GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,542
- 108,852
Kuna dada mmoja nahisi sijui kaniroga au vipi. Kwani kwa mwezi mmoja sasa katika mapenzi yetu keshanifanyia vitimbi 90 vya kila aina, lakini kila nikiwaza tu kumfukuza kesho yake basi nashangaa ghafla upendo unazidi maradufu kwake.
Na kuna siku nakumbuka nilimfukuza na kwenda kwao Kyaka Nkude kijijini na haikuzidi hata saa tano nikamfuata na kumrudisha hapa kwangu na juzi tu nimemfumania akifanya mapenzi" Live " na rafiki yangu wa karibu
Lakini nikashangaa badala ya kukasirika na kumpiga ndiyo kwanza nikajikuta namwambia amalize kufanya mapaenzi na huyo rafiki yangu kisha anipitie turudi wote nyumbani. Sasa hiyo tisa, kumi ni hii ya leo na sasa hivi nimerudi kutoka kazini nimekuta kafunga mlango wa chumbani anafanya mapenzi tena na mtu mwingine na kanitumia meseji katika simu kuwa nisubiri kwanza amalizane na jamaa.
Kisha ndipo atanifungulia mlango na cha kushangaza baada ya kuambiwa hivyo mimi ndiyo kwanza nipo zangu sebuleni nacheza video game na mwanangu Gentamycine Jr. Na kuna wazo linanijia kuwa akishamaliza tu na huyo mshikaji basi nimkodie jamaa teksi impeleke kwake kupumzika halafu na mimi baadae nitoke na mke wangu kwenda kumnunulia zawadi.
Jamani nifanyaje kwani nafanyiwa vitimbi vya kila aina lakini najikuta tu nashindwa kumwacha au kumfukuza. Je nina tatizo gani labda?
Naombeni mnipe basi mbinu za kunisaidia mimi niweze kumwacha na nitawashukuruni nyote.
Na kuna siku nakumbuka nilimfukuza na kwenda kwao Kyaka Nkude kijijini na haikuzidi hata saa tano nikamfuata na kumrudisha hapa kwangu na juzi tu nimemfumania akifanya mapenzi" Live " na rafiki yangu wa karibu
Lakini nikashangaa badala ya kukasirika na kumpiga ndiyo kwanza nikajikuta namwambia amalize kufanya mapaenzi na huyo rafiki yangu kisha anipitie turudi wote nyumbani. Sasa hiyo tisa, kumi ni hii ya leo na sasa hivi nimerudi kutoka kazini nimekuta kafunga mlango wa chumbani anafanya mapenzi tena na mtu mwingine na kanitumia meseji katika simu kuwa nisubiri kwanza amalizane na jamaa.
Kisha ndipo atanifungulia mlango na cha kushangaza baada ya kuambiwa hivyo mimi ndiyo kwanza nipo zangu sebuleni nacheza video game na mwanangu Gentamycine Jr. Na kuna wazo linanijia kuwa akishamaliza tu na huyo mshikaji basi nimkodie jamaa teksi impeleke kwake kupumzika halafu na mimi baadae nitoke na mke wangu kwenda kumnunulia zawadi.
Jamani nifanyaje kwani nafanyiwa vitimbi vya kila aina lakini najikuta tu nashindwa kumwacha au kumfukuza. Je nina tatizo gani labda?
Naombeni mnipe basi mbinu za kunisaidia mimi niweze kumwacha na nitawashukuruni nyote.