidi ushirikiano baina ya hizi nchi ili kuipa uimara jumuiya ya afrika mashariki...
Usiwaogope sana wakenya bali tuwatumie kifursa kujenga uchumi wetu na muhimu tujenge uhusiano wa kimkakati katika diplomasia ya uchumi ili ushirikiano wetu na wao uwe SMART na uchochee ukuaji wa uchumi na ustawi wa taifa.

Aidha, taarifa za kintelenjesia na ujasusi wa kiuchumi tuutumie sana kuwa contain wakenya bila kuharibu uhusiano. Dunia ni moja na twende nao kwa kanuni ya complimentarity badala ya ushindani.
 
Hoja nzuri, sasa ndio maana nilisema tunafanya makubaliano na Majirani zetu wote haswa Malawi

Iddi Amini na madai yake ya Mto Kagera zilikuwa ni Propaganda za kutaka Obote afukuzwe na Nyerere..
Sijachungulia budget ya jeshi la Israel wala Uswiss lakini naamini zitakuwa zinatenga dolari nyingi sana.

Nagoogle halafu nitaziweka hapa soon.
 
Sijachungulia budget ya jeshi la Israel wala Uswiss lakini naamini zitakuwa zinatenga dolari nyingi sana.


Nagoogle halafu nitaziweka hapa soon.
Uswiss haina jeshi waliingia mikataba na majirani zao wote ya Amani

Israel inajeshi dogo la kisasa na askari mgambo wengi wa akiba ambao hawalipwi mpaka itakapotokea vita.
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom