Nini madhara ya kupanda kwa gharama za umeme kwa Taifa?

Wakudadavuwa

JF-Expert Member
Feb 17, 2016
17,506
15,997
Kwa baadhi ya nchi mfano Afrika kusini kupanda bei ya mkate na maziwa inaweza kugharimu hata kazi ya Raisi au lundo la watunga sera ili kumnusuru Raisi.

Umeme ni gharama mtambuka kwani huathiri majumbani,biashara na viwandani.Kupanda gharama za umeme au kukosekana kwa umeme Tanzania limekuwa ni kaa la moto kwa mawaziri wengi hata kama sababu ni za ukame.

Kwa utangulizi huo juu ni dhahiri serikali ya nchi yeyote hujihami dhidi ya bei na upatikanaji wa nishati ya umeme.Kwani baada ya EWURA kutangaza kupanda gharama za umeme John Mnyika waziri kivuli wa nishati na madili alikuja na tamko zito la kupinga huku akiomba Waziri wa Nishati na Madini Prof.Muhongo na Raisi Dr.Magufuli Watengue uamuzi wa EWURA huku akiahidi kuja na mswada binafsi dhidi ya uamuzi huo.

Ni kweli umeme ulishapandishwa gharama kinyemela toka mwezi disemba kabla hata ya kuidhinishwa? kwanini Tanesco walifanya bila kibali?

Nini madhara ya kupanda gharama za nishati kiuchumi,kisiasa na kijamii?

Nakaribisha hoja za wadau.
 
A
Kwa baadhi ya nchi mfano Afrika kusini kupanda bei ya mkate na maziwa inaweza kugharimu hata kazi ya Raisi au lundo la watunga sera ili kumnusuru Raisi.

Umeme ni gharama mtambuka kwani huathiri majumbani,biashara na viwandani.Kupanda gharama za umeme au kukosekana kwa umeme Tanzania limekuwa ni kaa la moto kwa mawaziri wengi hata kama sababu ni za ukame.

Kwa utangulizi huo juu ni dhahiri serikali ya nchi yeyote hujihami dhidi ya bei na upatikanaji wa nishati ya umeme.Kwani baada ya EWURA kutangaza kupanda gharama za umeme John Mnyika waziri kivuli wa nishati na madili alikuja na tamko zito la kupinga huku akiomba Waziri wa Nishati na Madini Prof.Muhongo na Raisi Dr.Magufuli Watengue uamuzi wa EWURA huku akiahidi kuja na mswada binafsi dhidi ya uamuzi huo.

Ni kweli umeme ulishapandishwa gharama kinyemela toka mwezi disemba kabla hata ya kuidhinishwa? kwanini Tanesco walifanya bila kibali?

Nini madhara ya kupanda gharama za nishati kiuchumi,kisiasa na kijamii?

Nakaribisha hoja za wadau.
Acha porojo za eti Mnyika, Wapinzania wamependekeza mangapi mazuri wakapuuzwa,Nonsensical!
 
Hakuna Madhara kama wapandishaji wanakijua wanachokifanya!

Otherwise, Hesabu hazidanganyi

Kama Mwenye nyumba anakarabati nyumba kabla ya kupandisha kodi, Nani atalaumu? Kuna Madhara?

Kinyume cha hapo, HAKUNA MUUJIZA!

Tuendelee kutumbuana hata siku zisizo za kazi

Labda ndo kazi yetu!
 
Thread kama hizi Kutoka Lumumba fc tulizitarajia baada ya mukulu kuongea na kumtengua DG wa tanesco...ila angekaa kimya na nyie Nina uhakika 100% mngekaa kimya.

Unataka kutuambia tangia December waziri wa Wizara husika hakujua kuwa Umeme umepandishwa kinyamela kama usemavyo na kama alijua mm nadhani hilo ndo lingekuwa kosa sahihi la kumuondoa DG wa tenesco.

Na kama waziri alijua kuwa bei ya Umeme imepandishwa kinyamela kama usemavyo na akakaa kimya anafanya nn ofisini mpaka muda huu..nadhani yeye ndo alitakiwa kutumbuliwa kwa kutofanya Kazi yake vzuri.

Na kama hakujua aje hadharani atueleze shirika lilipo chini ya Wizara yake linawezaje kufanya jambo kubwa kiasi hiki bila yeye kujua.

Wakudadavuwa ulishakuja na Uzi hapa ukilalamika kuwa tanesco wamepandisha bei ya Umeme kinyamela bila kupata kibali Kutoka ewura..naomba unitag huo uzi tafadhali mkuu
 
Kama hujui kitu kaa kimya,hili ni baraza la fikra pevu si duara la kampeni.
I am neither Lumumba nor Ufipa (as you put it). I am talking from the scientific point of view! It is not because Mnyika has proposed to raise a bill in the Parliament which , among others reasons has prompted that change!
 
Hakuna Madhara kama wapandishaji wanakijua wanachokifanya!

Otherwise, Hesabu hazidanganyi

Kama Mwenye nyumba anakarabati nyumba kabla ya kupandisha kodi, Nani atalaumu? Kuna Madhara?

Kinyume cha hapo, HAKUNA MUUJIZA!

Tuendelee kutumbuana hata siku zisizo za kazi

Labda ndo kazi yetu!
Umeme ni "public good" kuna ruzuku nyingi sana za serikali.
 
I am neither Lumumba nor Ufipa (as you put it). I am talking from the scientific point of view! It is not because Mnyika has proposed to raise a bill in the Parliament which , among others reasons has prompted that change!
Electricity is a public good.Had it supplied in commercial terms we could not have witnessed a meaningful industrialization even in EU and US.
 
Thread kama hizi Kutoka Lumumba fc tulizitarajia baada ya mukulu kuongea na kumtengua DG wa tanesco...ila angekaa kimya na nyie Nina uhakika 100% mngekaa kimya.

Unataka kutuambia tangia December waziri wa Wizara husika hakujua kuwa Umeme umepandishwa kinyamela kama usemavyo na kama alijua mm nadhani hilo ndo lingekuwa kosa sahihi la kumuondoa DG wa tenesco.

Na kama waziri alijua kuwa bei ya Umeme imepandishwa kinyamela kama usemavyo na akakaa kimya anafanya nn ofisini mpaka muda huu..nadhani yeye ndo alitakiwa kutumbuliwa kwa kutofanya Kazi yake vzuri.

Na kama hakujua aje hadharani atueleze shirika lilipo chini ya Wizara yake linawezaje kufanya jambo kubwa kiasi hiki bila yeye kujua.

Wakudadavuwa ulishakuja na Uzi hapa ukilalamika kuwa tanesco wamepandisha bei ya Umeme kinyamela bila kupata kibali Kutoka ewura..naomba unitag huo uzi tafadhali mkuu
Sikuwahi kuleta uzi na pia sijachangia mjadala wowote japo kuna uzi humu una malalamiko ya kwamba umeme umepanda toka disemba.Je ungefurahi umeme ukipanda wewe binafsi?
 
Electricity is a public good.Had it supplied in commercial terms we could not have witnessed a meaningful industrialization even in EU and US.
Well, a public good indeed! Is making proposals to raise tariff justify sacking!
 
Sikuwahi kuleta uzi na pia sijachangia mjadala wowote japo kuna uzi humu una malalamiko ya kwamba umeme umepanda toka disemba.Je ungefurahi umeme ukipanda wewe binafsi?

Sijafurahia ila concern yangu ni kwamba....rais asingeliongelea hili hata nyie Lumumba fc msingeliongelea hilo nina uhakika nalo 100%

Kingine kama umeme umepanda tangia December kama usemavyo na wazuri husika akawa kimya nani wa kulaumiwa kwa ukimya huo.

Mm tangia watoe ule uchafu ulikuwa unaitwa service charge nikinunua Umeme wa 10,000 kwa M-PESA huwa napata units 14.8. Hata Jana nimenunua nikapata hzo hzo na ikabidi ninunue Umeme mwingi zaidi nikitarajia kuwa leo bei ingepanda kwa hyo ningepata kaunafuu.
 
Sijafurahia ila concern yangu ni kwamba....rais asingeliongelea hili hata nyie Lumumba fc msingeliongelea hilo nina uhakika nalo 100%

Kingine kama umeme umepanda tangia December kama usemavyo na wazuri husika akawa kimya nani wa kulaumiwa kwa ukimya huo.

Mm tangia watoe ule uchafu ulikuwa unaitwa service charge nikinunua Umeme wa 10,000 kwa M-PESA huwa napata units 14.8. Hata Jana nimenunua nikapata hzo hzo na ikabidi ninunue Umeme mwingi zaidi nikitarajia kuwa leo bei ingepanda kwa hyo ningepata kaunafuu.
Haya mkuu wa ufipa.
 
Well, a public good indeed! Is making proposals to raise tariff justify sacking!
No one here in JF has the real fact that caused dismisal of Tanesco MD....all are mere speculations....The matter of concern here is the rationale of Prof.Muhongo to suspend tariff hike,was it correct?
 
Haya mkuu wa ufipa.

Nashukuru kwa kuelewa siku nyingine usikimbilie kuanzisha Uzi hapa baada ya mtu fulani kuongea kitu fulani au kukaa kimya kwa sababu mtu fulani Jamaa kimya...hata kama upo upande wake 100% ni busara na Uhuru wa fikra kwenda tofauti naye pale ambapo unaona maamuzi yake yanaumiza wananchi waliowengi. Makofi tu kwa mukulu hata kama yeye na serikali yake wanaburunda sio sawa.

Lumumba fc muwe na Uhuru wa fikra msishikiliwe fikra na mtu fulani.

Kwa upande wangu nadhani hata waziri wa Nishati na Madini alitakiwa awajibishwe kwani ameacha mchakato ambao mukulu anasema upo kinyume na matakwa ya serikali yake uendelee mpaka Mwisho. Nadhani kuna gharama zimetumika kuendesha mchakato wa kupandisha bei ya Umeme mpaka hapo Ewura ilipopeleka pendekezo lake Tanesco. Ina maana mchakato huu ulikuwa unaendeshwa ndani ya Wizara ambayo hayo mashirika hapo chini yake bila waziri husika wala karibu Mkuu kujua...hakuna mtu Mwenye akili anaweza kubaliana na udanganyifu huu.

Kama DG wa tanesco ametumbuliwa kwa kupeleka pendekezo la nyongeza ya bei ya Umeme ewura je??huyo DG wa ewura ambaye ndo aliendesha mchakato wa kutafuta maoni kwa wadau na kuja na hilo pendekezo kwa Tanesco la kuongeza bei ya Umeme kwa 8.5% badala ya ombi la Tanesco la 18% tunamfanyeje au tunamvutia pumzi kwanza.
 
Nashukuru kwa kuelewa siku nyingine usikimbilie kuanzisha Uzi hapa baada ya mtu fulani kuongea kitu fulani au kukaa kimya kwa sababu mtu fulani Jamaa kimya...hata kama upo upande wake 100% ni busara na Uhuru wa fikra kwenda tofauti naye pale ambapo unaona maamuzi yake yanaumiza wananchi waliowengi. Makofi tu kwa mukulu hata kama yeye na serikali yake wanaburunda sio sawa.

Lumumba fc muwe na Uhuru wa fikra msishikiliwe fikra na mtu fulani.

Kwa upande wangu nadhani hata waziri wa Nishati na Madini alitakiwa awajibishwe kwani ameacha mchakato ambao mukulu anasema upo kinyume na matakwa ya serikali yake uendelee mpaka Mwisho. Nadhani kuna gharama zimetumika kuendesha mchakato wa kupandisha bei ya Umeme mpaka hapo Ewura ilipopeleka pendekezo lake Tanesco. Ina maana mchakato huu ulikuwa unaendeshwa ndani ya Wizara ambayo hayo mashirika hapo chini yake bila waziri husika wala karibu Mkuu kujua...hakuna mtu Mwenye akili anaweza kubaliana na udanganyifu huu.

Kama DG wa tanesco ametumbuliwa kwa kupeleka pendekezo la nyongeza ya bei ya Umeme ewura je??huyo DG wa ewura ambaye ndo aliendesha mchakato wa kutafuta maoni kwa wadau na kuja na hilo pendekezo kwa Tanesco la kuongeza bei ya Umeme kwa 8.5% badala ya ombi la Tanesco la 18% tunamfanyeje au tunamvutia pumzi kwanza.
Kwa hiyo unataka watumbuliwe.
 
Kama hujui kitu kaa kimya,hili ni baraza la fikra pevu si duara la kampeni.

Hapa umemtumia Mnyika kama sehemu ya kujilinda na wale jamaa wenye hoja nzito ambazo zinaisumbua serekali. Lakini iko wazi wewe na wenzako kabla ya tangazo la Serekali na Rais kugongelea msumari leo, mlikuwa mnajifanya eti wapinzani wanataka huduma ya umeme lakini hawataki kulipia. Saa hii unajifanya kupima upepo kwa kumtumia Mnyika kama sehemu ya kuogopa kushambuliwa. Nirudi kwenye hoja yako, kilichofanywa na serekali kuhusu kuzuia hilo ongezeko la kinyemela limetufurahisha wengi, ila tunachojiuliza muda wote ule serekali haikuona hivyo vikao vya kutaka kupandisha umeme mpaka jana ndio wamejua wakati tangazo limetoka?
 
Hapa umemtumia Mnyika kama sehemu ya kujilinda na wale jamaa wenye hoja nzito ambazo zinaisumbua serekali. Lakini iko wazi wewe na wenzako kabla ya tangazo la Serekali na Rais kugongelea msumari leo, mlikuwa mnajifanya eti wapinzani wanataka huduma ya umeme lakini hawataki kulipia. Saa hii unajifanya kupima upepo kwa kumtumia Mnyika kama sehemu ya kuogopa kushambuliwa. Nirudi kwenye hoja yako, kilichofanywa na serekali kuhusu kuzuia hilo ongezeko la kinyemela limetufurahisha wengi, ila tunachojiuliza muda wote ule serekali haikuona hivyo vikao vya kutaka kupandisha umeme mpaka jana ndio wamejua wakati tangazo limetoka?
Acha ramli,jenga hoja.
 
Hapa umemtumia Mnyika kama sehemu ya kujilinda na wale jamaa wenye hoja nzito ambazo zinaisumbua serekali. Lakini iko wazi wewe na wenzako kabla ya tangazo la Serekali na Rais kugongelea msumari leo, mlikuwa mnajifanya eti wapinzani wanataka huduma ya umeme lakini hawataki kulipia. Saa hii unajifanya kupima upepo kwa kumtumia Mnyika kama sehemu ya kuogopa kushambuliwa. Nirudi kwenye hoja yako, kilichofanywa na serekali kuhusu kuzuia hilo ongezeko la kinyemela limetufurahisha wengi, ila tunachojiuliza muda wote ule serekali haikuona hivyo vikao vya kutaka kupandisha umeme mpaka jana ndio wamejua wakati tangazo limetoka?
Acha ramli,jenga hoja.
 
Kwa hiyo unataka watumbuliwe.


Kabisa.... serikali hii inayojibaraguza kuwa ni serikali ya wanyonge na imeenda mbali zaidi na kusema yoyote atakayewabebesha mzigo wananchi atakiona cha mtema kuni...Je huyu waziri aliyeacha mchakato wa kuwatesa wanyonge pamoja na katibu Mkuu wake hawatakiwi kutumbuliwaaaa....kwangu watumbuliweeeee..

Huyu DG wa ewura ambaye ndo amekuja na nyongeza ya bei ya Umeme ya 8.5% kwa wanyonge wa Tanzania na kutishia kauli mbiu ya serikali ya viwanda tumfanyeje??? Atumbuliweeeee
 
Back
Top Bottom