Nini tunajifunza kutokana na kuliki kwa taarifa za NSA toka kwa Edward Snowden?

Kilongwe

JF-Expert Member
Feb 7, 2008
423
115
privacy.jpg
Katika habari zilizotawala uwanja wa Tehama kwa wiki hizi ni habari ya Snowden, mfanyakazi wa shirika la usalama la marekani (NSA) pia ni muajiriwa wa zamani wa CIA aliyelikisha taarifa za siri zinazoelezea jinsi marekani inavyofuatilia taarifa za watumia mtandao bila idhini yao. Kuna wanaomuona Snowden kama hero na wengine wanamuona kama msaliti. Kulingana na maelezo ya Snowden kama alivyonukuliwa na mtandao wa Guarnian, inamaana kila unachoongea, unachotuma kinachunguzwa, wanafanya hivi kila mahali hadi kwa washika dau wakuu kwenye hii nyanja ambao ni Facebook na Google. Taarifa inaelezea kuwa, mashirika haya yametakiwa kuwapa NSA uwezo wa kuingia kwenye mitambo yao na kuchota chochote wanachotaka bila taarifa ya ziada. Snowden ameamua kutoa taarifa hizi kwa kile alichokiita ni kuingiliwa kwa uhuru na unafasi wa watu (Privacy). HUYU NDIYE SNOWDEN, anasema hayuko tayari kukaa dunia ambayo kila anacho fanya kina rekodiwa Katika maelezo yake, Snowden anasema, taarifa nyingi zinazochunguzwa ni za watu na sio mashine hivyo watu hawa hawapo huru tena. Hii inakuja wakati serikali ya marekani ipo katika mvutano mkubwa wa masuala ya uvamizi wa mtandaoni na serikali ya China.

Siku chache zilizopita niliwahi kupata nafasi ya kuzungumza na professor mmoja anayejihusisha sana na mambo ya tafiti za mitandao hapa China, tulizungumza mengi, ila moja ya topiki ya mazungumzo ilikuwa ni kuhusu sababu za China kuzuia na kuendelea kuzuia mitandao mikubwa kama Google, Facebook, Twitter nk. Yeye alisema, sio tu kuwapa nafasi wataalamu wa nyumbani toka ushindani wa mataifa makubwa kama marekani bali pia hakuna kuaminiana kati ya nchi hizi mbili. Ukweli ni kuwa, kuna mambo mengi sana yanayoendelea nyuma ya panzia. Aliongelea mambo mengi, pia akanigusia suala la vikwazo kwa Huawei, malalamiko ya marekani kufanyiwa uspy na China nk. Hivyo, kitu kimoja nilichojifunza hapa ni kuwa, jamaa wanajuana na ndio maana hawaaminiani. Nilipomuuliza je kuna sababu nyingine yoyote, alijibu, "Ken ding ya" akimaanisha haswaa. Sababu nyingine aliyoelezea ni kuwa ni jambo la hatari endapo nchi haitokuwa na umiliki wa taarifa muhimu za watu wake, hivyo kitendo cha kuruhusu makampuni ya kichina kuwa na vitu vya inawasaidia kuwa na jeuri na uwezo wa kulinda vitu vyao. Hii ilinifanya nikumbuke lile vuguvugu la mapinduzi ya nchi za warabu (haswaa Tunisia) lilihamasishwa sana ndani ya Facebook.

Wakati ninatafakari na kutafuta baadhi ya reference kwa ajili ya makala hii, nikasema niende Facebook (ingawa ninajua kuwa ninafuatiliwa, hehe) ili nipate baadhi ya taarifa, nikakutana na picha kwenye ukurasa wa Masanja Mkandamizaji juu ya majina ya waliochaguliwa kujiunga na JKT, kwakuwa mimi ni mmoja wa wapenzi namba moja wa JKT, nikasema ni ngoja nikasome majina ya hawa vijana, nilipofika kule, nikakutana na ujumbe mzito " Bandwidth Limit Exceeded". Hii ikanipa mwanga zaidi wa kufikiria katika mtazamo mwingine.

jkt.jpg

Wavuti ya JKT kama ilivyokuwa inaonekana leo asubuhi.
Ukweli usiopingiza kuwa masikini hana staha, masikini hana chaguo na wala kuthaminiwa. Hivyo inabidi kujithamini wewe mwenyewe. Kama tukiangalia matuko haya yanayoendelea ni dhahiri, tunajifunza kitu kimoja, imefika wakati sisi kujithamini wenyewe. Tunaishi kwenye dunia yenye mashindao makubwa huku tukiwa kama nyama iliyonona inayogambaniwa na watu. Tumeona ni jinsi gani mataifa makubwa (US & China) wanayotupa kipaombele, hii si bure, na mtu hawezi kukupa kipaombele bila kujua nini kinaendelea kwako. Pia ni lazima kila mmoja wao atataka kujua nini unafanya na mpizani wake ili na yeye ajiandae vyema. Hivyo, tujue kwamba"TUNAFUATILIWA" kwa kina.

Baada ya kuona tukio la JKT, nilituma makala kwenye Facebook yangu, kuna marafiki zangu wengi walichangia, na kunitumia tovuti ya idara ya serikali ambayo ni muhusika mkuu wa shughuli za IT za serikali, Mwanzo : Wakala ya Serikali Mtandao nilitumia muda kupitia wavuti yao kuona nini lengo la hawa mawakala. Kitu ambacho nimejifunza ni kuwa bado kuna changamoto nyingi, kwa mfano, idara inayotegemewa kuja kuwa mkombozi mfumo mzima wa EGA ni utekelezaji na si upangaji. Kwa haraka haraka tunaweza kusema, bado hatujafikia sehemu ya kupanga mfumo ambao utalinda na kuchunga uendeshaji wa serikali kwenye medani ya Tehama.

serikali.jpg

Mfano mzuri , siku zilizopita tumeona matukio mengi ya kuhakiwa kwa wavuti za wizara (Ikiwemo wizara nyeti ya mambo ya ndani), kuzidiwa kwa bandwidth kwa Necta na hii ya JKT nk. Jaribu kutembelea Tanzania Embassy In USA, utapelekwa Embassy of Tanzania | This is the Official website for the Embassy of Tanzania in the United States of America. ukienda ile ya Italia Ambasciata della Repubblica Unita di Tanzania - Tanzania kuna hadi adsense, je nani anachukua hizo $$ rudi kwenye tovuti mama ya taifa The Tanzania National Website uangalie tovuti walizoweka zipo hai na lini ni mara ya mwisho kusasishwa(updated)? . Je nani wa kulaumiwa, wachunga tovuti (Webmasters) au mfumo mzima? Wengi wanaweza kusema ni kutokana na kutokuwa na mawebmaster wasio na ujuzi. Ila hapa tatizo ni mfumo. Kama tuna mfumo mzuri ambao utayakinisha kazi za webmaster, utarativu wa utendaji wa hazina za IT nk basi kama kazi ulipewa na baba yako mdogo bila kuwa na ujuzi, utakimbia mwenyewe wala hautongojea kufukuzwa.

Dunia ya leo si salama, tumezungukwa na maadui kila pande, hivyo tunahitaji njia thabiti za kujilinda, na njia hizi hazitotoka kokote bali kutokana na mipango thabiti yetu sisi wenyewe (mlizi hawezi toka nje). Tunahitaji utaratibu (Framework) utakaoongoza na kufuatwa kila idara za serikali na za watu binafsi ndani ya mipaka ya Tanzania. Leo hii ni jambo la kawaida kwa kila idara kuwa na na mifumo ya kwao isiyofuata kanuni yoyote na huku wengine wasipokuwa nayo kabisaaa. Athari hizi sio tu kwa idara za serikali, bali pia hata kwa mashirika / watu binafsi.


Nini kifanyike?

Baada ya kuandika mengi, labda nitoe maoni yangu na nini kifanyike kuokoa hili jahazi, kwa njia moja au nyingine linaweza kusaidia wahusika katika kujitegemea kwenye nyanja ya IT.

1. Kuanzisha vituo vya tafiti na gunduzi (Innovation) vya Tehama kwenye vyuo vyote vikubwa vya serikali ambavyo vitahusika kuvumbua, kuratibu, kushauri na kuja na mambo mapya yenye manufaa kwa Tanzania kama nchi.
2. Kuanzishwa (kama ipo kupewa nguvu) tume itakayohusika na upangaji wa mfumo (framework) wa taifa kwa upande wa Tehama na , kusimamia utekelezaji na kuishauri serikali.
3. Tume ya utumishi kuangalia upya utaratibu wa kuajiri watu wa tehama ili kupata wenye vigezo na sio kupeana.
4. Serikali kutoa fursa zaidi kwa Watanzania walio nje ya nchi na wenye ujuzi wa kina kushiriki kwenye ujenzi wa Tehama ya Tanzania. Ingawa hii inaweza kuchukuliwa kivingine, ila ushahidi unaonesha kuna idadi kubwa ya Watanzania wanaofanya vyema kwenye makampuni / mashirika makubwa duniani kote. (China ina utaratibu wa kuandaa semina ya Wachina walio / waliokuwa nje (haswaa zile nchi bora) inawakutanisha na wenzao walio nyumbani kubadilisha ujuzi kwa mustakabali wa taifa, pia hutoa punguzo la kodi kwao pindi wanapotaka kuja kuwekeza / kurudi nyumbani).


Faida Zake:

1. Kutoka katika mikono ya mabepari ambao wanatufuatilia kila kitu tunachofanya.
2. Kuongeza ufanisi kwenye idara za serikali / binafsi.
3. Kuongeza ajira kwa vijana kwani fursa nyingi zaidi zitagunduliwa.
4. Kuwa na udhibiti mkubwa juu ya taarifa zetu / zinazotuhusu.


Yapo mengi sana ya kuandika, ila yalishanenwa kuwa, uzuri wa mambo ni yale machache na yenye kueleweka. Pia ni vyema kuwapa watu wengine zaidi kuchangia kwenye hili.

Imeandikwa Na: Mkata Nyoni
Chief Business Development Officer - Dudumizi Solutions
Email: mnyoni@dudumizi.com Web: www.mkatanyoni.com
 
Sasa tutafanya nin na sisi hatukugunduwa internet?. Hizo web za serikali zilizohackiwa hivi karibuni wakulaumiwa ni webmasters tu na si wengine.
 
ndio maana hakuna wachangiaji maaana waosha kinywa wengi kama mimi inatugusa hii mweee.. :heh:
 
Hao wazungu wameshawahi mkuu na ukizungumzia China nao wako mbali mno,sisi hatutaweza hata kidogo kwani kazi ni za kupeana kwa hiyo fani ya IT sehemu kubwa ni vilaza waliobobea.Nina mifano mingi sana hasa eneo ninalofanya kazi.Kuhusu watanzania ambao wako nje kuwa ni wazuri kwenye hii field nakubaliana na wewe 100% ila siunajua kuna yale mambo ya kujifanya vyuo vyetu eti ndio vinatoa wanafunzi bora kuliko wale walioko nje ya Tanzania imefikia mahala hata wakirudi nchini kazi hawapewi kisa vyuo vya ulaya ni vya kitapeli.
 
Hao wazungu wameshawahi mkuu na ukizungumzia China nao wako mbali mno,sisi hatutaweza hata kidogo kwani kazi ni za kupeana kwa hiyo fani ya IT sehemu kubwa ni vilaza waliobobea.Nina mifano mingi sana hasa eneo ninalofanya kazi.


Hapa pana mambo mawili, moja ni kuwa Jamaa wameendelea ila nao walianza kama sisi (Ingawa ni miaka mia kadhaa iliyopita), ila kutokana na kurahisishwa na maendeleo ya tecknology ya sasa, nina uhakika sisi hatutohitaji muda mrefu kama waliotumia hawa jamaa kuweza kufika walipo, nasema INAWEZEKANA ila SIO kitu cha siku moja, mwaka mmoja wala karne moja. Ni kitu cha muda mrefu mrefu mno, ila sasa ni muda wa kuweka mizizi, kujaribu kusetup short tern and long term goals, hizi short term ndio zitatusaidia kuwa na uwezo wa kufikia long term goals. Sisi kama vijana, tutumie chance na nafasi tuliyopata angalau kwa ajili ya nchi yetu.

Kuna kitu nataka kushare na watu labda kitakuwa na msaada, hapa China, kama huna hela (Hongo) au huumjui mtu (Guanxi aka kujuana) huwezi kupata kazi ya maana unless una kipaji cha kipekee sana. Kila sehemu kuna kujuana na kuwekana, nimelishuhudia sana sana. Na matatizo mengi tulio nayo na wao wanayo vilevile, ila jamaa tofauti ya wao na sisi ni.

1. China watu wao wengi wana knowledge na uwezo wa kawaida (skilled labor), kwakuwa wana ile spirit ya kuwork hard so kila mtu hujifunza kulingana na sehemu alipo / anayotaka, hivyo basi hata kama kazi amepewa mtoto wa binamu kwa kujuana, siku ya mwisho kazi itafanyika (kwa ubora) na matokeo yataonekana. Tatizo la sisi, jamii yetu wengi ni wababaishaji, hivyo ni mwendo wa ubabaishaji kwa kwenda mbele, hata ukipewa pande, utabolonga na hakuna matokeo.

2. China hawaendi kwa matukio na wanadream high, ukiwa China, no matter unatokea wapi, wao taifa wanalolizimia ni Marekani, nimeona hii tangu nimekuja mwaka wa kwanza, hii imewasaidia sana kuwafanya watu wake wote wawe na dream moja, kushindana na Marekani, hata kama wasipomfikia (itachukua karne) ila ipo siku watafika huko. Jamaa wanaplan za miaka mingi.

Hao wazungu wameshawahi mkuu na ukizungumzia China nao wako mbali mno,sisi hatutaweza hata kidogo kwani kazi ni za kupeana kwa hiyo fani ya IT sehemu kubwa ni vilaza waliobobea.Nina mifano mingi sana hasa eneo ninalofanya kazi.Kuhusu watanzania ambao wako nje kuwa ni wazuri kwenye hii field nakubaliana na wewe 100% ila siunajua kuna yale mambo ya kujifanya vyuo vyetu eti ndio vinatoa wanafunzi bora kuliko wale walioko nje ya Tanzania imefikia mahala hata wakirudi nchini kazi hawapewi kisa vyuo vya ulaya ni vya kitapeli.
Kuhusu waliosoma nje ni wakali au waliosoma nyumbani, kimtindo hakuna kipimo kwenye hili, na binafsi sina jibu sahihi kwani nina marafiki zangu wengi wamesoma Mlimani na ni wazuri, hivyo umesoma wapi sio big deal. Point yangu ilikuwa, kwa kusoma nje na ukawa makini (nina maanisha UKAWA MAKINI), utakuwa na ufahamu mkubwa wa hiyo Nchi, hivyo, kwa kuwapa nafasi watu hawa itasaidia sana muingiliano wa Tanzania na nchi husika, mfano mzuri mtu aliyesoma Marekani, akafanya kazi marekani na akawa na ujuzi wa maana, leo hii akuridu Tanzania, ni dhahiri atakuja na kitu kipya toka marekani, akija Tanzania atashare na walio nyumbani, vilevile ni sawa kwa wale wa China, Ulaya nk, so point yangu hapa ilikuwa ni KUIBA ujuzi na kurahisisha ufanyaji kazi. Mfano mzuri ni kuwa, kwa miaka kadhaa nimekuwa nikideal na makampuni ya kawaida ya hapa China na kuona jinsi jamaa wanavyotoka na kufanya mambo yao, hivyo ni dhahiri nikishare na Watz itakuwa na msaada kwao. Pia kama kuna project ya IT ya Tanzania, nikifanya na Mchina na nikawa mzalendo, n dhahiri nitakuwa katika nafasi nzuri ya kutetea masilahi ya nchi yangu kuliko yule aliye nyumbani kwani ninaweza kujua mchina anafikiria nini kwenye hii project hata asipoongea.


Muda umefika wa kuact badala ya kulalamika, so vjana tuwe mfano kwa kuwork hard kwa kila nafasi tutakayopewa, jaribu wewe kuwa wa mfano angalau kwa ucache wake, ipo siku mabadiriko ya ukweli yatakuja.
 
Vijana wengi wa Tanzania ni wabinafsi na wachoyo huku kila mmoja akitaka atoke yeye, hakuna anayetaka kushirikiana na mwenzake, hii hufanya kuishi ndani ya wigo mwembamba uliozungukwa na simba kibao (Very very risk). Huu ubinafsi ndio unaotunyima nafasi za kuendelea na tunaishia palepale. Hivyo point yangu ni kuwa charity starts at home, tuanze na sisi wenyewe kwanza kabla ya kulaumu pia.

Hivyo ushauri wangu kwa sisi vijana (nikiwa na mimi kwani hakuna aliyekamilika).

1. Kujijengenea mazoea ya kujiendeleza, kushirikiana na kutanua wigo.

2. Kila moja wetu kufanya kazi kwa bidii zaidi. Ingawa Tanzania kazi watu hupeana, ilapia wapo wengi waliofika sehemu bila baba wala mama. So jaribu kuwa na malengo na ukipata nafasi onesha UTOFAUTI.

3. Kutokata tamaa, kuna maandiko yanasema kukata tamaa ni ukafiri, hivyo tusikate tamaa, tupigane hadi tone la mwisho na huu ndio siri ya ushindi.
 
Huyu kijana mbona jina lake sio geni masikioni mwangu.
Mbona marekani wanamfatilisa sana?
Kulikoni ndugu zangu.
View attachment 414716
umenichekesha sana mkuu, jina sio geni, kisha unamuulizia??
Jasusi raia wa kimarekani huyo, aliisaliti nchi yake kwa kufichua taarifa za udukuzi wa mawasiliano ya viongozi wakuu Duniani akiwemo ANGEL MMIKEL WA UJERUMANI.
KWA SASA anaishi uhaamishoni URUSI,
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom