Nini maana ya kutoa maoni juu ya katiba mpya?

Miwatamu

JF-Expert Member
Oct 2, 2012
1,450
487
Watanzania woooote kwa sasa tupo katika kipindi cha mpito cha kuandika Katiba mpya itakayotokana na maoni tunayoyachangia hivi sasa. Katika michango inayoendelea, wamejitokeza watu ambao wameeleza mapendekezo mengi mapya ambayo hayakuwahi kuwepo katika katiba ya sasa! Na hii ndiyo maana halisi ya mapendekezo mapya.

Wakati hayo yakiendelea, baadhi ya wananchi wametoa mapendekezo yao ya kutaka kuvunjwa kwa muungano au ufanyiwe marekebisho. Kitu cha ajabu, wakati bado mapendekezo yanaendelea kukusanywa, tayari kuna viongozi serikalini wamesimama na kutamka bayana kuwa hao wote wenye ndoto ya kutaka muungano ufanyiwe mabadiliko wanaota ndoto ya mchana. Kamwe haitatokea.........!!

Sasa nauliza, kama tayari viongozi wetu wanayo majibu ya nini kitakachoandikwa ndani ya katiba mpya kwa nini wapoteze muda kuzunguka nchi huku wakikausha mate ya wakesha hoi bure?
Tulijadili na hili...............
 
Watanzania woooote kwa sasa tupo katika kipindi cha mpito cha kuandika Katiba mpya itakayotokana na maoni tunayoyachangia hivi sasa. Katika michango inayoendelea, wamejitokeza watu ambao wameeleza mapendekezo mengi mapya ambayo hayakuwahi kuwepo katika katiba ya sasa! Na hii ndiyo maana halisi ya mapendekezo mapya.
Wakati hayo yakiendelea, baadhi ya wananchi wametoa mapendekezo yao ya kutaka kuvunjwa kwa muungano au ufanyiwe marekebisho. Kitu cha ajabu, wakati bado mapendekezo yanaendelea kukusanywa, tayari kuna viongozi serikalini wamesimama na kutamka bayana kuwa hao wote wenye ndoto ya kutaka muungano ufanyiwe mabadiliko wanaota ndoto ya mchana. Kamwe haitatokea.........!!
Sasa nauliza, kama tayari viongozi wetu wanayo majibu ya nini kitakachoandikwa ndani ya katiba mpya kwa nini wapoteze muda kuzunguka nchi huku wakikausha mate ya wakesha hoi bure?
Tulijadili na hili...............

Ndio maana tunasema kwa sheria ya mchakato wa katiba mpya ilivyo, hakutakuwa na katiba mpya. Ni usanii wa CCM tu! Shein anasema kuwa sera ya CCM ni serikali mbili, wakati katiba ndio itakayo amua hilo, mbona anakuwa kama anadictate sura ya muungano. Awaachie wananchi waamue.
 
Back
Top Bottom