GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,546
- 108,876
Leo alipokuwa mgeni rasmi wa mbio za Miguu huko Mkoani Kilimanjaro Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Mwanahabari Mkongwe,Mwanasheria Mbobezi na aliyewahi pia kuwa Mhadhiri Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dr. Harrison Mwakyembe alitoa ' Kali ' ya mwaka kwa kutoa ' Kijembe ' murua kabisa kwa Watanzania hasa baada ya Kukasirishwa kama siyo Kukerwa na Kitendo cha Tuzo zote za juu isipokuwa moja tu kuchukuliwa na Wageni kutoka nchini Kenya.
" Watanzania ni Watu wa ajabu sana na Mimi huwa siwaelewi yaani hapa katika mashindano haya ya Kukimbia Kili Marathon wamefanya vibaya na hawawezi kukimbia ila ngoja wafanye maandamano huko barabarani halafu Polisi wapige Mabomu uone watakavyochomoka mbio na ndani ya dakika moja ukimpigia kila Mtu Simu atakuambia ameshafika Kwake na mwingine atakuambia tayari ameshalala huku mwingine anaoga na wote wanakaa mbali. Sasa nawashangaa sana kwanini zile mbio zao za Kufyatuka wanazotuonyeshaga wakiwa wanafurumushwa na Polisi wasizihamishie hapa na kila mwaka Watanzania tukawa tunazoa tu hizi Tuzo? ".
Shikamoo Waziri Dr. Mwakyembe.
Nawasilisha.
" Watanzania ni Watu wa ajabu sana na Mimi huwa siwaelewi yaani hapa katika mashindano haya ya Kukimbia Kili Marathon wamefanya vibaya na hawawezi kukimbia ila ngoja wafanye maandamano huko barabarani halafu Polisi wapige Mabomu uone watakavyochomoka mbio na ndani ya dakika moja ukimpigia kila Mtu Simu atakuambia ameshafika Kwake na mwingine atakuambia tayari ameshalala huku mwingine anaoga na wote wanakaa mbali. Sasa nawashangaa sana kwanini zile mbio zao za Kufyatuka wanazotuonyeshaga wakiwa wanafurumushwa na Polisi wasizihamishie hapa na kila mwaka Watanzania tukawa tunazoa tu hizi Tuzo? ".
Shikamoo Waziri Dr. Mwakyembe.
Nawasilisha.