Sauti za Wananchi
Senior Member
- Sep 2, 2014
- 113
- 138
Mchakato wa Katiba mpya ulisimamiwa vyema na iliyokuwa Tume ya Marekebisho ya Katiba chini ya uenyekiti wa Jaji Joseph Warioba, ambao waliandaa rasimu ya Katiba iliyokabidhiwa Desemba 30, mwaka 2013.
Jaji Warioba na wenzeke walijikuta katika wakati mgumu, kwa kuvamiwa na kushambuliwa na watu ambao inadaiwa hawaikubali Rasimu hiyo bali wanaunga mkono Katiba pendekezwa ambayo ilitengenezwa na Bunge la Katiba.
Kutokana na kutoelewana ndani ya Bunge hilo, Aprili 16, mwaka 2014 wajumbe wa Bunge hilo wa upinzania zaidi ya 200 waliunda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) walisusia vikao kwa madai ya kutoridhishwa na mwenendo wa Bunge hilo ikiwamo kutozingatia maoni ya wananchi yaliyopo kwenye Rasimu ya Warioba.
Wajumbe waliobaki ndani ya Bunge hilo waliendelea hadi ikapatikana Katiba pendekezwa Oktoba 2014 na kubaki hatua ya kupigiwa kura ya maoni ambayo hufanywa na wananchi kwa mujibu wa sheria. Katiba inayopendekezwa chini ya uenyekiti wa Samuel Sitta, ilikabidhiwa kwa Rais wa Muungano na Zanzibar kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011, na kubaki kupelekwa kwa wananchi kupiga kura ambayo ilipagwa Aprili 30, mwaka 2015, lakini haikufanyika.
Hadi sasa Katiba hiyo ni kiporo ambacho haijulikani lini kitapashwa moto.
Je wewe kama mwananchi una maoni gani kuhusu kusimamishwa kwa mchakato huu?
Je unadhani maoni ya wananchi yalichukuliwa ipasavyo?
Unadhani ni sahihi kwa mchakato huo kufufuliwa hivi sasa na je ifanywe kwa njia gani.
MAONI YAKO MUHIMU.
KARIBU.
Jaji Warioba na wenzeke walijikuta katika wakati mgumu, kwa kuvamiwa na kushambuliwa na watu ambao inadaiwa hawaikubali Rasimu hiyo bali wanaunga mkono Katiba pendekezwa ambayo ilitengenezwa na Bunge la Katiba.
Kutokana na kutoelewana ndani ya Bunge hilo, Aprili 16, mwaka 2014 wajumbe wa Bunge hilo wa upinzania zaidi ya 200 waliunda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) walisusia vikao kwa madai ya kutoridhishwa na mwenendo wa Bunge hilo ikiwamo kutozingatia maoni ya wananchi yaliyopo kwenye Rasimu ya Warioba.
Wajumbe waliobaki ndani ya Bunge hilo waliendelea hadi ikapatikana Katiba pendekezwa Oktoba 2014 na kubaki hatua ya kupigiwa kura ya maoni ambayo hufanywa na wananchi kwa mujibu wa sheria. Katiba inayopendekezwa chini ya uenyekiti wa Samuel Sitta, ilikabidhiwa kwa Rais wa Muungano na Zanzibar kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011, na kubaki kupelekwa kwa wananchi kupiga kura ambayo ilipagwa Aprili 30, mwaka 2015, lakini haikufanyika.
Hadi sasa Katiba hiyo ni kiporo ambacho haijulikani lini kitapashwa moto.
Je wewe kama mwananchi una maoni gani kuhusu kusimamishwa kwa mchakato huu?
Je unadhani maoni ya wananchi yalichukuliwa ipasavyo?
Unadhani ni sahihi kwa mchakato huo kufufuliwa hivi sasa na je ifanywe kwa njia gani.
MAONI YAKO MUHIMU.
KARIBU.