Nini sababu ya miradi mikubwa ya maendeleo Tanzania kuchelewa au kukwama? Je, ni hujuma za majirani?

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,226
26,048
Amani iwe nanyi wadau!

Leo naomba niandike mada ngumu kwa wengi Ila nyepesi kwa wachache wenye akili na jicho la tatu!!

Mada hii imetokana na Jarida la African Report kuandika Makala inayoelezea kwa Jinsi gani Rais Samia anaweza pata ugumu katika kushawishi Kujengwa kwa Mradi wa Bandari ya Bagamoyo baada ya majadiliano ya kwanza yalioanza mwaka 2012/2013 kukwama mwaka 2019 hadi pale Rais Magufuli alivyoamua kuachana na hayo majadiliano (Kuachana na Mradi wa Bandari ya Bagamoyo)

Kwenye Jarida hili wameelezea mambo machache yanayoweza kufanya China asiwe na interest tena na Bandari ya Bagamoyo ikiwemo suala la China kuanza kujenga Bandari ya Djibout, Uwekezaji Mkubwa kwenye Bandari ya Lamu ambao umeshaanza kutake effect Kama vitu vitakavyoweza kuwafanya wachina wasiwe na interest tena kwenye ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo jambo ambalo Kwa upande mwingine inamaanisha kuwa mradi utakuwa umefeli.

Makala hii imenifanya niwaze sana juu ya miradi mingi iliyochelewa kufanyika kwetu na ikafanyika kwenye nchi jirani na wakapata faida kiuchumi na kwenye ajira. Niligundua sio mradi huu tu, kuna mradi wa Kiwanda cha kuchakata Gesi ambacho nacho kilitakiwa mpaka sasa kiwe kimeshaanza kujengwa au kinakaribia kumalizika, Kuna mradi wa Barabara ya Maloli, kuna mradi wa treni ya umeme katikati ya jiji la Dar es Salaam na miradi mingine mingi ambayo ni kama ilicheleweshwa kwa siasa ama propaganda fulani au imekuja kuanza baadae baada ya miradi kama iyo kufanyika nchi nyingine hasa za majirani.

Leo hii Pia Tanzania tukiwa tunaanza mchakato wa kujenga kiwanda cha kuchakata gesi, kule juu Egypt( Misri) wanakamilisha kiwanda chao Kwa ajiri ya soko la Ulaya na nchi nyingine za Africa. Hili limetangazwa pia kwenye jarida la African Report!

Makala hii imenifanya pia niwaze Kama Je Tanzania tungekuwa wa kwanza kujenga Bandari kubwa ya kisasa kwa ukanda wetu huu kuzidi Djibouti na Kenya tungekuwa wapi kiuchumi leo hii? Soko la kusafirisha bidhaa si lingekuwa kwetu?? Ajira si zingekywa kwetu, mapato na kodi makubwa si yangekuwa kwetu?

Makala hii imenifanya pia niulize Kama na sie kiwanda chetu cha kuchakata Gesi kingekuwa kinaenda kuanza kazi kama cha Egypt na kingetangulia kile cha Msumbuji tungekuwa wapi leo hii kimaendeleo? Au uwekezaji kwenye utafiti wa Gesi ungeendelea je Leo tungekuwa wapi?

Maswali haya yamenifanya niwaze kuwa Kuna hujuma kubwa imepenyezwa na majirani zetu kwenye nchi yetu hasa kwenye siasa na kwenye ngazi ya maamuzi ambayo kazi yake kubwa ni ku sabotage mipango mizuri yetu ya maendeleo ili either ichelewe au ikwame na wenzetu wawe mbele zaidi yetu zaidi kimaendeleo.

Hadi Leo nashindwa kuelewa ni kwa nini majadiliano yalioanza mwaka 2012/13 ya ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo yalikwama hadi Kenya na Djibouti wameanza ujenzi wa mega project zao za Bandari.

Hadi Leo nashindwa kuelewa ni kwa jinsi gani uwekezaji wa gesi uliotakiwa uwe umefikia hatua Nzuri na kuanza kuleta matunda ulikwama hadi msumbiji na sasa Misri wamekamilisha miradi yao ya LNG na kuanza kuteka masoko.

Je, Tanzania ianze kujisafisha na Majasusi wanaohujumu maendeleo yake wanaotumia Siasa na Ngazi za Juu za Maamuzi kuhujumu maendeleo yake?

Naomba mnisaidie majibu wanabodi

3C55F48F-26D5-46A1-AD7A-80D4A5AFC391.jpeg
 
Kama mnayataka yote hayo muwafurahishe waChina na kuongeza udugu basi wapeni sehemu waweke base yao ya kijeshi. Mbona Tanzania itakuwa China ya Afrika. Hilo tu na maeneo mengi tunayo tena makubwa mikakati hawa jamaa tuwape eneo wafungue military base. Hivi kutokea tanga hadi Ntwara tunakosa sehemu y akuwapa eneo? Na kwa hili mkichelewesha basi mjue kun anchi italivalia njuga.
 
Kama mnayataka yote hayo muwafurahishe waChina na kuongeza udugu basi wapeni sehemu waweke base yao ya kijeshi ,Mbona Tanzania itakuwa China ya Afrika ,hilo tu na maeneo mengi tunayo tena makubwa mikakati hawa jamaa tuwape eneo wafungue military base .Hivi kutokea tanga hadi Ntwara tunakosa sehemu y akuwapa eneo ? Na kwa hili mkichelewesha basi mjue kun anchi italivalia njuga.
Umeelewa mada? Au na wewe ndo mmoja wapo ya mapandikizi ya nchi jirani mliopewa kazi ya kuendesha propaganda za kisiasa ili kukwamisha mambo yetu ya kimaendeleo Tanzania?
 
Kama mnayataka yote hayo muwafurahishe waChina na kuongeza udugu basi wapeni sehemu waweke base yao ya kijeshi ,Mbona Tanzania itakuwa China ya Afrika ,hilo tu na maeneo mengi tunayo tena makubwa mikakati hawa jamaa tuwape eneo wafungue military base .Hivi kutokea tanga hadi Ntwara tunakosa sehemu y akuwapa eneo ? Na kwa hili mkichelewesha basi mjue kun anchi italivalia njuga.

Huko kwenye nchi nyingine walizofanya wachina, wamepewa base za kijeshi?
 
Umeelewa mada?? Au na wewe ndo mmoja wapo ya mapandikizi ya nchi jirani mliopewa kazi ya kuendesha propaganda za kisiasa ili kukwamisha mambo yetu ya kimaendeleo Tanzania?

Mkuu una hoja za msingi, ila sitegemei tena muwekazaji serious kuja kuwekeza hapa nchini. Kwenye nchi ambayo sheria zinatekelezwa kwa utashi wa rais aliye madarakani, sioni muwekazaji wa maana katika mazingira hayo.
 
Mkuu una hoja za msingi, ila sitegemei tena muwekazaji serious kuja kuwekeza hapa nchini. Kwenye nchi ambayo sheria zinatekelezwa kwa utashi wa rais aliye madarakani, sioni muwekazaji wa maana katika mazingira hayo.
Sidhani kama shida ni utashi wa Rais. Kuna Tatizo kubwa zaidi ya hapo!
 
Mada inayoishi!

Kwa nguvu zinazotumika kupinga Bandari Ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo ni hakika kuna mapandikizi wengi wanaotumika katika kuhakikisha Tanzania haipigi hatua katika maendeleo!
 
Amani iwe nanyi wadau!

Leo naomba niandike mada ngumu kwa wengi Ila nyepesi kwa wachache wenye akili na jicho la tatu!!

Mada hii imetokana na Jarida la African Report kuandika Makala inayoelezea kwa Jinsi gani Rais Samia anaweza pata ugumu katika kushawishi Kujengwa kwa Mradi wa Bandari ya Bagamoyo baada ya majadiliano ya kwanza yalioanza mwaka 2012/2013 kukwama mwaka 2019 hadi pale Rais Magufuli alivyoamua kuachana na hayo majadiliano (Kuachana na Mradi wa Bandari ya Bagamoyo)

Kwenye Jarida hili wameelezea mambo machache yanayoweza kufanya China asiwe na interest tena na Bandari ya Bagamoyo ikiwemo suala la China kuanza kujenga Bandari ya Djibout, Uwekezaji Mkubwa kwenye Bandari ya Lamu ambao umeshaanza kutake effect Kama vitu vitakavyoweza kuwafanya wachina wasiwe na interest tena kwenye ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo jambo ambalo Kwa upande mwingine inamaanisha kuwa mradi utakuwa umefeli.

Makala hii imenifanya niwaze sana juu ya miradi mingi iliyochelewa kufanyika kwetu na ikafanyika kwenye nchi jirani na wakapata faida kiuchumi na kwenye ajira. Niligundua sio mradi huu tu, kuna mradi wa Kiwanda cha kuchakata Gesi ambacho nacho kilitakiwa mpaka sasa kiwe kimeshaanza kujengwa au kinakaribia kumalizika, Kuna mradi wa Barabara ya Maloli, kuna mradi wa treni ya umeme katikati ya jiji la Dar es Salaam na miradi mingine mingi ambayo ni kama ilicheleweshwa kwa siasa ama propaganda fulani au imekuja kuanza baadae baada ya miradi kama iyo kufanyika nchi nyingine hasa za majirani.

Leo hii Pia Tanzania tukiwa tunaanza mchakato wa kujenga kiwanda cha kuchakata gesi, kule juu Egypt( Misri) wanakamilisha kiwanda chao Kwa ajiri ya soko la Ulaya na nchi nyingine za Africa. Hili limetangazwa pia kwenye jarida la African Report!

Makala hii imenifanya pia niwaze Kama Je Tanzania tungekuwa wa kwanza kujenga Bandari kubwa ya kisasa kwa ukanda wetu huu kuzidi Djibouti na Kenya tungekuwa wapi kiuchumi leo hii? Soko la kusafirisha bidhaa si lingekuwa kwetu?? Ajira si zingekywa kwetu, mapato na kodi makubwa si yangekuwa kwetu?

Makala hii imenifanya pia niulize Kama na sie kiwanda chetu cha kuchakata Gesi kingekuwa kinaenda kuanza kazi kama cha Egypt na kingetangulia kile cha Msumbuji tungekuwa wapi leo hii kimaendeleo? Au uwekezaji kwenye utafiti wa Gesi ungeendelea je Leo tungekuwa wapi?

Maswali haya yamenifanya niwaze kuwa Kuna hujuma kubwa imepenyezwa na majirani zetu kwenye nchi yetu hasa kwenye siasa na kwenye ngazi ya maamuzi ambayo kazi yake kubwa ni ku sabotage mipango mizuri yetu ya maendeleo ili either ichelewe au ikwame na wenzetu wawe mbele zaidi yetu zaidi kimaendeleo.

Hadi Leo nashindwa kuelewa ni kwa nini majadiliano yalioanza mwaka 2012/13 ya ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo yalikwama hadi Kenya na Djibouti wameanza ujenzi wa mega project zao za Bandari.

Hadi Leo nashindwa kuelewa ni kwa jinsi gani uwekezaji wa gesi uliotakiwa uwe umefikia hatua Nzuri na kuanza kuleta matunda ulikwama hadi msumbiji na sasa Misri wamekamilisha miradi yao ya LNG na kuanza kuteka masoko.

Je, Tanzania ianze kujisafisha na Majasusi wanaohujumu maendeleo yake wanaotumia Siasa na Ngazi za Juu za Maamuzi kuhujumu maendeleo yake?

Naomba mnisaidie majibu wanabodi

Mleta mada usisahau miradi yote hiyo tajwa inahitaji pesa, na hata kama tukiwaruhusu wachina kujenga miradi hiyo fahamu kwamba tunaingia katika madeni makubwa ambayo bila kuwa makini yanaweza kuibuka yale yaliyo mkuta Uganda na uwanja wa entebe.

Inabidi utambue kwamba china this guys are smart na hawakurupuki katika decisions zao wanaangalia potential ambayo itakua na benifit maradufu zaidi ya itakavyo tufaidisha sisi na hata ivo wanamasharti magumu yatakayo tulazimu kufata matakwa yao mpaka tutakapo walipa gharama za ujenzi wa hiyo miradi unayo iyona kama ni fursa.

lastly usidhani kama viongozi hawajaliona hili la ajira na makusanyo ya mapato katika completions za miradi hiyo ila they need to come up smart ideas ili masharti ya wawekezaji isituumizi sisi wananchi.
 
Mleta mada usisahau miradi yote hiyo tajwa inahitaji pesa, na hata kama tukiwaruhusu wachina kujenga miradi hiyo fahamu kwamba tunaingia katika madeni makubwa ambayo bila kuwa makini yanaweza kuibuka yale yaliyo mkuta Uganda na uwanja wa entebe.

Inabidi utambue kwamba china this guys are smart na hawakurupuki katika decisions zao wanaangalia potential ambayo itakua na benifit maradufu zaidi ya itakavyo tufaidisha sisi na hata ivo wanamasharti magumu yatakayo tulazimu kufata matakwa yao mpaka tutakapo walipa gharama za ujenzi wa hiyo miradi unayo iyona kama ni fursa.

lastly usidhani kama viongozi hawajaliona hili la ajira na makusanyo ya mapato katika completions za miradi hiyo ila they need to come up smart ideas ili masharti ya wawekezaji isituumizi sisi wananchi.
Kwa nini kuna watu hawataki hata kusikia juu ya mradi wa Bandari ya Bagamoyo? Hata Kwa masharti mazuri inayotaka serikali kuingia?

Je ni ma pandikizi wasiotaka maendeleo ya kweli ya Tanzania?
 
Mada inayoishi!

Kwa nguvu zinazotumika kupinga Bandari Ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo ni hakika kuna mapandikizi wengi wanaotumika katika kuhakikisha Tanzania haipigi hatua katika maendeleo!
Una akili ya maiti kweli, mnabuni miradi ya gharama kubwa zinazowashinda kuitekeleza mpaka mpate mikopo au misaada, halafu lawama zako unawapelekea wanaopinga uwepo wa hiyo miradi!.

Mfano LNG itself mnataka $30bil, mkiulizwa mtazitoa wapi mnaita watu wana chuki binafsi, nyie wapuuzi lazima mpingwe hili taifa sio la "werevu" wa sampuli yenu.
 
Kuna watu ukiwauliza hata kama wameona huo mkataba hawatasema, cha msingi uwekwe wazi kama kuna win win situation twendw nao.
 
Una akili ya maiti kweli, mnabuni miradi ya gharama kubwa zinazowashinda kuitekeleza mpaka mpate mikopo au misaada, halafu lawama zako unawapelekea wanaopinga uwepo wa hiyo miradi!.

Mfano LNG itself mnataka $30bil, mkiulizwa mtazitoa wapi mnaita watu wana chuki binafsi, nyie wapuuzi lazima mpingwe hili taifa sio la "werevu" wa sampuli yenu.
Kwani ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo ni uwekezaji wa sekta binafsi au inatakiwa kujengwa kwa fedha za Serikali? Nani alikwambia kuwa Tanzania ilipanga kujenga Bandari ile kwa fedha zake?
 
Kuna watu ukiwauliza hata kama wameona huo mkataba hawatasema, cha msingi uwekwe wazi kama kuna win win situation twendw nao.
Kwa sasa ninaamini kuwa jibu la Serikali ya Awamu ya sita kuwa hapajawai kuwa na mkataba ndo jibu sahihi!

Maana wanaoipinga hii Bandari wote wanaishia kusema maneno Matupu tu kuwaingiza chaka ukiwauliza huo mkataba Uko wapi wanaishia kubwabwaja tu!
 
Back
Top Bottom