scatter
JF-Expert Member
- Feb 15, 2013
- 1,667
- 925
Habari zenu wadau,
Kipindi kampeni zikiendelea kushika kasi kuna kitu kusema ukweli sisi kama Watanzania tuna tafakari mara mbili mbili hasa aina ya kampeni zinazofanyika na chama cha CCM.
Kumekuwa na wasanii wa muziki wa kizazi kipya, wasanii wa maigizo ambao wameshirikishwa kushiriki katika kampeni za CCM lakini ukitazama kwa jicho kali maana ya maudhui ya kazi zao za sanaa za kila siku wengi wao zimejaa mapenzi na kauli zenye ukakasi kusikiliza au kutizama pia maisha yao mfano hao bongo movie ni maisha ya kihuni na skendo zisizoisha.
Leo hii tunapokuja kufanya kampeni za chama lazima utamaduni na desturi za Kitanzania zisambazwe kwa njia ya sanaa kwani inakutanisha Watanzania wote na tunaangalia mustakbali wa maisha yetu kwa kipindi cha miaka mitano ijayo. Kwann inatumia pesa nyingi kulipa vikundi hivi ambavyo kwa baadhi yao kazi zao haziendani na utamaduni wa Mtanzania?
Je, hawa wenyeviti wa CCM kila mkoa na wilaya wana kazi gani?
Kwenye vyuo kuna wataalamu wa siasa ambao wamesome fani ya siasa kwanini wasishirikishwe katika kampeni za CCM ili sisi Watanziania tupewe madini ya kisiasa kuliko kila siku kuwatazama kina zuchu, Ali Kiba, Aunt Ezekiel, Wema Sepetu na wengineo.
Kuna vikundi vya ngoma za kitamaduni, sarakasi, ngonjera na mashairi ambao wanaakisi utamaduni wa Mtanzania moja kwa moja katika kazi zao kwa nini hawashirikishwi kwenye kampeni za Chama cha Mapinduzi?
Hakika picha mnayotupa sisi watanzania ni kwamba CCM mnatuona sisi ni wapumbavu sana kwa kutumia makundi haya ya sanaa yasioyokuwa na tija kwetu.
Haya yote ipo siku yatafika mwisho.
Kipindi kampeni zikiendelea kushika kasi kuna kitu kusema ukweli sisi kama Watanzania tuna tafakari mara mbili mbili hasa aina ya kampeni zinazofanyika na chama cha CCM.
Kumekuwa na wasanii wa muziki wa kizazi kipya, wasanii wa maigizo ambao wameshirikishwa kushiriki katika kampeni za CCM lakini ukitazama kwa jicho kali maana ya maudhui ya kazi zao za sanaa za kila siku wengi wao zimejaa mapenzi na kauli zenye ukakasi kusikiliza au kutizama pia maisha yao mfano hao bongo movie ni maisha ya kihuni na skendo zisizoisha.
Leo hii tunapokuja kufanya kampeni za chama lazima utamaduni na desturi za Kitanzania zisambazwe kwa njia ya sanaa kwani inakutanisha Watanzania wote na tunaangalia mustakbali wa maisha yetu kwa kipindi cha miaka mitano ijayo. Kwann inatumia pesa nyingi kulipa vikundi hivi ambavyo kwa baadhi yao kazi zao haziendani na utamaduni wa Mtanzania?
Je, hawa wenyeviti wa CCM kila mkoa na wilaya wana kazi gani?
Kwenye vyuo kuna wataalamu wa siasa ambao wamesome fani ya siasa kwanini wasishirikishwe katika kampeni za CCM ili sisi Watanziania tupewe madini ya kisiasa kuliko kila siku kuwatazama kina zuchu, Ali Kiba, Aunt Ezekiel, Wema Sepetu na wengineo.
Kuna vikundi vya ngoma za kitamaduni, sarakasi, ngonjera na mashairi ambao wanaakisi utamaduni wa Mtanzania moja kwa moja katika kazi zao kwa nini hawashirikishwi kwenye kampeni za Chama cha Mapinduzi?
Hakika picha mnayotupa sisi watanzania ni kwamba CCM mnatuona sisi ni wapumbavu sana kwa kutumia makundi haya ya sanaa yasioyokuwa na tija kwetu.
Haya yote ipo siku yatafika mwisho.