Nini nguvu ya mzazi au wazazi kwenye watu tunaotarajia kuoa au kuolewa nao

mazaga one

JF-Expert Member
Apr 16, 2015
2,463
3,932
Mimi ni kijana wa kiume ambaye nipo kwenye mahusiano na binti wa kabila X. Binti anaupendo kwa kweli na anajua kupenda haswa ila changamoto iliyopo wazazi wangu kila nikikaa nao wananionya sana kuhusu hilo kabila na inatokea mara nyingine mzazi wangu ananipigia kelele nyingi akinisihi niachane na huyo binti wa kabila X.

Je, ndugu zangu wa humu ndani kuna mtu ambaye ashawahi kupitia changamoto kama hii?

Je, nini nguvu ya wazazi kukataa kuoa au kuolewa kwenye kabila fulani?

Naombeni msaada wenu na maoni yenu kwani nipo njia panda na binti wa watu naona kabisa nampotezea muda na sijaweza kumwambia chochote mpaka sasa na ananipenda sana ila kila nikifikiria maneno ya mzazi wangu nakuwa nachanganyikiwa. Najitahidi kumpotezea lakini binti hachoki kuwa karibu yangu kunitafuta na kunijali.

Naombeni msaada wenu wakuu.

Nawasilisha.
 
Kosa la babu anakuja kuadhibiwa mjukuu..hiyo inatokana labda historia za nyuma kuwa kabila flani wanatabia flani au mila flani mara nyingi inakuwa ni dhana..kuwa mtu flani ni mchawi basi na kizazi chake chote watakuwa wachawi.Vitu kama hivyo.
Ila ukubwa dawa labda wameona kitu.kaanao chini wakupe sababu,alafu utachambua ipi pumba na ipi mchele.
 
Aisee kijana usije ukafanya kosa la kupenda papuchi ukaacha ushauri wa wazazi.
Papuchi unaweza replace wakati wowote lakini sio wazazi.

Halafu ngoja nikwambie mwanamke hapendi kamwe... Wanaangalia maisha sasa wee usijejidanganya oh ananipenda ananijali hamna hilo. Sikiliza wazazi... Huyo for the time being endelea kula papucbi kama anaileta mwenyewe. Kauli mbiu yetu ni kwamba papuchi haisuswi.
 
Aisee kijana usije ukafanya kosa la kupenda papuchi ukaacha ushauri wa wazazi.
Papuchi unaweza replace wakati wowote lakini sio wazazi.

Halafu ngoja nikwambie mwanamke hapendi kamwe... Wanaangalia maisha sasa wee usijejidanganya oh ananipenda ananijali hamna hilo. Sikiliza wazazi... Huyo for the time being endelea kula papucbi kama anaileta mwenyewe. Kauli mbiu yetu ni kwamba papuchi haisuswi.
Nimekuelewa Mkuu ushauri wako.Asante
 
Kosa la babu anakuja kuadhibiwa mjukuu..hiyo inatokana labda historia za nyuma kuwa kabila flani wanatabia flani au mila flani mara nyingi inakuwa ni dhana..kuwa mtu flani ni mchawi basi na kizazi chake chote watakuwa wachawi.Vitu kama hivyo.
Ila ukubwa dawa labda wameona kitu.kaanao chini wakupe sababu,alafu utachambua ipi pumba na ipi mchele.
Sawa mkuu
 
Mimi ni kijana wa kiume ambaye nipo kwenye mahusiano na binti wa kabila X. Binti anaupendo kwa kweli na anajua kupenda haswa ila changamoto iliyopo wazazi wangu kila nikikaa nao wananionya sana kuhusu hilo kabila na inatokea mara nyingine mzazi wangu ananipigia kelele nyingi akinisihi niachane na huyo binti wa kabila X.

Je, ndugu zangu wa humu ndani kuna mtu ambaye ashawahi kupitia changamoto kama hii?

Je, nini nguvu ya wazazi kukataa kuoa au kuolewa kwenye kabila fulani?

Naombeni msaada wenu na maoni yenu kwani nipo njia panda na binti wa watu naona kabisa nampotezea muda na sijaweza kumwambia chochote mpaka sasa na ananipenda sana ila kila nikifikiria maneno ya mzazi wangu nakuwa nachanganyikiwa. Najitahidi kumpotezea lakini binti hachoki kuwa karibu yangu kunitafuta na kunijali.

Naombeni msaada wenu wakuu.

Nawasilisha.
wazazi wanapowakataza usiowe flan au nyumba flan huwezi jua pengine kunakitu kimejificha nyuma ya pazia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi sidhani kama ni sahihi kumjaji mtu eti kwasababu ya kabila lake, kwasababu hakuna mtu yeyote aliyefanya juhudi yoyote kuwa na hilo kabila alilonalo ni inatokea tu unawazaliwa na wazazi ambao ni wachaga au wazaramu na automatically na wewe unakua hiyo kabila.
Maoni yangu muoe huyo dada kama ninyi wenyewe mmependana na kuridhiana. Mimi nadhani kuna umri unafika wazazi wako wanatakiwa kuwa watu wa kukushauri na kuonyesha njia, lakini sio wa kukutolea maamuzi. Maisha ni kuchagua na si kuchaguliwa.😎
 
Back
Top Bottom