Ndugu zangu,
Ningependa kujua sababu zinazowapelekea wabunge wa CCM kusema ndioooo hata kwa jambo ambalo wanajua wazi kuwa litakuwa na athari kubwa kwa taifa.
Mifano ni mingi sana ya mambo mbalimbali ambayo wabunge wa CCM wamewahi kuyapitisha kwa sauti kubwa za ndiooooo, na kupiga meza pwaa, pwaa, baada ya muda wakajikuta wameanza kulaumu kile walichokiamua na kuhisi hawakuwa miongoni mwa wale walihusika kupitisha jambo hilo. Wakati mwingine wafikia hatua ya kuhisi wakati jambo hilo linapitishwa CCM haikuwa madarakani bali chama kingine.
Kama ni kweli rafiki yangu mmoja amekuwa akiniambia kuwa wabunge wa CCM wakiwa bungeni wanapatwa na hali fulani hivi inayoteka ufahamu wao, wakitoka tu nje hali ya kawaida inawarudia. sijajua kama ni kweli au la.
Walipitisha kwa mbwembwe ununuzi wa ndege ya Rais wakati ule wa Rais Mkapa ndege ambayo ilinunuliwa kwa dhihaka kubwa kwa kuwaambia watanzania kama ni kula majani wananchi bora wale ila ndege ya Rais itanunuliwa tu, matokeo yake tuliletewa mtumba.
Wakapitisha kwa mbwembwe sheria za uchimbaji wa madini, tena kwa hati ya dharula. Wakapitisha sheria za kuchimba geni kwa hati ya dharua pia, Leo wamesahau kuwa ni wao waliopitisha sheria hizo, wameanza kulaumu wale wanaotaka sheria hizo zifanyiwe review kwanza.
ESCROW ndio hiyo ambayo kwa bahati mbaya JK alisema si pesa za Umma wakapiga tena meza pwaa, pwaa, pwaa. Leo wameanza tena kukubaliana na wale waliosimama kidete kutetea mali ya umma. Kaka yangu Kafulila aliitwa Tumbili wakapiga meza pwaa, pwaa,pwaa.
Hivi wabunge wa CCM kuna roho gani inawaingia wakiwa bungeni?
Ningependa kujua sababu zinazowapelekea wabunge wa CCM kusema ndioooo hata kwa jambo ambalo wanajua wazi kuwa litakuwa na athari kubwa kwa taifa.
Mifano ni mingi sana ya mambo mbalimbali ambayo wabunge wa CCM wamewahi kuyapitisha kwa sauti kubwa za ndiooooo, na kupiga meza pwaa, pwaa, baada ya muda wakajikuta wameanza kulaumu kile walichokiamua na kuhisi hawakuwa miongoni mwa wale walihusika kupitisha jambo hilo. Wakati mwingine wafikia hatua ya kuhisi wakati jambo hilo linapitishwa CCM haikuwa madarakani bali chama kingine.
Kama ni kweli rafiki yangu mmoja amekuwa akiniambia kuwa wabunge wa CCM wakiwa bungeni wanapatwa na hali fulani hivi inayoteka ufahamu wao, wakitoka tu nje hali ya kawaida inawarudia. sijajua kama ni kweli au la.
Walipitisha kwa mbwembwe ununuzi wa ndege ya Rais wakati ule wa Rais Mkapa ndege ambayo ilinunuliwa kwa dhihaka kubwa kwa kuwaambia watanzania kama ni kula majani wananchi bora wale ila ndege ya Rais itanunuliwa tu, matokeo yake tuliletewa mtumba.
Wakapitisha kwa mbwembwe sheria za uchimbaji wa madini, tena kwa hati ya dharula. Wakapitisha sheria za kuchimba geni kwa hati ya dharua pia, Leo wamesahau kuwa ni wao waliopitisha sheria hizo, wameanza kulaumu wale wanaotaka sheria hizo zifanyiwe review kwanza.
ESCROW ndio hiyo ambayo kwa bahati mbaya JK alisema si pesa za Umma wakapiga tena meza pwaa, pwaa, pwaa. Leo wameanza tena kukubaliana na wale waliosimama kidete kutetea mali ya umma. Kaka yangu Kafulila aliitwa Tumbili wakapiga meza pwaa, pwaa,pwaa.
Hivi wabunge wa CCM kuna roho gani inawaingia wakiwa bungeni?