Nionavyo lengo la wiki ya usalama barabarani ni kuuza stika, anayeamini kupungua kwa ajali anieleze ni kwa vipi

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Jan 26, 2013
18,658
22,255
Kila mwaka polisi huandaa wiki ya usalama barabarani lakini hali ilivyo barabarani ni ileile ya siku zote zaidi ya kuuziwa stika ambazo hazipunguzi ajali! Vurugu za bodaboda na daladala ziko vilevile na pacha wao ajali.

Mimi naona lengo si kudhibiti ajali kwa kuwakumbusha madereva juu ya matumizi sahihi ya barabara, wiki ikiisha hatujulishwi polisi wamekusanya pesa kiasi gani na zimeingizwa kwenye akaunti gani ya serikali.

Ipo haja ya kuubadili mwenendo wa wiki hii ya usalama barabarani isilenge mapato ila ilenge matumizi sahihi ya barabara.
 
kuna tatizo kubwa sana ndani ya jeshi la polisi na sina hakika igp anaweza kulifimua na kuliunda upya jeshi hili.
Post hii nimeiandika nikiwa Mbagala Rangitatu, eneo hili ni sawa na mto wenye mamba wengi wanaosubiri wanyama wawakamate wavukapo mto, hapa kuna bodaboda nyingi sana na zinatumia barabara kiholela shoto kulia na kwa mwendo kasi bila kujali na sehemu ya watembea kwa miguu au la, wao barabara zote ni zao! Eneo hili kila siku watu hugongwa na hasa usiku ndiyo balaa kwani ukiangalia kulia utagongwa na anayetokea kushoto, wao wako huru kutumia barabara watakavyo, hawa hawauziwi stika wala hawaulizwi leseni ya udereva, mungu awepe nini zaidi.
 
Bei za Stika
Private car stika ya 3000 inauzwa 5000. Stika ya 5000 (commercial vehicles) inauzwa 8,000 mpaka 10,000!
Binafsi sielewi kazi ya hizo stika na kwa nini zinauzwa! Nahisi ni may be ni chanzo kingine tu cha mapato !
 
Bei za Stika
Private car stika ya 3000 inauzwa 5000. Stika ya 5000 (commercial vehicles) inauzwa 8,000 mpaka 10,000!
Binafsi sielewi kazi ya hizo stika na kwa nini zinauzwa! Nahisi ni may be ni chanzo kingine tu cha mapato !
Lengo ni kukusanya hela ya kununua maziwa kwa ajili ya kufuta vumbi kooni, kubrashi mabuti na kununulia jiki ya kufulia unifomu.
 
Bei za Stika
Private car stika ya 3000 inauzwa 5000. Stika ya 5000 (commercial vehicles) inauzwa 8,000 mpaka 10,000!
Binafsi sielewi kazi ya hizo stika na kwa nini zinauzwa! Nahisi ni may be ni chanzo kingine tu cha mapato !
kwa sasa sticker kwaajili ya private car ni Tsh 5,000/= na sio elfu 3 mkuu... Imepanda
 
Kila mwaka polisi huandaa wiki ya usalama barabarani lakini hali ilivyo barabarani ni ileile ya siku zote zaidi ya kuuziwa stika ambazo hazipunguzi ajali! Vurugu za bodaboda na daladala ziko vilevile na pacha wao ajali. Mimi naona lengo si kudhibiti ajali kwa kuwakumbusha madereva juu ya matumizi sahihi ya barabara, wiki ikiisha hatujulishwi polisi wamekusanya pesa kiasi gani na zimeingizwa kwenye akaunti gani ya serikali.
Ipo haja ya kuubadili mwenendo wa wiki hii ya usalama barabarani isilenge mapato ila ilenge matumizi sahihi ya barabara.
Mtu mweusi hana uwezo wa kuongoza hata watu wa some vitabu viahamie vichwani hivio kuwalaumu ni sawa na kumlaumu mtoto mchange hasie weza kujisimamia
 
Tatizo uchumi unatumikia siasa chama cha mapiduzi na viongozi wa serikali waliochaguliwa wako tayari kutumia fedha za serikali kuhakikisha ccm inasalia madarakani.
 
kwa sasa sticker kwaajili ya private car ni Tsh 5,000/= na sio elfu 3 mkuu... Imepanda
Kama ni hivyo hizo stika kuzipata itakuwa shida, ulipokuwa ukiwapa 5000 hawarudishi chenji na ukija na chenji kamili hauudumiwi, au utaudumiwa kwa kuchelewa sana
 
Back
Top Bottom