Nionavyo mimi: Pinda si mtoto wa mkulima

Ananiboa sana maneno yake. kila siku anasema Watanzania tufike mahali ....wakati hatoi mwongozo na mikakati ya kufika hapo anapotaka tufike. Tufike mahali tiache kutumia magari ya kifahari, tufike mahali tuachane na matumizi yasiyo ya tija.
 
Of course kama magari yenyewe ni ghali unategemea kuyamaintain ni rahisi? cha msingi ni kwa serikali kupunguza u-Vasco Da Gama na kuimarisha vitengo vya IT ili movements ziwe limited. Kwamba kusiwe na misafara ya wanasiasa kukagua miradi au upuuzi mwengine kama huo usioleta tija.
 
Pinda si kiongozi bari ni kiongozi funika kombe mwanaharamu apite,anatumia magari ya kifahari wakati wananchi wake wanamaisha magumu ya kutisha jimboni kwake na watanzania kwa ujumla.
 
Nilishitushwa sana na kauli yako tata nyingine waziri Mkuu wangu, a.k.a. Mtoto wa Mkulima pale ulipokuwa unijaribu ku-promote Lugha yetu adhimu ya Kiswahili pale ulipotoa sifa lukuki ya kuwa Lugha hii sasa imekuwa na kuanza kuzungumzwa hata UN kwa hiyo si vibaya kama itaanza kutumika kwenye mitaala yetu ya elimu mpaka ya chuo kikuu.

Kilichoniacha hoi, ni pale ulipotolea mfano wa mtu unapozungumza Kiswahili fasaha hata Europe, Watu Wanaku "Admire"!

Huenda wewe mwenye hukuwa unakiamini ulichokuwa unazungumza na ukaona kuwa usipoingiza japo neno moja la Kidhungu utaonekana dhalili ndo maana ukapiga kiswa-english (Ku-admire)! Ina maana hakuna neno la Kiswahili ungeweza kulitumia badala ya Ku-Admire! Au wewe hukutaka Watu waku-admire kwa kuzungumza kiswahili sanifu!

Kuwa kama Lowasa, Chukua Uamuzi mgumu kwa kufanya unachokiamini hata kama kwa wengine ni kibaya lakini si kulazimisha jambo ambalo hata wewe mwenyewe huliamini. Au nawewe ukishapata Pesa kama wenzio ndipo utakapoanza kuwa na Msimamo wa kwako binafsi!
 
Watanzania tufahamu kuwa waziri mkuu wetu anayejitanabaisha kama mtoto wa mkulima ametusaliti. Sasa anashabikia wabunge walipwe posho nono. Hivi wakulima wenzie wanashindwa kununua hata jembe jipya yeye mkulima mwenzetu anashabikia wabunge wenzake wapate "mapesa". Badala ya kuelekezea pesa hizo kwa wakulima wenzie, je pinda tunae tena sisi wakulima maskini? Hakika pinda kalewa na madaraka. Kweli madaraka na fedha ni ndugu!!
 
hivi baada ya yote haya, bado twaweza endelea kumuita waziri mkubwa, mtoto wa mkulima???????

okay wengine wanaweza sema matatizo yake hayabadilishi ukweli kuwa wazazi wake walikuwa wakulima, lakini what is the point kumuita mtu jina ambalo halithamini. kilichofanyika juzi kimedhihirisha kuwa mkuu wetu huyu hathamini maisha ya watanzania wa hali ya chini na ya kawaida hasa wakulima na wafanyakazi. maamuzi yaliyokuwa yanasubiliwa na watu kibao yakageuzwa na kuwa maelezo ya kila siku, japo alinifurahisha kidogo kuwasifia simba, lakini haikuwa sehemu yake.

hivi nitakuwa na kosa kama nikianza kumuita huyu jamaa mtoto wa mfanyabiashara???????
 
inasemekana mtoto wa mkulima anayejiita hivyo anamiliki hisa kunako kampuni ya sumry kwa kiasi kikubwa sana kupitia kampuni moja hiv iliyoko arusha
huyu ni msanii, wengi ya watanzania wakuzaliwa wenye umri wake ni watoto wa wakulima, hivi utamuelewa mtu anayetoa vibali vya manunuzi ya magari ya serikali, anapiga marufuku ununuzi wa mashangangi kupunguza gharama zisizo za uhumimu, anajipitishia shangingi lake anapokabidhiwa analikataa, kutuhadaa sisi wananchi. Jiulize alikuwa amekusudia nini?, gari likishanunuliwa ukitaka kuliuza linauzwa kama second hand kwa bei ya chini, hapa ni kama mbinu, ni kutaka azuwe kwa bei ya chee kama ilivyombinu ya wakubwa wengi wenye element za kifisadi. Sasa ukulima hapo upo wapi? Au atueleze alilirudisha kwa wauzaji?
 
Mimi kwa mawazo yangu Mh.Pinda ni kiongozi ambaye ni mkweli na mwenye msimamo, tusianze kumlahumu wakati hatujuhi ni kitu gani kinajili behind the SCENE. Msikilizeni kwa makini anapozungumzia maswala ambayo yamekaa ndiyo sivyo Serikalini, mara nyingi anachukua RISK ya kukubaliana na maoni ya wabunge na kuachilia mbali mambo ya collective readership-huu ni ujasiri mkubwa sana lakini hilo watu awalioni! Chukulia mfano wa kauri yake kuhusu sakata la Mh. Jairo nadhani hicho ndio kingekuwa kipimo cha kumtathimini Mh. Pinda kwamba ana uzalendo wa kweli kweli - we sema mambo mengi yako nje ya mamlaka yake, sasa afanye NINI?

Tusianze kumlahumu kwenye vitu ambavyo ni obvious, he can't move mountain SOLO - yeye ni binadamu kama sisi, sasa anapojikuta yuko katikati ya ROCK and hard PLACE unategemea atafanya mihujiza GANI.
 
mtoto wa mkulima wa wapi labda wa jembe linalovutwa na V8 GX...alianza siasa zake kwa kujidai analia lia watu tumemstukia analeta siasa tu na machozi yake ya kinafki...TOA UYOOO
 
walatini walikuwa na msemo huu "Nemo dat quod non habet" Kwa taasifiri yangu ni kuwa huwezi kutoa ambacho huna, ni sawa yeye ni mtoto wa mkulima lakini hana roho ya mkulima. hawezi kuwa shujaa wakati hana roho ya ushujaa, hawezi kujiamini kama hana roho ya kujiamini. Hivyo hana ujasiri kama wa Sabodo. Na mbaya sana kwa sisi tutukao mjini huwa tunashangaa kwa muda mrefu sana na tunajitumbukiza kulingana na mkumbo. Mob psychology ya Mafisadi ukiwa nayo karibau utaiepa kwa vipi? Kuiepa angejiuzulu ukulu na hata chama na kujiunga na mapambano kama akina Slaa, h
 
mie bado nasema huyu jamaa ni wa kuadhibiwa akiwa wa kwanza. naona baadhi ya wadau wanasahau kuwa huyu jamaa na waziri mkuu. waziri mkuu ni mtu mwenye wadhifa mkubwa sana serikalini, huyu ana mamlaka makubwa na heshima. huyu jamaa angekuwa msafi tusingekuwa tumefika hapa tulipo, mind you huyu jamaa ni mkongwe na pia sioni sababu za yeye kuwa muoga kama sio kwamba na yeye yuko kwenye system. huyu jamaa yupo kwenye kila deal tunayosikia. hata kama mawaziri wale nane wataondoka, na huyu awafuate
 
Mimi kwa mawazo yangu Mh.Pinda ni kiongozi ambaye ni mkweli na mwenye msimamo, tusianze kumlahumu wakati hatujuhi ni kitu gani kinajili behind the SCENE. Msikilizeni kwa makini anapozungumzia maswala ambayo yamekaa ndiyo sivyo Serikalini, mara nyingi anachukua RISK ya kukubaliana na maoni ya wabunge na kuachilia mbali mambo ya collective readership-huu ni ujasiri mkubwa sana lakini hilo watu awalioni! Chukulia mfano wa kauri yake kuhusu sakata la Mh. Jairo nadhani hicho ndio kingekuwa kipimo cha kumtathimini Mh. Pinda kwamba ana uzalendo wa kweli kweli - we sema mambo mengi yako nje ya mamlaka yake, sasa afanye NINI?

Tusianze kumlahumu kwenye vitu ambavyo ni obvious, he can't move mountain SOLO - yeye ni binadamu kama sisi, sasa anapojikutaw yuko katikati ya ROCK and hard PLACE unategemea atafanya mihujiza GANI.

Ckubaliani nawe kwa namna moja kuwa asilaumiwe. Kama unaithamini na kujua maana ya utawala bora na uwajibikaji huwezi kusema asilaumiwe. Hapa ni suala la uwajibikajitu. Ukisema ni binadamu tu haitoshi ndio maana tumetungiwa na tukajitungia sheria, taratibu na kanuni ili kudhibiti ubinadamu wetu. Kama kashindwa kuwajibika ni kwa nini asijiuzuru kama akina mrema akina Mwinyi ambao wanaheshima zao mpaka sasa. Tusiutetee ubinadamu wetu wakati tayari tuanavitu nya kuudhibiti.Kwa nini mtu hajisaidi barabarani ovyo na watu wakimtazama na kusema ah ni binadamu na kwa kuwa binadamu ni mnyama pia alibananwa na tatizo. Tutakuona umechanganyikiwa. Na kiongozi aliyeapa kulinda sheria na katiba vile vile akiogopa eti ni binaodamu tena mwaga hafai kuongoza watu.
 
Hana mvuto wa kiutendaji wa kufanya Taifa lielewe nia ya serikali kusaidia wananchi. M4c ameanza kueleweka vizuri kwa wananchi na soon CDM wata-take over,
 
Wakuu mengi yamesemwa. Pinda ni mtoto wa mkulima kwa maana ya kuwa kazaliwa katika familia ya mkulima maskini.Pinda ni mtu wa busara na hekima sana kwa wanao mfahamu. Tatizo yupo ndani ya system yenye hulka ya kifisadi. Ndiyo maana kauli zake na maamuzi yake yanatofautiana na JK.JK ana kundi lake la mafisadi ambao ndio wanaomsaidia kuendesha nchi hii. Kesi zote zilizopo mahakamani i upuuzi mtupu.Cheo kikubwa lakini hakina meno. Makali anayo mtoto wa Msoga. Pinda ni jogoo wa shamba hawezi wika Pwani.
 
pinda hana lolote la kijivunia, kiutendaji kwa kuchambua, kufuatilia na kusimamia, heri mara mia mpiga deal lowassa. Lowassa alikuwa anawakimbiza mchwa wa kwenye halmashauri za miji. Wakurugenzi na wakuu wa wilaya na vigogo uchwara wa wilayani, walikuwa wanapata shida wakikumbana uso kwa uso na fisadi huyo.

Pinda yeye ni mtu wa kulalamika, mtoa ahadi na mipango isiyo na tija kwa wakati, pia ni mtu wa kulia lia kama mtoto! Hafai kuwa pm kwa nchi yenye changamoto nyingi kama hii.
hivi lile v8 alilolikataaga ili kubana matumizi akasema la zamani bado jipya lilirudishwaga toyota eeh? Au bado linakula wese letu kama kawa hebu tupeni ripoti tujue huyu mkulima alitupiga fiksi au vp?
 
Niliwahi kusoma makala moja ktk gazeti la raia mwema iliyoandikwa na mjengwa, akisimulia kisa cha mfalme mmoja mwaminifu kwa nchi yake, ni kisa cha kuwasha na kuzima mishumaa. Kwamba mfalme huyo alitembelewa na mgeni nyumbani kwake, bila shaka mgeni huyo alikuwa ni mwandishi wa habari, hivyo alikuwa akimhoji mfalme maswali mbalimbali. Wakati mfalme akihojiwa maswali hayo alikuwa akiwasha mshumaa fulani, mara anauzima na kuwasha mshumaa mwingine kwa kipindi chote cha mahojiano. Kitendo hicho kilimshangaza sana yule mgeni, kwa kuwa hakuwa ameelewa mantiki ya mfalme yule kuwasha na kuzima mara mshumaa ule mara huu, na hatimaye swali la mwisho alimuuliza mfalme yule ni kwanini katika muda wote wa mahojiano alikuwa anawasha na kuzima mishumaa, kwamba ni kwanini baada ya kuwasha mshumaa wa kwanza hakusubiri uishe ndio awashe mshumaa mwingine. Mfalme yule alimjibu kwamba alikuwa akiwasha na kuzima mishumaa ile kulingana na maswali aliyokuwa akiulizwa na mgeni yule, kwamba alikuwa akiulizwa maswali ya kiofisi kama mfalme anawasha mshumaa wa serikali, na pale alipokuwa akiulizwa masuala binafsi yaani yasiyo ya kiofisi kama vile idadi ya watoto wake, wake zake na mifugo yake alikuwa akizima mshumaa wa serikali na kuwasha mshumaa wake, kwa kuwa haikuwa maadili kwake kutumia mali ya serikali kwa mambo yake binafsi.
Baada ya kueleza kisa cha mfalme huyo, sasa ngoja nieleze ni kwa vipi Waziri mkuu Pinda ni fisadi kama walivyo mafisadi wengine nchini. Nilitembelea wilaya ya Mpanda Mkoa mpya wa Katavi mwezi August mwishoni mwaka huu. Nikiwa huko nilishangaa kukuta magari mengi makubwa ya JWTZ yakibeba matofali kutoka Mpanda mjini kuyapeleka Mpimbwe kibaoni nyumbani kwa waziri mkuu. Nikamuuliza dereva mmoja wa magari hayo kama walikuwa wakijenga kambi ya jeshi huko.Akanijibu hapana, hawajengi kambi, wao wapo kule kwa ajili ya kubeba mahindi ya serikali toka Sumbawanga kuyapeleka Mpanda ambapo yanapandishwa kwenye garimoshi kwenda kwenye maghala ya akiba ya taifa kanda ya ziwa. Kwa hiyo wakifika mpanda wakishusha mahindi wanapakia matofari ya kuchoma ya waziri mkuu na kuyasusha kibaoni kwa waziri mkuu umbali wa kama km 100 toka mpanda mjini kisha kuendelea hadi sumbawanga kupakia mahindi, na wanaendelea hivyohivyo. Nilishangaa sana, na nikauliza kwanini basi hakufyatulia matofali hayo hukohuko kibaoni badala ya kufyatulia mjini na kuyabeba kuyapeleka kijijini, akanijibu kwamba kule kibaoni haikuwa rahisi rahisi kwake waziri mkuu kupata wafungwa wa kumfyatulia matofari yale. Hapo nikaelewa kwamba kumbe licha ya kutumia magari ya JWTZ kubeba matofali yake hata hayo matofari katumia rasilimali ya serikali kuyafyatua, na huu ni ufisadi mkubwa uliopitiliza. Kutumia wafungwa kufyatua matofali ya mtu binafsi ni ufisadi, na kutumia magari ya JWTZ kubeba matofali hayo ni ufisadi pia kwa kuwa hata kama magari yale yanapita pale kwa waziri mkuu, lakini bado yanakuwa yametumia muda mwingi wa kupakia na kushusha matofali yale na hivyo zoezi la kubeba mahindi litachukua muda mrefu zaidi kwa sababu yake. Kitendo hicho ni ufisadi mkubwa, na hamna namna yoyote ya waziri mkuu kujitetea kwa hili, na kama ingekuwa ni nchi ya maadili kama nchi za wenzetu hili pekee linatosha kwa waziri mkuu kujiuzulu kwa ufisadi.
 
Niliwahi kusoma makala moja ktk gazeti la raia mwema iliyoandikwa na mjengwa, akisimulia kisa cha mfalme mmoja mwaminifu kwa nchi yake, ni kisa cha kuwasha na kuzima mishumaa. Kwamba mfalme huyo alitembelewa na mgeni nyumbani kwake, bila shaka mgeni huyo alikuwa ni mwandishi wa habari, hivyo alikuwa akimhoji mfalme maswali mbalimbali. Wakati mfalme akihojiwa maswali hayo alikuwa akiwasha mshumaa fulani, mara anauzima na kuwasha mshumaa mwingine kwa kipindi chote cha mahojiano. Kitendo hicho kilimshangaza sana yule mgeni, kwa kuwa hakuwa ameelewa mantiki ya mfalme yule kuwasha na kuzima mara mshumaa ule mara huu, na hatimaye swali la mwisho alimuuliza mfalme yule ni kwanini katika muda wote wa mahojiano alikuwa anawasha na kuzima mishumaa, kwamba ni kwanini baada ya kuwasha mshumaa wa kwanza hakusubiri uishe ndio awashe mshumaa mwingine. Mfalme yule alimjibu kwamba alikuwa akiwasha na kuzima mishumaa ile kulingana na maswali aliyokuwa akiulizwa na mgeni yule, kwamba alikuwa akiulizwa maswali ya kiofisi kama mfalme anawasha mshumaa wa serikali, na pale alipokuwa akiulizwa masuala binafsi yaani yasiyo ya kiofisi kama vile idadi ya watoto wake, wake zake na mifugo yake alikuwa akizima mshumaa wa serikali na kuwasha mshumaa wake, kwa kuwa haikuwa maadili kwake kutumia mali ya serikali kwa mambo yake binafsi.
Baada ya kueleza kisa cha mfalme huyo, sasa ngoja nieleze ni kwa vipi Waziri mkuu Pinda ni fisadi kama walivyo mafisadi wengine nchini. Nilitembelea wilaya ya Mpanda Mkoa mpya wa Katavi mwezi August mwishoni mwaka huu. Nikiwa huko nilishangaa kukuta magari mengi makubwa ya JWTZ yakibeba matofali kutoka Mpanda mjini kuyapeleka Mpimbwe kibaoni nyumbani kwa waziri mkuu. Nikamuuliza dereva mmoja wa magari hayo kama walikuwa wakijenga kambi ya jeshi huko.Akanijibu hapana, hawajengi kambi, wao wapo kule kwa ajili ya kubeba mahindi ya serikali toka Sumbawanga kuyapeleka Mpanda ambapo yanapandishwa kwenye garimoshi kwenda kwenye maghala ya akiba ya taifa kanda ya ziwa. Kwa hiyo wakifika mpanda wakishusha mahindi wanapakia matofari ya kuchoma ya waziri mkuu na kuyasusha kibaoni kwa waziri mkuu umbali wa kama km 100 toka mpanda mjini kisha kuendelea hadi sumbawanga kupakia mahindi, na wanaendelea hivyohivyo. Nilishangaa sana, na nikauliza kwanini basi hakufyatulia matofali hayo hukohuko kibaoni badala ya kufyatulia mjini na kuyabeba kuyapeleka kijijini, akanijibu kwamba kule kibaoni haikuwa rahisi rahisi kwake waziri mkuu kupata wafungwa wa kumfyatulia matofari yale. Hapo nikaelewa kwamba kumbe licha ya kutumia magari ya JWTZ kubeba matofali yake hata hayo matofari katumia rasilimali ya serikali kuyafyatua, na huu ni ufisadi mkubwa uliopitiliza. Kutumia wafungwa kufyatua matofali ya mtu binafsi ni ufisadi, na kutumia magari ya JWTZ kubeba matofali hayo ni ufisadi pia kwa kuwa hata kama magari yale yanapita pale kwa waziri mkuu, lakini bado yanakuwa yametumia muda mwingi wa kupakia na kushusha matofali yale na hivyo zoezi la kubeba mahindi litachukua muda mrefu zaidi kwa sababu yake. Kitendo hicho ni ufisadi mkubwa, na hamna namna yoyote ya waziri mkuu kujitetea kwa hili, na kama ingekuwa ni nchi ya maadili kama nchi za wenzetu hili pekee linatosha kwa waziri mkuu kujiuzulu kwa ufisadi.

Janja yake kulia bungeni kupoteza maboya. Muulize Tibaijuka kaishia wapi na vigelegele!
 
kaka nchi hii ni ya ajabu sana nafikiri inahitajika kuwekwa kwenye record za dunia viongozi wetu ni wa ajabu sana tumuombe Mungu tu lakini watu kama wa kina Pinda ni balaa kubwa kwa mustakabali wa nchi hii
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom