Nini sababu ya wabunge wa CCM kusema ndiyo na kupiga makofi kwa jambo litaloleta athari baadae?

Mimi ningependa niwe neutral kwa faida ya mjadala mpana zaidi..... shida kubwa ni wabunge kuingia kwa tiketi za vyama hivyo mnachokubaliana kwenye kamati kuu ndicho wabunge mnaelekezwa kukisimamia bungeni?? Yaani mwenyekiti wa chama akielekeza kwamba swala hili ni ndio au sio wewe kma mbunge huwezi kwenda kubadilisha msimamo bungeni utaitwa msaliti rejea marehem filikunjombe alipotia saini kuhusu kutokuwa na imani na waziri mkuu!!!!

Hivyo tusiwalaumu sana wabunge ila tulaumu mfumo wa kuingia bungeni kwa udhamini wa chama cha siasa naona ndio mwiba mkali sana maana chama kikikutimua ndio unapoteza sifa ya kuwa mbunge...... warioba aliliona hili na kuweka mfumo mzuri ila naona mapendekezo yalipigwa teke

Uchama uchama unaua bunge
 
hili ni swali kila mtu anajiuliza . Je ni uvivu wa kusoma au ni ushabiki tu.

Sent from my TECNO R7 using JamiiForums mobile app



Hilo swali halijapata jibu, ndio maana tumeanza kuhisi kuna roho fulani inayowaandama wabunge wa ccm na makada wake. Ni jambo la kushangaza sana kuona hata watu wazuri wenye hekima wakijiunga au kupewa vyeo kwenye serikali ya ccm ufahamu unaharibika kabisa.
 
Back
Top Bottom