Nini maana ya "Vetting", na kuna umuhimu upi wa kufanya "Vetting" Serikalini na kwenye Taasisi zetu

S.N.Jilala

JF-Expert Member
Jan 26, 2012
540
507
TAFAKURI.

Nini maana ya "Vetting", na kuna umuhimu upi wa kufanya "Vetting" Serikalini na kwenye Taasisi zetu zote?.

Vetting ni neno la Kiingereza, lakini sijui linaitwaje kwa Lugha yetu ya Kiswahili. Vetting ni mchakato unaofanyika hasa wa kufuatilia Historia ya mtu kabla ya kumwajili au kumpa zawadi ya heshima iwe kwenye Taasisi au serikalini. Watu wengi tunaamini kuwa watu ambao wanatakiwa kufanyiwa Vetting ni watu ambao wanataka kuajiliwa katika Idara nyeti tu hasa USALAMA WA TAIFA. Lakini, sehemu nyingi kama zinataka kuajili watu huwafanyia watu Vetting, japokuwa si ile Vetting ambayo anafanyiwa ambaye anataka kupatiwa nafasi kubwa.

Kwa kazi ya kawaida, mara nyingi Vetting yao ni kutumia CV ya mtu fulani na watu wanaokufahamu ukiacha ndugu zako yaani Referee. Hii ni Vetting fupi kabisa ambayo inasaidia angalau kujua A,B,C fupi kuhusu mtu ambaye mnatakiwa kumwajili. Kama huyo mtu anataka kuchukua nafasi kubwa sana kwenye Taasisi, iwe ya serikali au binafsi, anatakiwa kufanyiwa Vetting kubwa zaidi. Uchunguzi lazima uwe wa kina zaidi kuhusu mtu huyo.

Kwa mfano, hamuwezi kama Taifa kumuweka mtu kuwa Mkuu wa Majeshi kabla ya Taasisi husika hazijamfatilia kwa undani kabisa kuhusu Historia yake kiutendaji na kimaadili pamoja na vitu vingine ambavyo wataalamu wa vetting wanavijua.

Jambo hili la Vetting halijaanza leo, limeanza zamani sana. Hata enzi za Mababu zetu hili jambo lilikuwepo sana. Ili Jamii ikutawaze kuwa Chief kwa mfano, lazima uwe umeshaonyesha huko nyuma Uzalendo na Uaminifu mkubwa sana katika utendaji wako na umeonyesha mambo makubwa pia. Hapo zamani Jamii zetu zilikuwa zinazingatia mambo mengi sana, mojawapo ni kuwa na uwezo mkubwa wa kutumia "Nguvu za Giza" kuwazidi wote katika Jamii.

Vetting ilikuwepo zama na zama na Mababu zetu walikuwa wanafanya japo zinatofautiana na za sasa hasa katika njia, mbinu na kinachoangaliwa hasa. Mengine kwa mfano Uzalendo, Uwezo wa kutenda jambo husika na Maadili huwa ni mambo ya msingi sana tangu zamani. Na endapo Mtawala yoyote akagundua kuwa Msaidizi wake kwa mfano hana sifa zile ambazo alizitegemea, hakika wale wanaohusika na "Vetting" mara nyingi walikuwa wanapata wakati mgumu sana.

Nini faida ya "Vetting"

1. Kujirizisha kama huyo mtu mnayetaka kumwajili kama ana sifa ambazo amesema anazo.

2. Kuangalia mambo mengi sana ukiacha uwezo tu wa kufanya hiyo kazi; pia kuangalia kama ana maadili ya kutosha kukabidhiwa nafasi hiyo kubwa.

3. Kujirizisha zaidi na zaidi maana huyo mtu anaweza kuwa ni Jasusi na mkaliingiza Taifa lenu katika kashfa kubwa na kuhatarisha USALAMA WA TAIFA LENU.

4. Kujua uwezo ambao anao kama kweli alisitahili kuwa nao, hapa ni kufuatilia kama kweli anachokionyesha ni halali kabisa.

5. Kufuatilia kwa undani kama alishawahi kupatikana na makosa ya jinai kama kuuwa na mengine ili kujua kwa nini alifanya hivyo; n.k

Kwa hiyo basi, kama nilivyosema hapo juu, kama mtu anataka kuchukua nafasi kubwa zaidi Kiserikali au Taasisi binafsi, ni lazima afanyiwe Vetting. Tena Vetting ya undani ambayo ni Professional Vetting. Taasisi binafsi au Serikali inawajibika kufanya hivyo kwa sababu huyo mtu anaenda kukabidhiwa majukumu makubwa mojawapo ya majukumu ni ya SIRI KUBWA kuhusu Taifa au Taasisi. Ndiyo maana, Mataifa mengi wanapenda sana kuwapatia nafasi kubwa watu waliopitia maswala ya USALAMA WA TAIFA kwa sababu wanajua umuhimu wa kutunza siri. Au wanapatiwa watu ambao ni waaminifu sana na wamethibitika hivyo kulingana na walikopita baada ya Vetting kufanyika.

Rais wa Taifa lolote lile, mara nyingi huletewa majina ambayo yameshafanyiwa Vetting na Taasisi husika. Na endapo itathibitika kuwa wasaidizi aliwachagua hawana sifa ambazo alizitegemea, lazima asikitike sana na inabidi awe na wajibu wa kutatua changamoto hiyo. Na aliyethibitika hivyo, moja ya njia rahisi kabisa ni kuwajibika haraka sana iwezekanavyo ili angalau aonekane kuwa naye ameguswa na jambo hilo. Ndiyo maana tunaona mara nyingi viongozi wengi wakiwajibika Duniani kote.

Vetting ni jambo ambalo lina njia, mbinu, ujuzi na malengo yake. Nchi zilizoendelea ni rahisi sana kufanya Vetting kwa sababu Historia za watu kuhusu wao binafsi na kazi zao huko nyuma ziko wazi kabisa na zinaelewaka. Pia zipo kwenye mitandao. Huku kwetu, ni ngumu sana kufanya Vetting kwa sababu ya maisha tuliyonayo kwa ujumla. Kwa mfano, ni kawaida sana kuzaliwa na ukawa mtu mzima ukiwauliza wazazi wako pengine hawajui ulizaliwa lini na wao hawajui walizaliwa lini. Na hili lipo sana katika jamii za Wakulima na Wafugaji.

14/03/2017
 
Hivi Raisi anafanyiwa Vetting? Kama ni ndio nani anafanya na nani anazifikisha kwenye vyama ili viweze kufanya maamuzi sahihi?

Kama Rais kama kiongozi mkuu hafanyiwi vetting kwa nini wengine wafanyiwe?
 
Hivi Raisi anafanyiwa Vetting? Kama ni ndio nani anafanya na nani anazifikisha kwenye vyama ili viweze kufanya maamuzi sahihi?

Kama Rais kama kiongozi mkuu hafanyiwi vetting kwa nini wengine wafanyiwe?
Mimi nadhani ili Chama kimpitishe mgombea yoyote lazima kuna Vetting kali, kuna Vetting Kubwa hufanyika ndani ya chama na pia hapa hata watu wa USALAMA huwa wanashauri ikibidi. Vigezo wanajua wenyewe ndani ya chama husika.
 
Asante kwa somo la vetting. Vetting ilikuwa zamani wakati wa Nyerere tuu, ingefanyika hata Mkapa asingekuwa rais wala huyu. Awamu hii ni awamu ya hapa kazi tuu, sifa ya kuteuliwa sio historia wala vetting bali ni bidii ya mtu uchapakazi na delivery.

Kama lengo la kuibuka hii mada kuhusu vetting ni issues za Daudi Bashite na Paul Makonda, huyu ni mchapa Kazi hodari hahitaji vetting na tumeisha mshauri rais azipuuze hizi ni kelele tuu za uongo, majungu na fitna za wauza unga.

Kumbe ni Uongo, Uzushi, Fitna, Majungu, Wivu na Kijicho Dhidi ya Mafanikio Yake!. Makonda Wapuuze! .

Watanzania ni watu wa ajabu sana!, Wanamwaminije Gwajima kuliko Rais wao?!.

Na ikitokea ikawa ni kweli Gwajima ana vyeti vinavyothibitisha Daudi Bashite ndiye Paul Makonda, tumemshauri Magufuli kufanya mambo matatu haya.
1. Kutengua uteuzi wa Paul Makonda kutokuwa tena Mkuu wa Mkoa wa DSM.
2. Kutoa msamaha wa jumla kwa wote waliofoji vyeti,majina na kufanya udanganyifu.
3. Amteue Daudi Bashite kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.
Heko Rais Magufuli kwa msimamo thabiti. Shikilia hapo hapo. Kelele za Mlango Zisikukoseshe Usingizi!
Hizi kelele ziishe.

Paskali
 
TAFAKURI.

Nini maana ya "Vetting", na kuna umuhimu upi wa kufanya "Vetting" Serikalini na kwenye Taasisi zetu zote?.

Vetting ni neno la Kiingereza, lakini sijui linaitwaje kwa Lugha yetu ya Kiswahili. Vetting ni mchakato unaofanyika hasa wa kufuatilia Historia ya mtu kabla ya kumwajili au kumpa zawadi ya heshima iwe kwenye Taasisi au serikalini. Watu wengi tunaamini kuwa watu ambao wanatakiwa kufanyiwa Vetting ni watu ambao wanataka kuajiliwa katika Idara nyeti tu hasa USALAMA WA TAIFA. Lakini, sehemu nyingi kama zinataka kuajili watu huwafanyia watu Vetting, japokuwa si ile Vetting ambayo anafanyiwa ambaye anataka kupatiwa nafasi kubwa.

Kwa kazi ya kawaida, mara nyingi Vetting yao ni kutumia CV ya mtu fulani na watu wanaokufahamu ukiacha ndugu zako yaani Referee. Hii ni Vetting fupi kabisa ambayo inasaidia angalau kujua A,B,C fupi kuhusu mtu ambaye mnatakiwa kumwajili. Kama huyo mtu anataka kuchukua nafasi kubwa sana kwenye Taasisi, iwe ya serikali au binafsi, anatakiwa kufanyiwa Vetting kubwa zaidi. Uchunguzi lazima uwe wa kina zaidi kuhusu mtu huyo.

Kwa mfano, hamuwezi kama Taifa kumuweka mtu kuwa Mkuu wa Majeshi kabla ya Taasisi husika hazijamfatilia kwa undani kabisa kuhusu Historia yake kiutendaji na kimaadili pamoja na vitu vingine ambavyo wataalamu wa vetting wanavijua.

Jambo hili la Vetting halijaanza leo, limeanza zamani sana. Hata enzi za Mababu zetu hili jambo lilikuwepo sana. Ili Jamii ikutawaze kuwa Chief kwa mfano, lazima uwe umeshaonyesha huko nyuma Uzalendo na Uaminifu mkubwa sana katika utendaji wako na umeonyesha mambo makubwa pia. Hapo zamani Jamii zetu zilikuwa zinazingatia mambo mengi sana, mojawapo ni kuwa na uwezo mkubwa wa kutumia "Nguvu za Giza" kuwazidi wote katika Jamii.

Vetting ilikuwepo zama na zama na Mababu zetu walikuwa wanafanya japo zinatofautiana na za sasa hasa katika njia, mbinu na kinachoangaliwa hasa. Mengine kwa mfano Uzalendo, Uwezo wa kutenda jambo husika na Maadili huwa ni mambo ya msingi sana tangu zamani. Na endapo Mtawala yoyote akagundua kuwa Msaidizi wake kwa mfano hana sifa zile ambazo alizitegemea, hakika wale wanaohusika na "Vetting" mara nyingi walikuwa wanapata wakati mgumu sana.

Nini faida ya "Vetting"

1. Kujirizisha kama huyo mtu mnayetaka kumwajili kama ana sifa ambazo amesema anazo.

2. Kuangalia mambo mengi sana ukiacha uwezo tu wa kufanya hiyo kazi; pia kuangalia kama ana maadili ya kutosha kukabidhiwa nafasi hiyo kubwa.

3. Kujirizisha zaidi na zaidi maana huyo mtu anaweza kuwa ni Jasusi na mkaliingiza Taifa lenu katika kashfa kubwa na kuhatarisha USALAMA WA TAIFA LENU.

4. Kujua uwezo ambao anao kama kweli alisitahili kuwa nao, hapa ni kufuatilia kama kweli anachokionyesha ni halali kabisa.

5. Kufuatilia kwa undani kama alishawahi kupatikana na makosa ya jinai kama kuuwa na mengine ili kujua kwa nini alifanya hivyo; n.k

Kwa hiyo basi, kama nilivyosema hapo juu, kama mtu anataka kuchukua nafasi kubwa zaidi Kiserikali au Taasisi binafsi, ni lazima afanyiwe Vetting. Tena Vetting ya undani ambayo ni Professional Vetting. Taasisi binafsi au Serikali inawajibika kufanya hivyo kwa sababu huyo mtu anaenda kukabidhiwa majukumu makubwa mojawapo ya majukumu ni ya SIRI KUBWA kuhusu Taifa au Taasisi. Ndiyo maana, Mataifa mengi wanapenda sana kuwapatia nafasi kubwa watu waliopitia maswala ya USALAMA WA TAIFA kwa sababu wanajua umuhimu wa kutunza siri. Au wanapatiwa watu ambao ni waaminifu sana na wamethibitika hivyo kulingana na walikopita baada ya Vetting kufanyika.

Rais wa Taifa lolote lile, mara nyingi huletewa majina ambayo yameshafanyiwa Vetting na Taasisi husika. Na endapo itathibitika kuwa wasaidizi aliwachagua hawana sifa ambazo alizitegemea, lazima asikitike sana na inabidi awe na wajibu wa kutatua changamoto hiyo. Na aliyethibitika hivyo, moja ya njia rahisi kabisa ni kuwajibika haraka sana iwezekanavyo ili angalau aonekane kuwa naye ameguswa na jambo hilo. Ndiyo maana tunaona mara nyingi viongozi wengi wakiwajibika Duniani kote.

Vetting ni jambo ambalo lina njia, mbinu, ujuzi na malengo yake. Nchi zilizoendelea ni rahisi sana kufanya Vetting kwa sababu Historia za watu kuhusu wao binafsi na kazi zao huko nyuma ziko wazi kabisa na zinaelewaka. Pia zipo kwenye mitandao. Huku kwetu, ni ngumu sana kufanya Vetting kwa sababu ya maisha tuliyonayo kwa ujumla. Kwa mfano, ni kawaida sana kuzaliwa na ukawa mtu mzima ukiwauliza wazazi wako pengine hawajui ulizaliwa lini na wao hawajui walizaliwa lini. Na hili lipo sana katika jamii za Wakulima na Wafugaji.

14/03/2017
Vetting ni lazima serikalini.Kwani ulitaka kusemaje?
 
Vetting ni muhimu sana kwa taasisi mbalimbali za Serikali na hata zisizo za kiserikali. Hii ni kwasababu pamoja na mambo mengine lakini usalama wa nchi ni jambo la msingi zaidi kuzingatia. Maadui wa nchi wanapenyezwa sehemu yoyote ile iwe Serikalini, taasisi binafsi, NGOs n.k.

Hivyo kuweka nchi salama zaidi ndio maana kumewekwa utaratibu wa kuwepo mamlaka mbalimbali (mf Sumatra, Brela, TIC, BOT, nk) zinazohusika na usajili, udhibiti,
ufuatiliaji n.k

Hivyo kama isingekuwa vetting ndani ya CCM kupitia kamati yake ya maadili na nidhamu basi leo hii Mh Lowassa angekuwa raisi wa nchi hii
 
Siku hizi hakuna vetting ndio maana tunaona nyaraka za serikali zenye muhuri wa SIRI zinakuwa hapa JF
 
TAFAKURI.

Nini maana ya "Vetting", na kuna umuhimu upi wa kufanya "Vetting" Serikalini na kwenye Taasisi zetu zote?.

Vetting ni neno la Kiingereza, lakini sijui linaitwaje kwa Lugha yetu ya Kiswahili. Vetting ni mchakato unaofanyika hasa wa kufuatilia Historia ya mtu kabla ya kumwajili au kumpa zawadi ya heshima iwe kwenye Taasisi au serikalini. Watu wengi tunaamini kuwa watu ambao wanatakiwa kufanyiwa Vetting ni watu ambao wanataka kuajiliwa katika Idara nyeti tu hasa USALAMA WA TAIFA. Lakini, sehemu nyingi kama zinataka kuajili watu huwafanyia watu Vetting, japokuwa si ile Vetting ambayo anafanyiwa ambaye anataka kupatiwa nafasi kubwa.

Kwa kazi ya kawaida, mara nyingi Vetting yao ni kutumia CV ya mtu fulani na watu wanaokufahamu ukiacha ndugu zako yaani Referee. Hii ni Vetting fupi kabisa ambayo inasaidia angalau kujua A,B,C fupi kuhusu mtu ambaye mnatakiwa kumwajili. Kama huyo mtu anataka kuchukua nafasi kubwa sana kwenye Taasisi, iwe ya serikali au binafsi, anatakiwa kufanyiwa Vetting kubwa zaidi. Uchunguzi lazima uwe wa kina zaidi kuhusu mtu huyo.

Kwa mfano, hamuwezi kama Taifa kumuweka mtu kuwa Mkuu wa Majeshi kabla ya Taasisi husika hazijamfatilia kwa undani kabisa kuhusu Historia yake kiutendaji na kimaadili pamoja na vitu vingine ambavyo wataalamu wa vetting wanavijua.

Jambo hili la Vetting halijaanza leo, limeanza zamani sana. Hata enzi za Mababu zetu hili jambo lilikuwepo sana. Ili Jamii ikutawaze kuwa Chief kwa mfano, lazima uwe umeshaonyesha huko nyuma Uzalendo na Uaminifu mkubwa sana katika utendaji wako na umeonyesha mambo makubwa pia. Hapo zamani Jamii zetu zilikuwa zinazingatia mambo mengi sana, mojawapo ni kuwa na uwezo mkubwa wa kutumia "Nguvu za Giza" kuwazidi wote katika Jamii.

Vetting ilikuwepo zama na zama na Mababu zetu walikuwa wanafanya japo zinatofautiana na za sasa hasa katika njia, mbinu na kinachoangaliwa hasa. Mengine kwa mfano Uzalendo, Uwezo wa kutenda jambo husika na Maadili huwa ni mambo ya msingi sana tangu zamani. Na endapo Mtawala yoyote akagundua kuwa Msaidizi wake kwa mfano hana sifa zile ambazo alizitegemea, hakika wale wanaohusika na "Vetting" mara nyingi walikuwa wanapata wakati mgumu sana.

Nini faida ya "Vetting"

1. Kujirizisha kama huyo mtu mnayetaka kumwajili kama ana sifa ambazo amesema anazo.

2. Kuangalia mambo mengi sana ukiacha uwezo tu wa kufanya hiyo kazi; pia kuangalia kama ana maadili ya kutosha kukabidhiwa nafasi hiyo kubwa.

3. Kujirizisha zaidi na zaidi maana huyo mtu anaweza kuwa ni Jasusi na mkaliingiza Taifa lenu katika kashfa kubwa na kuhatarisha USALAMA WA TAIFA LENU.

4. Kujua uwezo ambao anao kama kweli alisitahili kuwa nao, hapa ni kufuatilia kama kweli anachokionyesha ni halali kabisa.

5. Kufuatilia kwa undani kama alishawahi kupatikana na makosa ya jinai kama kuuwa na mengine ili kujua kwa nini alifanya hivyo; n.k

Kwa hiyo basi, kama nilivyosema hapo juu, kama mtu anataka kuchukua nafasi kubwa zaidi Kiserikali au Taasisi binafsi, ni lazima afanyiwe Vetting. Tena Vetting ya undani ambayo ni Professional Vetting. Taasisi binafsi au Serikali inawajibika kufanya hivyo kwa sababu huyo mtu anaenda kukabidhiwa majukumu makubwa mojawapo ya majukumu ni ya SIRI KUBWA kuhusu Taifa au Taasisi. Ndiyo maana, Mataifa mengi wanapenda sana kuwapatia nafasi kubwa watu waliopitia maswala ya USALAMA WA TAIFA kwa sababu wanajua umuhimu wa kutunza siri. Au wanapatiwa watu ambao ni waaminifu sana na wamethibitika hivyo kulingana na walikopita baada ya Vetting kufanyika.

Rais wa Taifa lolote lile, mara nyingi huletewa majina ambayo yameshafanyiwa Vetting na Taasisi husika. Na endapo itathibitika kuwa wasaidizi aliwachagua hawana sifa ambazo alizitegemea, lazima asikitike sana na inabidi awe na wajibu wa kutatua changamoto hiyo. Na aliyethibitika hivyo, moja ya njia rahisi kabisa ni kuwajibika haraka sana iwezekanavyo ili angalau aonekane kuwa naye ameguswa na jambo hilo. Ndiyo maana tunaona mara nyingi viongozi wengi wakiwajibika Duniani kote.

Vetting ni jambo ambalo lina njia, mbinu, ujuzi na malengo yake. Nchi zilizoendelea ni rahisi sana kufanya Vetting kwa sababu Historia za watu kuhusu wao binafsi na kazi zao huko nyuma ziko wazi kabisa na zinaelewaka. Pia zipo kwenye mitandao. Huku kwetu, ni ngumu sana kufanya Vetting kwa sababu ya maisha tuliyonayo kwa ujumla. Kwa mfano, ni kawaida sana kuzaliwa na ukawa mtu mzima ukiwauliza wazazi wako pengine hawajui ulizaliwa lini na wao hawajui walizaliwa lini. Na hili lipo sana katika jamii za Wakulima na Wafugaji.

14/03/2017

Tulikotoka ni wazi tunaweza kujitetea kuwa kuwa nchi zinazoendelea kufanya "vetting" ni jambo gumu lakini ni wakati tujiulize tunafanya nini kutatua changamoto hii na nyingine?

kuanza kujenga mifumo yenye data base za wananchi na kuweka anwani za makazi zinazoeleweka na kufikika inaweza kuwa hatua kubwa.

ni kazi bure kukuta unatakiwa kujaza fomu na katika fomu unatakiwa kujaza anwani unakaa wapi lakini hata wewe mwenyewe unapajua physically tu lakini hata mtaa wenyewe hujui unaitwaje.
 
Back
Top Bottom