Nionavyo Mimi: Hizi ndio Tabia Kuu za Watanzania [Sterio Type]

Huku ni kukosa ustaarabu kabisa na kuingilia privacy za watu!
Huwezi kumpa namba yangu mtu mwingine bila kuniuliza.


Mkuu Sumba-Wanga, hayajakukuta haya na unaishi hapa Tanzania? Kitu privacy hapa Bongo hakuna yaani ni kama ziro tu, we umelala mtu kapata namba yako ya simu toka kwa mtu mwingine ambaye huna hata mpango naye utaona anakupigia simu na kuongea utumbo. Unashangaa hata na fulani ana namba yako, kaipataje? Mimi niliachwa hoi mwaka jana, yaani jamaa walikuwa wanabishania usajili wa wachezaji wa Yanga kijiweni tu. Katika hali isiyo ya kawaida, jamaa mmoja mlalahoi tu (anazoa takataka hapa mtaani na mkokoteni) kwa hasira akasema Yanga isipotwaa ubingwa mwaka jana angempigia simu Ridhiwani Kikwete amtukane kwani yeye Ridhi anahusika na usajili pale Yanga. Watu wakacheka sana na kumkashifu jamaa. Kwa kuondoa ubishi, jamaa akampigia Ridhiwani simu bahati nzuri Ridhi hakupokea. Toka silu ile mpaka leo jamaa anaitwa mshikaji, yaani kaacha kudharauliwa kisa anaijuwa namba ya simu ya Ridhiwani.
 
Last edited by a moderator:
mh...lafudhi kubwa manake nini?

Tabia nyingine ya waTz (haikeri lakini inashangaza), ni watu kujudge lafudhi za watu hasa za english. Sasa unataka wale wa 'ze windi izi blowingi'??

bubbs, lafudhi kubwa ni kama ile mnayoitumia nyie watangazaji wa Clouds. In short, ni kule kuongea English kwa kulazimisha kama walivyo watangazaji wengi wa redio hapa nchini au vijana walio wengi. Utakuta mtu anajitahidi kuongea kiingereza na kutia broken words huku akivuta maneno ambayo hatamki vizuri mpaka unajiuliza, what's the point kwa mtu kama yule kuongea lugha kwa kulazimisha. Huku si ku judge bali ni ujinga kwa anayejuwa hali halisi. Don't pretend to be who you are NOT, be yourself kwani ukiongea kiswahili the majority wanakuelewa.
 
Last edited by a moderator:
Mtu katoka kukojoa uchochoroni bila hata kunawa, then anakupa mkono kukusalimia, yaani harufu yote ya joto la pumbu linakuwa mikononi mwako.
 
Mtu kaja kwako siku moja tu na kamwona mkeo. Kesho anakuja peke yake na kilo ya nyama wakati wewe uko kazini, then kwa ujanja anamuomba mkeo nafasi ya kulala kwenye kochi huku mkeo akishughulikia ile nyama jikoni.
 
Saa tano usiku mtu anakupigia simu anakuja nyumbani kwako kuangalia mechi za Premier League wakati bar zinazo onyesha hizo mechi zipo kibao.
 
Wanawake wanaotoa maziwa yao hadharani na kunyonyesha watoto wao bila hata kujifunika na kanga!

Sasa kwani wawanyonyesheje jamani na wewe? Mbona unacomplicate maisha! Pata picha bebi anaangua kilio kikali wakati uko kwenye basi unasafiri, what will u do?
 
  1. Kuomba umkopeshe huku akiahidi kukurudishia kwa muda fulani, unashangaa muda huo unapita na wala hakupi feedback yoyote...hata ukimkumbushia anakuwa hasense kabisa!
  2. Mtu kukubip afu unapiga anakwambia nilitaka kukusalimia
  3. Mtu mzima kutumia choo akatoka bila kuflash
  4. Mtu kukutembelea muda ukaisha akawa anadeley kuondoka
 
ananikera mtu:
  1. anayeshindwa kufanya maamuzi haraka
  2. hajishughurishi kufanya mambo yanakayomletea maendeleo badala yake anakaa kulaumu waliofanikiwa
  3. anayejiunga na SUPER CHEKA kwa lengo la kupiga simu akupumzikie bile kujali we una ratiba gani kwa muda huo
 
Sasa kwani wawanyonyesheje jamani na wewe? Mbona unacomplicate maisha! Pata picha bebi anaangua kilio kikali wakati uko kwenye basi unasafiri, what will u do?

Kwa hiyo na wewe utalitoa wazi tu?
hebu jaribu kufanya hivyo kwenye dala dala uone utaambiwa nini?
Kwani huna kanga?
Si ufuike ziwa lako na kanga wakati jamaa ana enjoy?
Ziwa halina maana hadi ulimwage wazi wazi tu?
 
ananikera mtu:
  1. anayeshindwa kufanya maamuzi haraka
  2. hajishughurishi kufanya mambo yanakayomletea maendeleo badala yake anakaa kulaumu waliofanikiwa
  3. anayejiunga na SUPER CHEKA kwa lengo la kupiga simu akupumzikie bile kujali we una ratiba gani kwa muda huo

No2 ndio ule ujinga wa kusema liyejuu mngoje chini badala ya kumpandia huko huko juu
No 3 inakera sana
 
Mizaha mizaha hata kwenye mambo ya msingi kisingizio eti maisha magumu kwa hiyo huhitaji kuitumikisha sana akili!Hii kwa kawaida huwa ni tabia ya watu wenye mtindio wa ubongo

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums


Mhh hapo umepiga Ikulu
 
Mijitu inayocheua kwa sauti.

Unakuta jitu limekula kuku-makange halafu linashushia ama na bia au koka kola, migesi inajaa tumbo halafu lenyewe linacheua kwa sauti kama mbuzi....burrrrrrp

Wakati linacheua linakuwa linajichokonoa kwenye meno kuondoa vinyama vilivyonasa. Na mbaya zaidi huo mcheuo utoe harufu.

Ukiwa na kinyaa kama cha Nyani Ngabu unaweza ukapatwa na kichefuchefu kabisa.

Cc: The Boss
Bcc: King'asti

On top of that; jingine linatafuna kwa sauti kama mbwa au paka akinywa maziwa. Mimi sielewi malezi mengine ya wapi? Inakera mno kama tuna tabia hizi lazima tuziache.
 
kurushia maji watembea kwa miguu ukiwa kwenye gari lako, hasa wakati huu wa mvua.
 
This is very serious! INa maana wataanza kuja nyumbani kwako ukiwa kazini!


Oh Yes, na wakija wanakuta chakula kwenye hot pot. Watakula na pengine watalala kitandani kwako kukusanifu tu huku wakipena raha zao na kulowesha shuka zako, wewe uko kazini unamenyeka kutafuta pesa za kumlipa house girl wako. Mimi na biashara ya ma house girl sina kabisa kwani wengi wao ni machangu toka huko walikotoka wanakuja mjini kuendeleza libeneke lao.
 
Huyo ana lake jambo......


Anakuja kucheck jinsi atakavyopokelewa na mkeo ama house girl wako ili siku nyingine apate nafasi ya kuja nyumbani kiulaini wakati wewe ukiwa kazini. Na utashangaa ipo siku atakuja kwako wakati wewe upo kazini na hakuambii kama alikuwa kwako.
 
Oh Yes, na wakija wanakuta chakula kwenye hot pot. Watakula na pengine watalala kitandani kwako kukusanifu tu huku wakipena raha zao na kulowesha shuka zako, wewe uko kazini unamenyeka kutafuta pesa za kumlipa house girl wako. Mimi na biashara ya ma house girl sina kabisa kwani wengi wao ni machangu toka huko walikotoka wanakuja mjini kuendeleza libeneke lao.

Nasikia harufu ya damu....
 
Back
Top Bottom