Kama hawana tofauti, kwa nini mnyama mmoja tupoteze muda kumpa majina mawili?
Ni kweli...Nyati ni jina la huyo mnyama na mbogo ni jina la tabia yake ya ukali.
Ndiyo maana neno mbogo pia hutumika kama sifa ya ukali wa baadhi ya watu, utasikia ikisemwa mtu fulani kawa mbogo baada ya kufanyiwa jambo asilolipenda.
Hapo ingefaa ungesema Mbogo ni Nyati aliyejeruhiwa, kwani katika hali yoyote yeye atabaki kuwa Nyati tu.Akiwa kwenye hali/ tabia hii tunamuita "mbogo" badala ya "nyati".
Labda Nyati maji wanaofugwa (water buffalo), lakini sio hao wa porini (Cape buffalo).Je, kuna nyati mpole?
Sio kweli. Nyati ni jina la jumla la huyo mnyama, mbogo ni nyati aliyetengwa kwenye kundi lao hasa hasa huwa ni dume. Hii hutokea pale dume anapozeeka au kuwa na maradhi hivyo kupigwa na madume mengine ili kuongoza kundi. Akisha tolewa kwenye kundi uishi peke yake na huwa ni mkali kwelikweli.Nyati ni jina la huyo mnyama na mbogo ni jina la tabia yake ya ukali.
Ndiyo maana neno mbogo pia hutumika kama sifa ya ukali wa baadhi ya watu, utasikia ikisemwa mtu fulani kawa mbogo baada ya kufanyiwa jambo asilolipenda.
Ndio Nyati!🐃Sio kweli. Nyati ni jina la jumla la huyo mnyama, mbogo ni nyati aliyetengwa kwenye kundi lao hasa hasa huwa ni dume. Hii hutokea pale dume anapozeeka au kuwa na maradhi hivyo kupigwa na madume mengine ili kuongoza kundi. Akisha tolewa kwenye kundi uishi peke yake na huwa ni mkali kwelikweli.
Ndio tabia ya lugha mkuu, kitu kimoja kinaweza kuwa na msamiati zaidi ya mmoja, TEMBO /NDOVU, MOYO / MTIMA, AFYA / SIHA , FAMILIA / AILA...hayo mengine najua vijana wenzangu mtayauliza kama ni Kiswahili , ila ukikaa na mababu unajua mengi.Kama hawana tofauti, kwa nini mnyama mmoja tupoteze muda kumpa majina mawili?
Na mara nyingi ukichunguza vizuri utakuta kuna uwezekano mkubwa kuwa neno mojawapo kati ya hayo limekopwa na mojawapo ndiyo la kiasili.Ndio tabia ya lugha mkuu, kitu kimoja kinaweza kuwa na msamiati zaidi ya mmoja, TEMBO /NDOVU, MOYO / MTIMA, AFYA / SIHA , FAMILIA / AILA...hayo mengine najua vijana wenzangu mtayauliza kama ni Kiswahili , ila ukikaa na mababu unajua mengi.
Muda gani ulipotezwa?Kama hawana tofauti, kwa nini mnyama mmoja tupoteze muda kumpa majina mawili?
Swali gani hili? Kuna lugha ambayo haina maneno yake ya asili? Unamaanisha nini?Kwani Kiswahili kina maneno yake ya asili?
Si wanasema kuwa ni lingua franca.
Nyati ni kiswahili lakini mbogo ni kilugha kilicho changamka na kuwa kama kiswahili.Kama hawana tofauti, kwa nini mnyama mmoja tupoteze muda kumpa majina mawili?
Mbogo ni nyanti na nyati ni mbogo.
Kifupi ni kama Baba, mwana na roho mtakatifu.
Kiswahili ni lingua franca.
Lingua Franca - Lugha iliyojitokeza kuwezesha mawasiliano na muingiliano baina ya watu wa jamii tofauti ambao lugha zao pia zimetofautiana.
Hivyo maneno ya mwanzo ya Kiswahili yamekopwa kutoka lugha mbalimbali za Kibantu, Kiarabu, Kijerumani etc. ili kuwezesha huo muingiliano katika Pwani ya Afrika Mashariki.
Ni nyati 😆Hapo umenichanganya! Sasa kati ya mbogo na nyati ni yupi mbogo...?!