Jitihada haiondoi kudra au (Jitihada haishindi kudra).
Maana yake jambo alilopanga Mungu binadamu hawezi kulipangua.
Jitihada ni harakati za Mungu na kudra ni mipango ya Mungu.
Mfano kama kuna jambo unahangaika nalo ili lifanikiwe hayo mahangaiko yako ndiyo jitihada baada ya kuhangaika jambo hilo likaleta matokeo tofauti na jitihada (mahangaiko) yako basi hapo watu wanaweza kusema kwamba; jitihada haishindi kudra, yaani Mungu ndiye amepanga jambo hilo liende kinyume na jitihada zako.
Jitihada hazishindi kudra>Bidii au juhudi katika jambo lolote unalofanya haziwezi kuzaa matunda kuzidi vile ulivyoandikiwa na Mungu (kudura/kudra/qadr)
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.