( Nimeunasa mjadala unaopamba moto kule kwanzajamii.com
Mbashiri said:
Mchomeko;
Ni nini hasa nia ya Butiku na wenzake?
Na Abdul Mbashiri wa Mbashiri
KWA watu walioshikilia madaraka, tena kwa miaka mingi, wakayatumia kama walivyopenda, wakitamba na hata kuonea watu lakini wakayapoteza madaraka hayo ghafla na wasijue jinsi ya kuyapata tena, siyo jambo la ajabu wala la kushangaza kusikia na kuona watu hao wakitapatapa kwa kauli zisizo za msingi dhidi ya utawala ulioko madarakani sasa.
Wakubwa hawa wanadai kuwa nchi inakwenda ovyo. Kwamba nchi imejaa rushwa (wenyewe wamepata neno jipya la ufisadi). Kwamba nchi imegawanyika vipande vipande. Kwamba inafaa kurudisha Azimio la Arusha. Kwamba nchi inaharibiwa na Mtandao. Kwamba Rais Jakaya Kikwete amezungukwa na majizi.
Hakuna namna bora zaidi ya kuzielezea kauli hizi zinazotolewa na watu ambao wamepata kuwa viongozi, tena wakubwa Serikalini, ila kusema kuwa kauli hizi ni kauli za hatari kwa uhai na usalama wa nchi, na kwa kweli ni ushahidi halisi za watu wanaotahayari baada ya kupoteza madaraka hata kama wanaendelea kuyasaka kwa udi na uvumba kwa njia nyingine.
Pamoja na uhatari wake, hizo ndizo baadhi ya kauli zilizotawala Mjadala wa Kongamano la Miaka 10 ya Kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, lililofanyika majuzi mjini Dar Es Salaam kwa kuandaliwa na Mfuko wa Mwalimu Nyerere (Nyerere Foundation).
Hakuna shaka, hata kidogo, kuwa kongamano hili lilikuwa zuri na muhimu kumuenzi Baba wa Taifa, kiongozi ambaye pamoja na kwamba utawala wake haukuwa kamilifu hasa katika maeneo kama ya uchumi na utawala bora, bado alikuwa na anabakia kuwa nguzo kuu la Taifa la Tanzania, na nyota iliyongara na inaendelea kungara katika Bara la Afrika.
Mwalimu Nyerere anabakia kiongozi ambaye amelijenga Taifa Huru la Tanzania, atabakia kiongozi mfano wa uadilifu, hasa wa mali. Waliomharibia wakati wa utawala wake na pengine wanaoendelea kuharibu jina lake kwa kulitumia vibaya jina hilo ni hawa akina Joseph Butiku, Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Mwalimu Nyerere - Nyerere Foundation na wenzake ndani na nje ya taasisi hiyo.
Hakuna njia mbaya zaidi ya kumuezi Mwalimu Nyerere kama wanavyofanya akina Butiku kwa kutumia jina la Mwalimu kama kichaka cha kuficha tamaa na laghai zao kwa wananchi na kuendeleza maslahi, mahitaji na matakwa yao binafsi.
Kuna mambo kadhaa yanayostahili kuwekwa wazi mapema ili kufuatilia vizuri makala hii na zile zitakazofuatia. La kwanza ni kujua shahaba kuu ya kuanzishwa kwa Nyerere Foundation. La pili kujiuliza ni kwa nini mashambulizi haya yanazushwa sasa hivi. La tatu ni kujiuliza mashambulizi hayo yanamlenga nani hasa - Serikali, nchi ama kiongozi wa vyote viwili na mwisho ni kujiuliza nini hasa nia ya akina Butiku na wenzake. Nini kinawasukuma kuwa katika mstari wa mbele kabisa kuushambulia uongozi wa sasa wa Tanzania.
Tuanze na la kwanza. Nyerere Foundation inazo shabaha kadhaa, lakini kubwa kuliko zote ni kwamba huu ni Mfuko ulioanzishwa kwa nia kuu ya kuendeleza yale makuu ambayo aliyaanzisha, akayasimamia na kuyaenzi Mwalimu wakati wa uhai wake wote, ndani ama nje ya madaraka ya uongozi.
Na moja kubwa katika hayo ni nia ya dhati, iliyoungwa mkono na vitendo vya dhahiri kabisa ni jitihada zake kubwa kujenga Taifa la Tanzania, kuleta Umoja wa Tanzania, na kuhakikisha kuwa nchi hii inaendelea kuwa na utulivu na amani katika eneo la dunia ambako mambo hayo mawili ni tunu kubwa.
Ni dhahiri kuwa kauli za akina Butiku zinavunja kabisa msingi huu mkubwa wa Mwalimu, na hivyo nia ya watoa kauli hizo, haiwezi kuwa wanalenga kumuenzi Mwalimu, bali ni kutumia jina lake vibaya tu, na kama kichocheo cha kuendeleza chuki na ajenda zao binafsi.
Mashambulizi haya ya wakubwa hawa yasiyoisha dhidi ya uongozi wa sasa hayalengi kujenga taifa lenye Umoja, bali yanajaribu kubomoa Umoja wa Taifa letu kwa kuwarubuni wananchi waamini kuwa uongozi wa sasa siyo makini na haustahili kuwa madarakani. Ni aina ya hatari ambayo tumeishuhudia ikiziingiza nchi nyingi za Afrika katika zahama kubwa.
Kauli hizi za uchochezi za akina Butiku, ikitokea zikasababisha vurugu, uvunjwaji wa amani na upotevu wa maisha na mali katika nchi, ni dhahiri kuwa katika dunia ya sasa, Butiku na wenzake wanahusika na kuwajibishwa moja kwa moja, siyo tu na vyombo vya Tanzania tu, bali hata vile vya kimataifa.
Mfano halisi ni jirani zetu wa Kenya ambako viongozi waliohusika na machafuko, mauaji na upoteza wa maisha na mali baada ya Uchaguzi Mkuu wa Desemba 2007, sasa wanahaha kujinasua katika ndoani ya Mahakama ya Kimataifa ya Uharifu (ICC) na mwendeshaji wa mashitaka ya Mahakama hiyo, Bwana Luis Moreno Ocampo.
Akina Butiku wanasahau hata sifa kuu za uongozi. Moja ya sifa kubwa ya kiongozi mzuri ni kujua nini la kusema na wakati gani. Kiongozi hawezi kuwa mropokaji, tena hadharani, juu ya mambo ambayo yangeweze kusemwa kwa busara zaidi kwa kuyaelekeza kwa wanaohusika moja kwa moja bila kutumia jukwaa la kisiasa. Na basi ni vyema mtu kuropoka ukijiaminisha kuwa mtu safi ambaye hana madoa makubwa na ya dhahiri kabisa katika uongozi.
Hoja ya pili na ya tatu hapo juu zinaweza kujibiwa kwa pamoja na kwa maelezo mafupi. Mashambulizi haya yanazuka sasa kwa sababu wenye kuyaendesha wanahisi kuwa baada ya kuwa wamejaribu na kushindwa huko nyuma, sasa ndiyo wakati mwafaka wakati nchi inajiandaa kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwakani.
Na kwa kweli hii ndiyo nafsi yao ya mwisho kujaribu kuwashawishi wananchi kwa propaganda zao dhaifu na zisizo kweli. Wanaamini kuwa propaganda hizo zikifanikiwa wanaweza kujaribu tena kumpamba na kumwingiza mgombea wao katika kinyanganyiro cha uchaguzi mkuu wa mwakani.
Tatu ni kwamba mashambulizi ya sasa, hata kama waendeshaji mashambulizi hayo wanajificha vipi, yanamlenga moja kwa moja kiongozi wa sasa wa Serikali na taifa la Tanzania, yaani Rais Jakaya Mrisho Kikwete. Haya siyo aina ya mashambulizi yanayomlenga mtu mwingine yoyote wa chini ya Rais.
Mwisho ni kwa nini akina Butiku wanamlenga Rais Kikwete? Nini nia ya akiba Butiku na wenzake? Nini kinasukuma wazee hawa kumshambulia kijana ambaye walimlea wenyewe katika uongozi, kwa miaka mingi.
Kubwa la kwanza ni kwamba tokea mwanzo, kundi hili la wazee halikumtaka Jakaya Mrisho Kikwete kuwa Rais wa Tanzania. Na wala halijapata kumkubali ama hata kumsamehe Kiongozi huyo kwa kuweza kuwashinda wakati wa mchakato wa kuwania uongozi mwaka 2005.
Na ndiyo maana zinajegwa hoja zinazodiriki kuhoji hata ni kwa namna gani aliingia madarakani, wakisahau kuwa ni wananchi wenyewe wa Tanzania katika hatua mbali mbali waliomwingiza Rais Kikwete madarakani, tena kwa kumwuunga mkono kwa wingi wa kushangaza sana.
Na siyo tu kwamba aliwashinda kuweza kuingia madarakani. Lakini pia wanahisi kuwa kuwapo kwake madarakani kunafunga milango ya maslahi na matakwa yao kuweza kutumikiwa vizuri na utawala wake. Kwa namna nyingine pia wana hofu kuwa udhaifu wao na uongozi na uchafu wa baadhi yao walipokuwa madarakani unaweza kuanikwa hadharani.
Hivyo, wanatumia janja tu ya jukwaa la kumuenzi Mwalimu Nyerere kujitafutia umaarufu binafsi na kutaka waenziwe wao. Na wako tayari kulifanya hili kwa gharama zote zote ikiwa ni pamoja na kutumia siri za vikao
Ni sababu hiyo ya msingi ambayo siku zote imewasukuma viongozi hao kuushambulia moja kwa moja uongozi wake. Wamekuwa wanashindwa kumshambulia yeye moja kwa moja kwa jina na cheto chake kwa sababu wanaogopa hasira ya wananchi, lakini baada ya mashambulizi ya Kongamano la majuzi ni dhahiri kuwa sasa wanajiandaa kuianza kazi hiyo kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya. Na wala wananchi wasije kushangazwa na hili.
(Makala hii itaendelea)
CHANZO: http://www.kwanzajamii.com
Mbashiri said:
Mchomeko;
Ni nini hasa nia ya Butiku na wenzake?
Na Abdul Mbashiri wa Mbashiri
KWA watu walioshikilia madaraka, tena kwa miaka mingi, wakayatumia kama walivyopenda, wakitamba na hata kuonea watu lakini wakayapoteza madaraka hayo ghafla na wasijue jinsi ya kuyapata tena, siyo jambo la ajabu wala la kushangaza kusikia na kuona watu hao wakitapatapa kwa kauli zisizo za msingi dhidi ya utawala ulioko madarakani sasa.
Wakubwa hawa wanadai kuwa nchi inakwenda ovyo. Kwamba nchi imejaa rushwa (wenyewe wamepata neno jipya la ufisadi). Kwamba nchi imegawanyika vipande vipande. Kwamba inafaa kurudisha Azimio la Arusha. Kwamba nchi inaharibiwa na Mtandao. Kwamba Rais Jakaya Kikwete amezungukwa na majizi.
Hakuna namna bora zaidi ya kuzielezea kauli hizi zinazotolewa na watu ambao wamepata kuwa viongozi, tena wakubwa Serikalini, ila kusema kuwa kauli hizi ni kauli za hatari kwa uhai na usalama wa nchi, na kwa kweli ni ushahidi halisi za watu wanaotahayari baada ya kupoteza madaraka hata kama wanaendelea kuyasaka kwa udi na uvumba kwa njia nyingine.
Pamoja na uhatari wake, hizo ndizo baadhi ya kauli zilizotawala Mjadala wa Kongamano la Miaka 10 ya Kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, lililofanyika majuzi mjini Dar Es Salaam kwa kuandaliwa na Mfuko wa Mwalimu Nyerere (Nyerere Foundation).
Hakuna shaka, hata kidogo, kuwa kongamano hili lilikuwa zuri na muhimu kumuenzi Baba wa Taifa, kiongozi ambaye pamoja na kwamba utawala wake haukuwa kamilifu hasa katika maeneo kama ya uchumi na utawala bora, bado alikuwa na anabakia kuwa nguzo kuu la Taifa la Tanzania, na nyota iliyongara na inaendelea kungara katika Bara la Afrika.
Mwalimu Nyerere anabakia kiongozi ambaye amelijenga Taifa Huru la Tanzania, atabakia kiongozi mfano wa uadilifu, hasa wa mali. Waliomharibia wakati wa utawala wake na pengine wanaoendelea kuharibu jina lake kwa kulitumia vibaya jina hilo ni hawa akina Joseph Butiku, Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Mwalimu Nyerere - Nyerere Foundation na wenzake ndani na nje ya taasisi hiyo.
Hakuna njia mbaya zaidi ya kumuezi Mwalimu Nyerere kama wanavyofanya akina Butiku kwa kutumia jina la Mwalimu kama kichaka cha kuficha tamaa na laghai zao kwa wananchi na kuendeleza maslahi, mahitaji na matakwa yao binafsi.
Kuna mambo kadhaa yanayostahili kuwekwa wazi mapema ili kufuatilia vizuri makala hii na zile zitakazofuatia. La kwanza ni kujua shahaba kuu ya kuanzishwa kwa Nyerere Foundation. La pili kujiuliza ni kwa nini mashambulizi haya yanazushwa sasa hivi. La tatu ni kujiuliza mashambulizi hayo yanamlenga nani hasa - Serikali, nchi ama kiongozi wa vyote viwili na mwisho ni kujiuliza nini hasa nia ya akina Butiku na wenzake. Nini kinawasukuma kuwa katika mstari wa mbele kabisa kuushambulia uongozi wa sasa wa Tanzania.
Tuanze na la kwanza. Nyerere Foundation inazo shabaha kadhaa, lakini kubwa kuliko zote ni kwamba huu ni Mfuko ulioanzishwa kwa nia kuu ya kuendeleza yale makuu ambayo aliyaanzisha, akayasimamia na kuyaenzi Mwalimu wakati wa uhai wake wote, ndani ama nje ya madaraka ya uongozi.
Na moja kubwa katika hayo ni nia ya dhati, iliyoungwa mkono na vitendo vya dhahiri kabisa ni jitihada zake kubwa kujenga Taifa la Tanzania, kuleta Umoja wa Tanzania, na kuhakikisha kuwa nchi hii inaendelea kuwa na utulivu na amani katika eneo la dunia ambako mambo hayo mawili ni tunu kubwa.
Ni dhahiri kuwa kauli za akina Butiku zinavunja kabisa msingi huu mkubwa wa Mwalimu, na hivyo nia ya watoa kauli hizo, haiwezi kuwa wanalenga kumuenzi Mwalimu, bali ni kutumia jina lake vibaya tu, na kama kichocheo cha kuendeleza chuki na ajenda zao binafsi.
Mashambulizi haya ya wakubwa hawa yasiyoisha dhidi ya uongozi wa sasa hayalengi kujenga taifa lenye Umoja, bali yanajaribu kubomoa Umoja wa Taifa letu kwa kuwarubuni wananchi waamini kuwa uongozi wa sasa siyo makini na haustahili kuwa madarakani. Ni aina ya hatari ambayo tumeishuhudia ikiziingiza nchi nyingi za Afrika katika zahama kubwa.
Kauli hizi za uchochezi za akina Butiku, ikitokea zikasababisha vurugu, uvunjwaji wa amani na upotevu wa maisha na mali katika nchi, ni dhahiri kuwa katika dunia ya sasa, Butiku na wenzake wanahusika na kuwajibishwa moja kwa moja, siyo tu na vyombo vya Tanzania tu, bali hata vile vya kimataifa.
Mfano halisi ni jirani zetu wa Kenya ambako viongozi waliohusika na machafuko, mauaji na upoteza wa maisha na mali baada ya Uchaguzi Mkuu wa Desemba 2007, sasa wanahaha kujinasua katika ndoani ya Mahakama ya Kimataifa ya Uharifu (ICC) na mwendeshaji wa mashitaka ya Mahakama hiyo, Bwana Luis Moreno Ocampo.
Akina Butiku wanasahau hata sifa kuu za uongozi. Moja ya sifa kubwa ya kiongozi mzuri ni kujua nini la kusema na wakati gani. Kiongozi hawezi kuwa mropokaji, tena hadharani, juu ya mambo ambayo yangeweze kusemwa kwa busara zaidi kwa kuyaelekeza kwa wanaohusika moja kwa moja bila kutumia jukwaa la kisiasa. Na basi ni vyema mtu kuropoka ukijiaminisha kuwa mtu safi ambaye hana madoa makubwa na ya dhahiri kabisa katika uongozi.
Hoja ya pili na ya tatu hapo juu zinaweza kujibiwa kwa pamoja na kwa maelezo mafupi. Mashambulizi haya yanazuka sasa kwa sababu wenye kuyaendesha wanahisi kuwa baada ya kuwa wamejaribu na kushindwa huko nyuma, sasa ndiyo wakati mwafaka wakati nchi inajiandaa kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwakani.
Na kwa kweli hii ndiyo nafsi yao ya mwisho kujaribu kuwashawishi wananchi kwa propaganda zao dhaifu na zisizo kweli. Wanaamini kuwa propaganda hizo zikifanikiwa wanaweza kujaribu tena kumpamba na kumwingiza mgombea wao katika kinyanganyiro cha uchaguzi mkuu wa mwakani.
Tatu ni kwamba mashambulizi ya sasa, hata kama waendeshaji mashambulizi hayo wanajificha vipi, yanamlenga moja kwa moja kiongozi wa sasa wa Serikali na taifa la Tanzania, yaani Rais Jakaya Mrisho Kikwete. Haya siyo aina ya mashambulizi yanayomlenga mtu mwingine yoyote wa chini ya Rais.
Mwisho ni kwa nini akina Butiku wanamlenga Rais Kikwete? Nini nia ya akiba Butiku na wenzake? Nini kinasukuma wazee hawa kumshambulia kijana ambaye walimlea wenyewe katika uongozi, kwa miaka mingi.
Kubwa la kwanza ni kwamba tokea mwanzo, kundi hili la wazee halikumtaka Jakaya Mrisho Kikwete kuwa Rais wa Tanzania. Na wala halijapata kumkubali ama hata kumsamehe Kiongozi huyo kwa kuweza kuwashinda wakati wa mchakato wa kuwania uongozi mwaka 2005.
Na ndiyo maana zinajegwa hoja zinazodiriki kuhoji hata ni kwa namna gani aliingia madarakani, wakisahau kuwa ni wananchi wenyewe wa Tanzania katika hatua mbali mbali waliomwingiza Rais Kikwete madarakani, tena kwa kumwuunga mkono kwa wingi wa kushangaza sana.
Na siyo tu kwamba aliwashinda kuweza kuingia madarakani. Lakini pia wanahisi kuwa kuwapo kwake madarakani kunafunga milango ya maslahi na matakwa yao kuweza kutumikiwa vizuri na utawala wake. Kwa namna nyingine pia wana hofu kuwa udhaifu wao na uongozi na uchafu wa baadhi yao walipokuwa madarakani unaweza kuanikwa hadharani.
Hivyo, wanatumia janja tu ya jukwaa la kumuenzi Mwalimu Nyerere kujitafutia umaarufu binafsi na kutaka waenziwe wao. Na wako tayari kulifanya hili kwa gharama zote zote ikiwa ni pamoja na kutumia siri za vikao
Ni sababu hiyo ya msingi ambayo siku zote imewasukuma viongozi hao kuushambulia moja kwa moja uongozi wake. Wamekuwa wanashindwa kumshambulia yeye moja kwa moja kwa jina na cheto chake kwa sababu wanaogopa hasira ya wananchi, lakini baada ya mashambulizi ya Kongamano la majuzi ni dhahiri kuwa sasa wanajiandaa kuianza kazi hiyo kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya. Na wala wananchi wasije kushangazwa na hili.
(Makala hii itaendelea)
CHANZO: http://www.kwanzajamii.com