Baba Heri
JF-Expert Member
- Jul 23, 2013
- 1,503
- 2,222
Kwa hali ya teknolojia ya habari na mawasiliano ilivyo kwa sasa hapa Tanzania ni rahisi sana kupata habari kupitia Redio, TV, magazeti na Mitandao ya Kijamii.
Najiuliza kama mchapishaji gazeti analenga kufanya biashara kwanini anakubali media nyingine ziwasomee wateja wake kilichochapwa kwenye gazeti lake, ataliuzaje?
Mimi naamka asubuhi kabla sijatoka nyumbani nimeshasomewa magazeti yote tena kwa kubembelezwa kuitwa mpenzi msikilizaji, napata wapi hamu ya kununua gazeti?
Maana kuna watangazaji wengine wanasoma habari halafu wanaichambua kuliko gazeti lenyewe nisipotosheka na uchambuzi naingia mitandaoni, gazeti sikutani nalo kabisa labda kwenye maandazi.
Nawashauri mfikirie upya huu utaratibu wa kuchapa magazeti na kutusomea bure.
Najiuliza kama mchapishaji gazeti analenga kufanya biashara kwanini anakubali media nyingine ziwasomee wateja wake kilichochapwa kwenye gazeti lake, ataliuzaje?
Mimi naamka asubuhi kabla sijatoka nyumbani nimeshasomewa magazeti yote tena kwa kubembelezwa kuitwa mpenzi msikilizaji, napata wapi hamu ya kununua gazeti?
Maana kuna watangazaji wengine wanasoma habari halafu wanaichambua kuliko gazeti lenyewe nisipotosheka na uchambuzi naingia mitandaoni, gazeti sikutani nalo kabisa labda kwenye maandazi.
Nawashauri mfikirie upya huu utaratibu wa kuchapa magazeti na kutusomea bure.