Nini tiba sahihi ya presha?

border

Senior Member
Jun 22, 2017
145
142
Kwa muda sasa nimekuwa nikishuhudia watu wengi wakipatwa na ugonjwa wa Presha na kisukari. Lakini mara wanapogundulika kuwa na ugonjwa upewa dawa za hospital na wengine huanzishiwa kliniki lakini kupona kabisa ni hamna.

Nina rafiki yangu kijana mwenye umri wa miaka 39 kabla ya kupima na kugundulika na Presha alikuwa anaishi vizuri huku akila karibu Kila chakula. Licha ya kuwa alikuwa na matatizo ya mkono wa kushoto kuishiwa nguvu mara Moja Moja.

Sasa wiki iliyopita alipima na kugundulika ana Presha tangu amepima ugonjwa ndio umeongezeka mara dufu mpaka mwili mzima unaishiwa nguvu na anashindwa kufanya kazi kama kawaida na anapopata swala la kunkwaza kidogo ila inakuwa mbaya zaidi.

Dawa alizopewa hospital nimemshauri asianze kuzitumia kwanza. Naomba wanajukwaa mnisaidie dawa sahihi ya huu ugonjwa ni ipi na je mtu mwenye tatizo kama hili anatakiwa kufanya nini?

Natanguliza shukrani.
 
Kana Ni presha ya kipanda atumie unga wa mbegu ya parachichi.inashuka vizuuri Mimi ndio zilizo niponya Mkuu,Kama Ni ya kushuka ajitahidi kula michapati wali sembe itakuwa haishuki hovyo
 
Chukua mbegu ya parachichi isage na blenda ya mkono. Anika ndani au jua la jioni ambalo sio Kali Sana baada ya siku 1 itakuwa kavu atumie kijiko kidogo kimoja kila asubuhi kwa siku 3 TU presha Kwisha ili isirudi Tena awe anafanya zoezi la kutembea japo kwa wiki maramoja nusu SAA TU muda wa asubuhi au jioni
 
Ahsante ubarikiwe
Chukua mbegu ya parachichi isage na blenda ya mkono. Anika ndani au jua la jioni ambalo sio Kali Sana baada ya siku 1 itakuwa kavu atumie kijiko kidogo kimoja kila asubuhi kwa siku 3 TU presha Kwisha ili isirudi Tena awe anafanya zoezi la kutembea japo kwa wiki maramoja nusu SAA TU muda wa asubuhi au jioni
 
Kwa muda sasa nimekuwa nikishuhudia watu wengi wakipatwa na ugonjwa wa Presha na kisukari. Lakini mara wanapogundulika kuwa na ugonjwa upewa dawa za hospital na wengine huanzishiwa kliniki lakini kupona kabisa ni hamna...
We ndo utampoteza.

Mwache atumie dawa la sivyo atapooza au kufariki muda si mrefu
 
Kana Ni presha ya kipanda atumie unga wa mbegu ya parachichi.inashuka vizuuri Mimi ndio zilizo niponya Mkuu,Kama Ni ya kushuka ajitahidi kula michapati wali sembe itakuwa haishuki hovyo

Hapo umetuliza tu itakuja kuibuka ghafla
 
Mzee wangu Lanka hajastaafu alikuwa na presha mpaka Yukawa tuna hofu na Manisha yake,

Alipostaafu ,alikuja kuacha dawa ila ulaji wake ni chuku chuku.

Mpaka Leo halalamiki Ila ana dhurura mchana Kama mchuuzi kwenye heka heka za biashara zake.
 
Back
Top Bottom