Nini ni tatizo la soko la filamu Tanzania

ubongokid

JF-Expert Member
Apr 30, 2017
2,030
3,907
Filamu ni moja kati ya zana bora sana ya kuelimisha na kuburidisha

Nafahamu kwamba wako waigizaji na watayarishaji wa filamu za kibongo wengi na wengine walishakufaga na walifanya kazi nzuri sana.
Pamoja na ukweli huo lakini bado naona kuna tatizo kubwa katika soko la filamu la Bongo.
Baadhi ya matatizo ninayoyaona ni kama haya

  1. Kukosekana kwa great stories;Filamu nyingi za kibongo zinakuwa na story dhaifu zisizokuwa na msisimko na mbali na hapo zinakuwa hazina uelekeo sahihi
  2. Tatizo la pili ni tatizo la Fedha,Financing..Soko la filamu limevamiwa na PIMPs ambao wanalenga zaidi kutumia sanaa hii katika maswala ya anasa zaidi na kupata mabinti wazuri
  3. Tatizo la tatu ni udhaifu wa Basata.Basata imeshindwa kabisa kuweka uwanja mzuri unaowezesha soko la filamu kukua na kuwezesha ulinzi wa kazi za sanaa.Wanatumia Muda mwingi kufungia kazi za sanaa kuliko kufuatilia na kuhamasisha wasanii wafanye kazi bora na zenye viwango
  4. PAmoja na wingi wa Media hapa Tanzania bado hakuna Media ambayo imeweza kuwekeza katika soko la Filamu.Bado ni ivgumu kwa Filamu kupata Airtime kwenye TV za kibongo
  5. Elimu nayo ni tatizo kwani wengi wanaojishughulisha na sanaa hawana hata elimu ya kuwaida ya kuweza kutambua masuala ya kawaida kabisa kama vile seting ya ujambazi ambapo kwa kawaida jambazi havui viatu akivamia.
Tuliadili soko la filamu usiku huu tuone wadau wana maoni na mtazamo gani
 
Tatizo la kwanza wanaangalia uzuri wa mtu kuliko kipaji cha mtu, mwanamke akiwa na sura nzuri au hips na matako makubwa tayari ashakuwa msanii, mwanaume ukiwa shombeshombe HB full kung'ata lips tayari ushakuwa msanii.

Matokeo yake hata kazi zao zinakosa ubunifu sababu hazikuchezwa na wasanii wenye vipaji na ndio maana wadangaji kibao wa kike na wakiume wapo bongo movie mpaka sometimes huwaga najiulizaga labda Kuna rushwa za ngono ndio maana wanachagua wenye mwonekano mzuri.

Ila kwa TZ naweza kusema Madebe anajitahidi sana kutengeneza filamu nzuri, hata wasanii wake anaocheza nao wengi wana vipaji, ila hao wengine wauza sura hamna kitu . Sometimes najiuliza Lupita angezaliwa bongo sizani kama angekuwa actress.

La pili wawe na mgawanyo wa kazi kwa watu tofauti, sio mtu mmoja anakuwa na nafasi tatu script writer yeye, actor yy, director yy, ila kama ana uwezo na uzoefu wa kumudu nafasi zaidi ya moja apewe kama hana uwezo bora waache.

La tatu wajitahidi kutafuta story kutoka kwa waandishi na watu tofauti tofauti, sio kila siku mwandishi yule yule tu. Mwisho wa siku anatunga stori zinazofanana.
 
Umenikumbusha style ya kufoka kila movie ya Ray kigosi au kujua mwisho wa movie nini kinatokea.

Ubunifu zero, tumeshindwa hata kuiga series za US kama homeland nk.

Tuna history za kuifundisha jamii yetu
mfano boers era during nyerere
Harakati za ukombozi SADC
Jamii zetu kabla ya ukoloni etc

Lakini naona tupo busy na movies za demu mkare mwenye pesa anamtokea jamaa fukara wanafall in love jamaa anabadili maisha 😂😂😂
 
Tatizo walipojiunga kwenye kampeni ya "mama mkanye mwanao" ndio wanalipia sasa.
 
Back
Top Bottom