Dijovisonjn
JF-Expert Member
- Nov 14, 2011
- 466
- 125
Heri ya Mwaka mpya wadau wa JF!
wadau huwa kuna habari kuwa wakati waziri wa sasa wa Afrika Mashariki ndugu Samuel Sitta anasoma pale UDSM, mwalimu Nyerere aliwahi kuhamrisha achapwe viboko. Napenda kujua Mheshimiwa alikosa nini hadi akachapwa viboko na kwanini yeye tu alichapwa na sio wenzake aliokuwa nao?!
Nashukuru.
wadau huwa kuna habari kuwa wakati waziri wa sasa wa Afrika Mashariki ndugu Samuel Sitta anasoma pale UDSM, mwalimu Nyerere aliwahi kuhamrisha achapwe viboko. Napenda kujua Mheshimiwa alikosa nini hadi akachapwa viboko na kwanini yeye tu alichapwa na sio wenzake aliokuwa nao?!
Nashukuru.
Wakati S Sitta akiwa mwanafunzi wa chuo kikuu UDSM alikumbana na kadhia hiyo ya kuchapwa viboko na Mwl nyerere kama sharti la kurudishwa chuoni. Sitta alituhumiwa kuwa kinara wa mgomo huo.
Ilivyokuwa:
Wanafunzi waligoma na kuandamana kupinga kujiunga na jeshi la kujenga Taifa na kukatwa mishahara yao baada ya kumaliza jeshi.
Baada ya shinikizo hilo la wanafunzi Nyerere alikubali kupunguza mshahara wake wa Tsh 4000 bila kodi na kuagiza pia mishahara ya mawaziri ipunguzwe kwa asilimia 2. Miezi miwili baadae akatangaza azimio la Arusha kuyapa nguvu malalamiko ya wanafunzi hao.
Sitta na Mwabulambo (sasa ni marehemu) na wengine kadhaa waliojitoa muhanga kutetea kile walichokiita haki zao, walimshutumu Mwl Nyerere kwa maneno makali wakidai " Ni heri wakati wa ukoloni kuliko utawala wa Mwalimu.
Mwalimu Nyerere alikasirika na kuwafukuza wanafunzi wote 400 kwa kile alichokiita " kwenda kufunzwa adabu majumbani mwao".
Hasira zilipoisha mwalimu aliamua kuwarudisha wanafunzi 392 tu huku sitta na wenzie 7 wakiendelea kubaki nyumbani.
Mwalimu alipobembelezwa sana alikubali kwa sharti la kuwatandika viboko watukutu wawili (Sitta na Mwabulambo) yeye mwenyewe.
Hii ndiyo ilikuwa pona ya Sitta ambaye alirejea UDSM na kuendelea na masomo kwa miaka kadhaa hadi alipohitimu mwaka 1971.
Chanzo: Mwananchi, Juni 4, 2015.