Nini sababu ya watoto wa maskini kutoendelea na elimu ya chuo kikuu?

Rack Fikiri

Member
Oct 13, 2012
23
1
Kwa uchunguzi mdogo uliofanyika watoto wa maskini hufanya vizuri katika mitihani ya kidato cha nne na sita.Lakini asilimia kubwa hawaendelei na elimu ya chuo kikuu na hii imetokana na kuwa asilimia kubwa hunyimwa mkopo toka bodi ya mikopo ya elimu ya juu mfano mtoto mmoja wa maskini ameshindwa kwenda chuo kikuu kwa sababu mwaka jana alipata chuo MZUMBE UNIVERSITY lakini hakupata mkopo akaacha mwaka huu amepata SOKOINE UNIVERSITY tena hana mkopo ko mwaka huu chuo kwake ndoto huyu ni mfano tu lakini wapo wengi kibao Swala ambalo huwa sielewi ni je hii bodi ya mikopo ni ya wenye nacho au ya kusaidia maskini? Watoto wa matajiri wakubwa, viongozi,viongozi maarufu wastafu wabunge waliopigwa chini na walomo mjengoni wanapewa mikopo hafu maskini ananyimwa wanamanisha nini au ndo kauli ya mwenye nacho ataongezewa na huyu maskini atanyanganywa na hiki kidogo alichonacho? Hatujui 2naelekea wapi nchi hii watoto wa Maskini
 
Sina uhakika kama thread yako ina ukweli ndani yake. Hivi kweli watoto/waanafunzi waliojaa pale Mlimani kwa mfano wote ni watoto wa mafisadi? Siamini. Ninachoweza kukubaliana na wewe ni kwamba wapo wanafunzi ambao wana sifa lakini wanakosa mikopo!
 
siku hz watoto wa matajiri wamestuka nao wanakata shule sana!! Yale mambo ya mtoto wa masikini anashindia uji na mihogo wanafaulu siku hiz hakuna!! Kufaulu xul ni nyenzo na jitihada vinahitajika....
 
Sio wote wanakosa mikopo ila watoto wa masikini wakosapo mkopo ndoto zao huzikwa 1@1 lkn tajiri akikosa huendelea na elimu kwani kulipa anaweza ila wanataka ku2mia haki za walalahoi kujifaidisha
 
Mimi nadhani tunapoilaumu Bodi ya mikopo tusiangalie watu awliokosa mikopo tu,tuangalie pia wale waliopata kwani wapo watoto wengi maskini ambao kama wasingepata mkopo wangeshindwa kusoma. Bodi wanaendeliea kujitahidi sana hasa ukilinganisha kipindi walipoanza miaka ile ya 1995/6,-2012 wamepiga hatua sana. Jamani tuangalie pia mazuri waliyoboresha, Hongera sana Bodi ya Mikopo.
 
kwa upande wangu nawapongeza sana board kwa kazi wanayoifanya ila bado nawalaumu kitu kimoja, wanaplace mkopo kwa wanafunzi ambao wanauwezo wa juu na mtoto wa maskini anakosa mwisho wa siku elim ya huyu mtoto inaishia hapo, hii inadhihirisha kauli ya aliyenacho anaongezewa na hasyekuwanacho hata kile alichonacho ananyang'anywa.
 
Tatizo kubwa la cc watz tunashindwa kuonesha uwezo wetu wa kipato,ndo maana hawa jamaa wa bodi wanashindwa kutambua kama cc mtoto ni masikini au ni tajiri. Watoto wengi wa masikini wanashindwa kuonesha uwezo wao kiuchumi through documents wanaishia kuongea tu,pia budget inakuwa ndogo ndo maana wanabana kwenye kozi za kipaumbele kama elimu na u doctor,kiukweli jamaa wanajitahidi sana ukilinganisha na nchi zingine sema cc hatujui hayo mafanikio.
 
Back
Top Bottom