Nini priority za sasa kama nchi?

Majighu2015

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
2,924
3,904
1.Sekta ya afya hali mbaya--Madawa hakuna hospitalini. Kuna vituo hata panadol havina.
2. Sekta ya viwanda naona bado tuko nyuma sana.
3.Sekta ya elimu bado tunasuasua. Ile sera ya elimu bure naona ina hali mbaya.
4.Uchumi bado unadorora.
5. Ukusanyaji kodi tumerudi kulekule alipotuacha Rais Kikwete 900 bil.
6.Sekta ya kilimo na ufugaji bado hamna mipango inayoeleweka.
7.Michezo bado tuko nyuma sana..Huwa najiuliza kwa nini kila siku serikali ina-finance timu ya taifa ya mpira wa miguu na hamna mafanikio.
8.Uhuru wa kujieleza umeminywa.
......Na mengineyo

Sasa najiuliza ni kwamba serikali inajipanga au ni nini shida. Kama nchi ni nini priority yetu? Wapi tumekwama na tufanyaje kurekebisha? Je tutafika uchumi wa kati kwa style ya sasa?
 
1.Sekta ya afya hali mbaya--Madawa hakuna hospitalini. Kuna vituo hata panadol havina.
2. Sekta ya viwanda naona bado tuko nyuma sana.
3.Sekta ya elimu bado tunasuasua. Ile sera ya elimu bure naona ina hali mbaya.
4.Uchumi bado unadorora.
5. Ukusanyaji kodi tumerudi kulekule alipotuacha Rais Kikwete 900 bil.
6.Sekta ya kilimo na ufugaji bado hamna mipango inayoeleweka.
7.Michezo bado tuko nyuma sana..Huwa najiuliza kwa nini kila siku serikali ina-finance timu ya taifa ya mpira wa miguu na hamna mafanikio.
8.Uhuru wa kujieleza umeminywa.
......Na mengineyo

Sasa najiuliza ni kwamba serikali inajipanga au ni nini shida. Kama nchi ni nini priority yetu? Wapi tumekwama na tufanyaje kurekebisha? Je tutafika uchumi wa kati kwa style ya sasa?
Priority ni MIUNDO MBINU!
 
Mwenye kuweza kujibu hili swali ni mkemia alie bobea. Maana yeye ndie dereva wa gari hili, na niyeye pekee ndie anae tambua wapi anatupeleka.
 
Kuhakikisha Faru John anapatikana akiwa Hai

Pia kuhakikisha Lema anafudishwa adabu akiwa magereza

Mwisho ni Ben saa nane apotee machoni petu mpaka tumsahau kama Balali
 
nchi hii kwa sasa kama dharura inahitaji rehema na utakaso wa mwenyezi mungu
.... no more .... no less
 
JPM ana dream dege la DREAMLINER huku majaliwa akilala akiamka FARU JOHN anamuijia kichwani kwa hiyo nafikiri hizo ndo priority zao,
JPM nae siku hizi clouds imekuwa kama mtu aliepata demu mpya.
 
Ila tuache mzaha,

Vipaumbele vyetu kama Taifa kwa sasa ni vipi? And how far have we moved to attain them?
 
Kutumbua majipu.

Mambo mengine ya msingi ni baadaye huko tukikaribia uchaguzi. Pia tutafyatua fulana, kanga, na kofia za yanga za kutosha.

-Kaveli-
 
Back
Top Bottom