NINI TUNAJIFUNZA KUTOKA MCHAKATO WA BREXIT

Mzalendo_Mkweli

JF-Expert Member
Jan 30, 2012
1,988
1,175
Kwanza niaze kwa kusema kwamba mama Theresa may (PM) katika mchakato huu wa Brexit alianza akiwa kama Mpagani (asiyeuamini kabisa) akiwa kundi moja na akina David Cameron. Ghafla, David Cameron alipojiuzulu uwaziri mkuu na Thresa May kukabidhiwa uongozi Mama May akawa BORN AGAIN lakini sio kule kunakotamkwa katika BIBILIA au ule wa George Bush katika Skull and Bones. Katika huu ukigeugeu Mama May alishambuliwa sana na wapinzani wake siku awali ila baadaye walipoona hayumbishwi na mashambulizi yao wakajisemea kimoyomoyo yamkini amekuwa BORN AGAIN kweli. Sasa katika bunge la uingereza kuna changamoto kubwa kwani baadhi ya wabunge wanafanya wanayofanya ili wasije baadaye wakaoneka aidha walizuia/chelewesha mchakato wa Brexit au wanaogopa kuingia katika Historia ya nchi yao kwamba walichangia nchi yao kujitoa katia EU. Sasa kinachoonekana ni kwamba kuna uwezekano kwamba Uingereza inaweza isiwe imepata mpango thabiti wa kujitoa EU (deal) kabla ya tarehe ya mwisho 29/03/2019. Sasa tayari tangazo likiwa limeshatolewa na Rais wa EU Donald Tusk kwamba wote walioshabikiwa Brexit bila kuwa na mpango mkakati wana nafasi muhimu kule jehanamu (Special place in hell), sijui litamfanya Mrs May awe BORN AGAIN tena,
Kwa mtizamo wako unadhani sisi watanzania au nchi zinazoendelea tunajifunza nini kutokana na kinachoendea huko uingezera?


Ahsante
 
Back
Top Bottom