Brooklyn
JF-Expert Member
- Mar 17, 2009
- 1,459
- 284
Hivi wadau mke wa Rais ni kiongozi wa serikali? Nimesoma vizuri katiba yetu ya JMT, hakuna ibara hata moja inayotamka kutambua nafasi ya mke wa Rais wa JMT na naamini hakuna sheria inayompa madaraka ya kusomewa taarifa za maendeleo ya mikoa, potelea mbali misululu ya magari ya serikali anayoambatana nayo pamoja na yale ya viongozi wanaokwenda kumpokea.
Ninastaajabishwa na kuendelea kuchezea hovyo hovyo rasilimali za taifa hili katika mambo yasiyo na tija. Picha hapo chini zinaonyesha viongozi wa mkoa wa Lindi waliokwenda kumpokea mke wa rais. Naamini WAMA ni taasisi ya binafsi ya mke wa rais na maswahiba wake, ingawa anatumia nafasi na ushawishi aliyonayo pale ikulu ku solicit misaada kutoka kwa wafadhili ambayo hatujui nani ananufaka mwisho wa siku. Nasema hivi kwa sababu taasisi ya mke wa Rais mstaafu Benjamin Mkapa, tuliambiwa ni ya kwake binafsi. Kwa hivyo mumewe alipoondoka madarakani, naye akaondoka na taasisi yake.
Wakati wa kampeni za kuwania Urais mwaka jana, Mama Salma alidiriki kutumia ndege za serikali kumkampenia mume wake Mh. Rais Kikwete.
Wana JF mnalionaje hili? Binafsi linanikwaza sana!!
http://mohammeddewji.com/blog/wp-content/uploads/2011/04/Picha-no-14.jpg
Ninastaajabishwa na kuendelea kuchezea hovyo hovyo rasilimali za taifa hili katika mambo yasiyo na tija. Picha hapo chini zinaonyesha viongozi wa mkoa wa Lindi waliokwenda kumpokea mke wa rais. Naamini WAMA ni taasisi ya binafsi ya mke wa rais na maswahiba wake, ingawa anatumia nafasi na ushawishi aliyonayo pale ikulu ku solicit misaada kutoka kwa wafadhili ambayo hatujui nani ananufaka mwisho wa siku. Nasema hivi kwa sababu taasisi ya mke wa Rais mstaafu Benjamin Mkapa, tuliambiwa ni ya kwake binafsi. Kwa hivyo mumewe alipoondoka madarakani, naye akaondoka na taasisi yake.
Wakati wa kampeni za kuwania Urais mwaka jana, Mama Salma alidiriki kutumia ndege za serikali kumkampenia mume wake Mh. Rais Kikwete.
Wana JF mnalionaje hili? Binafsi linanikwaza sana!!
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo nchini (WAMA) mama Salma Kikwete akipokewa na viongozi mkoa wa Lindi mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege mkoani Lindi leo. Mama Salma Kikwete yuko mkoani humo kushiriki na kuhimiza shughuli za maendeleo ya wananchi.(Picha na Aron Msigwa MAELEZO).
http://mohammeddewji.com/blog/wp-content/uploads/2011/04/Picha-no-14.jpg