Nini madhara ya kutokwenda jeshini kwa aliemaliza form six mwaka huu

Truly

JF-Expert Member
Jan 27, 2011
228
32
Habari zenu wana jamvi
Kuna mtoto wa kaka kamaliza form six mwaka huu na kapangiwa kwenda jeshini mwenzi ujao. Hataki kabisa kwenda huko jeshini. Naombeni kujua impact yake ili nikambwagie tusije kulaumiane baadae. Yeye anasema jeshi halina ishu mara ataenda baadae akimaliza chuo mara sijui nini. Mimi sikwenda jeshini maana enzi zangu jeshi lilikuwa limeshafutwa. Nitashukuru kupata mawili matatu kutoka kwenu.
 
Wapo ambao hawajaenda na chuoni wameenda kama kawaida. Hakuna tatizo kwa nijuavyo mimi.
Pia kwa wasichana ushauri wasiende maana wajeda watafaidi
 
Wapo ambao hawajaenda na chuoni wameenda kama kawaida. Hakuna tatizo kwa nijuavyo mimi.
Pia kwa wasichana ushauri wasiende maana wajeda watafaidi

Huyu ninaemzungumzia ni mvulana ingepaswa aende ila hataki. Ndio nikataka kujua kama kuna madhara yoyote nimpe angalizo mapema before its too late.
 
mtakapopeleka maombi ya jira na wakisema waliomaliza kuanzia mwaka wenu lazima wake na cheti cha jeshi usije hapa kupiga mayowe
 
Mwambie anipe hiyo nafasi, nimehitimu chuo 2011 nina upper second class tatizo tangu nimalize sijapata ajira niliyoitarajia,kwss naona nibora niende jeshi nikatumikie nchi yangu,ajira nzuri uraiani naona zina wenyewe
 
Huyu ninaemzungumzia ni mvulana ingepaswa aende ila hataki. Ndio nikataka kujua kama kuna madhara yoyote nimpe angalizo mapema before its too late.

Mkuu hataki nimeona yupo serious kwamba hataki tumeshatumia muda mwingi kubishana nkaona hatufikii muafaka. Nataka nikishapata data hapa nikaongee nae tena
 
Habari zenu wana jamvi
Kuna mtoto wa kaka kamaliza form six mwaka huu na kapangiwa kwenda jeshini mwenzi ujao. Hataki kabisa kwenda huko jeshini. Naombeni kujua impact yake ili nikambwagie tusije kulaumiane baadae. Yeye anasema jeshi halina ishu mara ataenda baadae akimaliza chuo mara sijui nini. Mimi sikwenda jeshini maana enzi zangu jeshi lilikuwa limeshafutwa. Nitashukuru kupata mawili matatu kutoka kwenu.

si wa kwanza kutokwenda. na hakuna chochote cha kuhofia mkuu
 
Wakati jeshi lilipokuwepo kipindi hiko kwa.mujibu wa sheria kama leo hii Wangapi hawakwenda na hatua gani walichukuliwa?? tuache kupeana presha za bure. Huyo Mtoto aende kwasbb ni wa kiumeni ila apart from hapo nothing else.
 
kwenye ajira kuanzia mwaka wao atatakiwa kuwa na cv ya j.k.t vinginevyo hapati kazi...!
 
Asanteni kwa mchango wenu wa mawazo. Ngoja nikaongee nae mara ya mwisho maana kama safari anatakiwa aanze jumapili kwenda Tabora ikiwa tutaelewana. I just pray aende na hivi ni miezi mitatu tu sio mingi
 
Asanteni kwa mchango wenu wa mawazo. Ngoja nikaongee nae mara ya mwisho maana kama safari anatakiwa aanze jumapili kwenda Tabora ikiwa tutaelewana. I just pray aende na hivi ni miezi mitatu tu sio mingi

kwa sisi ambao utumwa wa kuajiliwa tulishaachana nao siku nyingi huwa kauli za wanasiasa wala hazina uzito kwetu sitajii kuomba kazi popote pale najitahidi kuzalisha ajira hata chache.

Na huyu ridhiwani kikwete anakwenda lini jkt?
 
Kwa kweli uoga upo maana hawakawii kukwamisha vitu maana serikali haitabiriki
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom