Nini maana ya kupigwa tunch?

Wajameni, nimemsikiliza Mh Rais ila pale aliposema maneno kupigwa tunch nimeshindwa kumuelewa. Nisaidiane..
Mkuu Geza kupiga tanchi ni kuruka dau katika ujanja kuwahi na ujanja kupata.

Tanchi imefanyika kwa kununua ndege mbili kati ya ndege 10 za order ya ndege za shirika la ndege la Kazakhstan ambazo wangenunua kwa mkopo. Tuliweza kuwapiga tanchi Kazakhstan kwa sababu sisi tulilipa cash! . Ni jambo la ajabu sana kwa nchi kununua kitu kikubwa kama ndege kwa cash badala ya hire purchase! . Na kwa nchi masikini kama Tanzania ni ajabu zaidi.

Rais amesema badala ya Tanzania kutoa order za ndege zake ambazo huwa zina take time kutengenezwa, tutaendelea kupiga tanchi order za watu wengine kwa kubeba koba la mihela na kuzilipia cash.

Kitu ambacho masikini rais wetu hakujua na washauri wake hawakumweleza, ni sababu za manunuzi kwa hire purchase badala ya cash.

Sababu kuu ya hire purchase ni security delivery na performance guarantee.

Ukinunua kwa cash, delivery inafanyika at the point of sale (POS) kwa kama ni gari then ni FOB, unakabidhiwa mzigo wako biashara imeishia hapo. Utasafirisha mwenyewe na ukifika usipofanya kazi, utajijua mwenyewe, no security, no guarantee. Hata nchi tajiri wenye cash wananunua kwa hire purchase ili kupata delivery na performance guarantee.

Ukinunua kwa hire purchase, delivery inafanyikia nchini mwako, at the place of performance, kama kuna hitilafu yoyote, muuzaji ndie anabeba gharama, hivyo hii ni security performance guarantee, kama ni gari ni CIF Dar es Salaam. Baada ya kulipia CIF, ni jukumu la muuzaji kufanya delivery ya mzigo wako kwako unatumiwa bills of landing na kwenda kuchukua mzigo wako tena wengine unaongeza pesa kidogo tuu wanakufanyia clearance.

Hiki tulichofanya kwa kununua midege kwa cash, kwa sasa tunamshangilia na kujiona wajanja tunajua kupiga tanchi, lakini tutakuja kujuta huko baadae, endapo kama midege hii ni mibovu ikagomea environment yetu, au engines zikaleta hitilafu, imekula kwetu!.

Pasco
 
Mkuu Geza kupiga tanchi ni kuruka dau katika ujanja kuwahi na ujanja kupata.

Tanchi imefanyika kwa kununua ndege mbili kati ya ndege 10 za order ya ndege za shirika la ndege la Kazakhstan ambazo wangenunua kwa mkopo. Tuliweza kuwapiga tanchi Kazakhstan kwa sababu sisi tulilipa cash! . Ni jambo la ajabu sana kwa nchi kununua kitu kikubwa kama ndege kwa cash badala ya hire purchase! . Na kwa nchi masikini kama Tanzania ni ajabu zaudi.

Rais amesema badala ya Tanzania kutoa order za ndege zake ambazo huwa zina take time kutengenezwa, tutaendelea kupiga tanchi order za watu wengine kwa kubeba koba la mihela na kuzilipia cash.
Pasco

Nonsense, at the expense of masikini kukosa aspirin, masikini kukosa mikopo, Nonsense
 
Nonsense, at the expense of masikini kukosa aspirin, masikini kukosa mikopo, Nonsense
Mkuu Retired kiukweli ni ajabu, ila Watanzania hawajashangaa!, lengo la hire purchase pia ni guarantee ya adaptation kama sio adaptive zinarudishwa unajengewa nyingine more adaptive. Kwanza tumenunua ndege za watu, kisha tunalipa cash kwa guarantee gani my God!.

Tukisema tuchunguze sense ya aliyeshauri haya ili tujiridhishe kama ana senses kweli au ni nonsense, tutakuja kuambiwa tunatukana watu! .

Kuna maamuzi yanafanywa na nchi yetu yanashangaza sana, hadi kuniaminisha baadhi ya viongozi wetu are just insane! .

Kwa vile utafiti umeisha onyesha kuwa Tanzania kila watu 4, mmoja ni insane, naomba kukiri mimi ni mmoja kati ya wanne hao.
Pasco
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom