everybody
JF-Expert Member
- Oct 30, 2010
- 337
- 103
Nimelitafakari sana hili suala la posho za wabunge, na mwishowe nikaona kama vile JK na Ikulu yake wanatuchezea akili watanzania. Hivi kama mtu amekuomba kitu, halafu ukamwambia nakukubalia ila tumia busara, je inamaanisha kwamba umemkatalia? Kwa tafsiri yangu hapa ni kwamba JK aliwakubalia wabunge walipwe hizo posho, ila alitaka kutumia maneno ambayo mwisho wa siku kama wananchi wata 'react' kama walivyofanya apate upenyo wa kutokea. Kauli ya JK kwamba anakubali ila wabunge watumie busara, kama kweli ndivyo alivyosema, naona kama ni ya kuudhi na ambayo haina mwelekeo na sidhani kama ilistahili kutoka kwa kiongozi wa nchi.
Kiongozi wa nchi anatakiwa awe ni mtu mwenye kutoa msimamo bila kubabaisha, na maneno yake yawe yenye kueleweka, kwani kama mkuu wa nchi, na amiri jeshi mkuu, ulimi wake ukiteleza kidogo anaweza kutuingiza katika hatari ambayo hatukuitegemea. Natamani sana kama lile dokezo lililotoka kwa JK kwenda kwa Pinda, kuhusu hizo posho lingewekwa hadharani na hapo ndo tungejua JK ni mtu wa aina gani.
Inasikitisha sana. Wote kuanzia hao wabunge wanaotaka kujiongezea posho ili waweze kulipa madeni yao waliyoyaingia kwa ajili ya kufanikisha hanasa zao, na huyu Rais wetu sijui wanatutakia nini sisi Watanzania!
Kiongozi wa nchi anatakiwa awe ni mtu mwenye kutoa msimamo bila kubabaisha, na maneno yake yawe yenye kueleweka, kwani kama mkuu wa nchi, na amiri jeshi mkuu, ulimi wake ukiteleza kidogo anaweza kutuingiza katika hatari ambayo hatukuitegemea. Natamani sana kama lile dokezo lililotoka kwa JK kwenda kwa Pinda, kuhusu hizo posho lingewekwa hadharani na hapo ndo tungejua JK ni mtu wa aina gani.
Inasikitisha sana. Wote kuanzia hao wabunge wanaotaka kujiongezea posho ili waweze kulipa madeni yao waliyoyaingia kwa ajili ya kufanikisha hanasa zao, na huyu Rais wetu sijui wanatutakia nini sisi Watanzania!