Mjina Mrefu
JF-Expert Member
- Dec 6, 2016
- 3,030
- 3,324
Wakuu habari,
Wasomi wa kiume wa siku hizi wanajifanya wapo selective sana katika suala la wake wa kuoa. Wengi hutamani kuoa wake wasomi kama wao na kudhani kuwa, kufanya hivyo ndipo kutawapunguzia mzigo wa majukumu.
Ikumbukwe kwamba, nilishapandisha uzi hapa jamvini kuelezea jinsi rafiki yangu(msomi wa degree) wa karibu alivyokuwa akisita kumwoa binti mrembo (mwenye elimu ya form 4 asiye na kazi).
Mke asiye msomi na asiye na kazi ni mzigo?
Jamaa nilimshauri sana amuoe huyo mrembo hadi nikamwonyesha ule ushauri wenu humu jukwaani but akawa anasua sua. Mwanamke alimuuliza kila mara kama ana nia ya kumwoa kweli but jamaa akawa hajibu majibu yaliyonyooka.
Mwanamke akaona msela hana mwelekeo na last week kuna jamaa mfanyabiashara wa vipodozi vya jumla Kariakoo kaenda kumvisha yule dada pete ya uchumba.
Msela ndiyo anahuzunika balaa hadi kazi hawezi kufanya. Anabaki akimwapiza yule dada na kusema kuwa hamwombei mazuri kwenye ndoa atakayoifunga na huyo mfanyabiashara.
Imebidi nichukue time yangu nimbembeleze msela na nijifanye niko upande wake maana mwanzo nilianza kumcheka kanyang'anywa mrembo alikua very stressed nikaona asijefanya maamuzi mabaya bure.
Jamaa hapa anasema kila saa hatokaa apende tena
Wasomi wa kiume wa siku hizi wanajifanya wapo selective sana katika suala la wake wa kuoa. Wengi hutamani kuoa wake wasomi kama wao na kudhani kuwa, kufanya hivyo ndipo kutawapunguzia mzigo wa majukumu.
Ikumbukwe kwamba, nilishapandisha uzi hapa jamvini kuelezea jinsi rafiki yangu(msomi wa degree) wa karibu alivyokuwa akisita kumwoa binti mrembo (mwenye elimu ya form 4 asiye na kazi).
Mke asiye msomi na asiye na kazi ni mzigo?
Jamaa nilimshauri sana amuoe huyo mrembo hadi nikamwonyesha ule ushauri wenu humu jukwaani but akawa anasua sua. Mwanamke alimuuliza kila mara kama ana nia ya kumwoa kweli but jamaa akawa hajibu majibu yaliyonyooka.
Mwanamke akaona msela hana mwelekeo na last week kuna jamaa mfanyabiashara wa vipodozi vya jumla Kariakoo kaenda kumvisha yule dada pete ya uchumba.
Msela ndiyo anahuzunika balaa hadi kazi hawezi kufanya. Anabaki akimwapiza yule dada na kusema kuwa hamwombei mazuri kwenye ndoa atakayoifunga na huyo mfanyabiashara.
Imebidi nichukue time yangu nimbembeleze msela na nijifanye niko upande wake maana mwanzo nilianza kumcheka kanyang'anywa mrembo alikua very stressed nikaona asijefanya maamuzi mabaya bure.
Jamaa hapa anasema kila saa hatokaa apende tena