Nini suluhisho la kushidwa kuhimili maji kwa mda mrefu!

G M S

JF-Expert Member
Mar 30, 2011
502
53
Wadau naomba kujua ni ipi njia itayosaidia kwa mtu ambaye ukinywa maji ya kutosha kama inavyoshauliwa haipiti muda mrefu unaanza safari za kwenda kukojoa mara kwa mara?
 
mi nalala na kidumu nikijisikia 2 nageukia kidumu wakati wa ucku
 
Wadau naomba kujua ni ipi njia itayosaidia kwa mtu ambaye ukinywa maji ya kutosha kama inavyoshauliwa haipiti muda mrefu unaanza safari za kwenda kukojoa mara kwa mara?
swali zuri sana G spanner, nimeona nilifupishe jibu lako, lakini kupata maelezo zaidi tafadhari tembelea Utangulizi | maajabu ya maji au nitumie email yako katika 0769779533. fanya ifuatavyo:

Kisha kunywa maji, maji yanapaswa kubaki ndani ya mwili masaa 2 mpaka 2 na nusu ili kuupa mwili muda wa kutosha kuyatumia maji hayo vizuri.

Ikiwa inakulazimu kukojoa (peeing) chini ya muda wa masaa 2 tangu unywe maji, utalazimika kuacha kunywa maji matupu, jaribu kunywa juisi (uliyotengeneza mwenyewe) ya chungwa, ya limau au ya zabibu au juisi nyingine yeyote isipokuwa kwa watu wanaosumbuliwa na pumu (asthma) ambao hawatakiwi kunywa juisi ya chungwa.

Wakati huo huo mhimu kukumbuka kuongeza robo tatu gramu za chumvi katika kila nusu lita ya juisi yako.

Ikiwa kunywa juisi hakutasaidia kupunguza kwenda bafuni kila mara, jaribu kunywa maji huku ukila mkate. Unaweza kuongeza krimu ya siagi au jamu kwenye mkate wako (the magic bagel).

Kisha kutumia mkate siku moja au mbili unaweza kupunguza sasa kiasi cha mkate mpaka nusu yake, robo yake na mwisho juisi pekee pamoja na mlo wako.

Utapaswa kurudi taratibu tena kutoka kunywa maji juisi mpaka kunywa maji matupu tena, baada ya siku kadhaa itakupasa kujaribu aunsi 2 za maji matupu nusu saa kabla ya chakula, kesho yake aunsi 4, siku inayofuata itakuwa aunsi 6 kisha 8 na kuendelea mpaka ufikie kiasi chako unachotakiwa.

Ikiwa kunywa maji pamoja na kula mkate au katika juisi hakukusaidii kupunguza kwenda bafuni, Glasi ya maji (ml 250) matupu ikiongezwa na kijiko (kijiko cha chakula) kimoja cha asali au sukari halisi au walau sukari nyeupe kutakutatulia tatizo hili ukiongeza na chumvi 1/8 ya kijiko cha chai , tikisa na kisha kunywa mchanganyiko huo.

Bilashaka umewahi kusikia msemo, “Kwa sehemu kubwa tumetokana na maji”, hii ndiyo sababu zaidi ya asilimia 94 ya damu yetu ni maji, zaidi ya asilimia 85 ya ubongo wetu ni maji, huku zaidi ya asilimia 75 ya sisi ni maji.

unaweza usifanikiwe siku ya kwanza tu utakapojaribu, jaribu mpaka siku 2 kama njia ya kwanza haisaidii jaribu ya pili kwa siku 2 tena, ukishindwa zote nitumie email yako 0769779533. cha msingi usinywe maji mengi kwa wakati mmoja, glasi nane zikigawanywa mara nane kwa siku nzima, glasi 1=250ml. Ipo fomula ya kila mtu kujuwa anahitaji maji kiasi gani kwa siku KUTEGEMEA na uzito wake, nimeshaiandika mara kadhaa hapa, ikiwa uliikosa nijulishe nitakutumia upya.

Muda gani unywe maji:

  • Kitu cha kwanza kufanya mara uamkapo tu, ni kunywa glasi 2 za maji (ml 500) kwakuwa umetumia glasi 2 za maji kwa kulala mpaka asubuhi.
  • Kunywa glasi 1 robo saa au glasi 2 nusu saa kabla ya chakula cha asubuhi, mchana na jioni, kisha hesabu masaa 2 au 2 na nusu kila baada ya chakula cha asubuhi, mchana na jioni bila kunywa wala kula chochote, ndipo unywe glasi 1 ya maji.
  • Kunywa glasi 1 ya maji kila uendapo kulala.
  • Muda wowote uamkapo usiku kwenda bafuni, kunywa nusu glasi ya maji na kipande cha chumvi kisha rudi kulala.
  • Muda wowote unapopatwa na kiu kunywa maji.
Utangulizi | maajabu ya maji
 
Wadau naomba kujua ni ipi njia itayosaidia kwa mtu ambaye ukinywa maji ya kutosha kama inavyoshauliwa haipiti muda mrefu unaanza safari za kwenda kukojoa mara kwa mara?
hii hutokea kwakuwa mwili haujazoea lakini tatizo hili halitakuwepo baada ya muda,pia mwili kwa kawaida unaweza kutumia glasi moja tu ya maji kila nusu saa kwahiyo ukinywa zaidi ya hapo lazima utasikia haja ndogo,pia wataalamu wanasema usinywe maji mengi wakati wa usiku,ukijisahau na ukinywa maji mengi usiku na hutaki kuamka kila mara lamba kijiko kimoja cha asali lakini usifanye hivi kila mara.
 
Back
Top Bottom