Nini Kumbukumbu Yako Ya Baba Wa Taifa?

Nyani Ngabu

Platinum Member
May 15, 2006
92,002
112,625
Katika kumkumbuka Baba wa taifa, naomba mchangie kumbukumbu zenu binafsi au zinginezo mlizonazo za hayati Mwalimu.

Nianze mwenyewe: wakati niko mtoto mdogo mwanzoni mwa miaka ya themanini baba yangu mpendwa siku moja alinipeleka kwenda kusali kwenye kanisa la Mtakatifu Peter pale Oysterbay. Siku hiyo tulikwenda kusali hapo kwa makusudi kabisa. Makusudi yenyewe yalikuwa ni kumwona kwa macho Raisi Nyerere na ikiwezekana kumsalimia na kushikana naye mkono. Wakati misa inaendelea mimi mawazo, akili, na macho yangu yalikuwa yameelekezwa kwa Raisi Nyerere. Nakumbuka alikuwa anapenda kukaa pale mbele mbele karibu na altare. Siku hiyo mimi na baba yangu mpendwa tuliwahi na kuapata nafasi ya kukaa kwenye moja ya viti (mabenchi) ya mbele ambapo tuliweza kumwona vizuri Raisi Nyerere. Macho yangu hayakubanduka kwake. Nashindwa hata kusimulia jinsi nilivyokuwa najisikia asubuhi ile. Kwa vile Raisi Nyerere alikuwa na mazoea ya kusalimiana na watu pale nje kwenye ngazi baada ya misa kuisha, mimi na baba yangu mpendwa tuliwahi kutoka na tukajipanga kwenye mwanzo wa zile ngazi za kushukia chini ili tuweze kusalimiana naye na kumwona ka karibu. Ndoto yangu ilitimia pale alipotoka na kuanza kusalimiana na watu. Alipofika tulipokuwa tumesimama sisi akanishika kichwa halafu akanyoosha mkono wake na mimi nikanyoosha wa kwangu na tukasalimiana. Siku hiyo nilikuwa ni mtoto mwenye furaha isiyo na kifani. We fikiria, nimeshikana mkono na Raisi Nyerere...nakwambia nilirudi nyumbani na kuanza kuwatambia marafiki zangu, ndugu zangu, na kila mtu niliyekutana naye. Kamwe sitaweza kuisahau siku hiyo kwani nami nilijipatia sekunde zangu kumi na tano za umaarufu.

Haya washirika wenzangu tuendelee.....
 
Mie Nyerere namkumbuka kwenye mkutano mmoja wa kampeni mwaka 1995,musoma mjini,akimpigia debe mkapa.Alihutubia kwa makini sana,katika meza kuu alikuwepo pia mgombea wa ubunge jimbo la musoma mjini kupitia ccm,lakini cha ajabu Nyerere alivyotofauti na watu wengine alisema hivi huku akimponda mgombea huyo wa ccm,
namnukuu"Kama ningelikua mpiga kura wa jimbo la musoma mjini,huyu
mgombea wa ubunge kupitia ccm asingepata kura yangu,ni mla rushwa"

Najiuliza kila siku leo hii kuna mtu wa ccm anaweza kusema kauli hii?
 
Mimi nakumbuka siku mwili wa marehemu ulivyorudishwa kutoka London, asubuhi na mapema tulidamka mimi na rafiki zangu wawili kwenda kuupokea, uwanja wa ndege wa zamani, siku hiyo ilikuwa ni siku very "tense" ,kama kumbukumbu zangu zingalipo ilipigwa mizinga kadhaa ya heshima na kikosi cha mizinga. jeneza lilovikwa bendera ya taifa lilipotoka kwenye ndege umati wa watu ulizizima kwa majonzi.
Halafu Jeneza liliwekwa katika gari maalum la kijeshi huku raisi Benjamin William Mkapa akiwa katika gari hilo nadhani na makamanda wakuu wa jeshi akiwemo Jenerali Mboma wakiongoza msafara .
Sisi wananchi hususan Vijana tulikimbia mchakamchaka tukilisindikiza jeneza lilobeba mwili wa mwalimu. kwa kweli kwa mtu aliyemshuhudia Raisi Mkapa siku hiyo, atakwambia ni kwa namna gani alionekana akiwa katika lindi la mawazo tele.

Watu walikimbia siku hiyo , wapo watu waliokimbia hadi msasani kwa Mwalimu, huku wakiimba "Mkombozi Ametutoka"
Binafsi sikufika Msasani ,lakini naamini ule umbali niliokimbia ni umbali mrefu, na hii ni kwa dhati ya kuamini kwamba Mwalimu ni mtu aliyestahili kupewa heshima za kutosha.

Mwalimu yeye binafsi wakati wa kudai uhuru alikuwa akitembea kutoka Pugu mpaka mjini kufanya harakati za kudai uhuru ,just imagine umbali wa kutoka pugu mpaka posta au kariakoo utembee kwa mguu! na si mara moja, mara nyingi tu, kwa hivyo ni dhahiri vijana wale walimpa heshima Mwalimu, heshima itakayokumbukwa na vizazi vijavyo,heshima ya kumuaga shujaa kishujaa!
 
Mimi namkumbuka Nyerere katika mahojiano yake haya na Ikaweba Bunting. I wish angefufuka leo na kuyaona yaliyotusibu ktk mazuri na mabaya.

Ikaweba Bunting:- Does the Arusha Declaration still stand up today?

Mwalimu JKN:- I still travel around with it. I read it over and over to see what I would change. Maybe I would improve on the Kiswahili that was used but the Declaration is still valid: I would not change a thing. Tanzania had been independent for a short time before we began to see a growing gap between the haves and the have-nots in our country. A privileged group was emerging from the political leaders and bureaucrats who had been poor under colonial rule but were now beginning to use their positions in the Party and the Government to enrich themselves. This kind of development would alienate the leadership from the people. So we articulated a new national objective: we stressed that development is about all our people and not just a small and privileged minority.
The Arusha Declaration was what made Tanzania distinctly Tanzania. We stated what we stood for, we laid down a code of conduct for our leaders and we made an effort to achieve our goals. This was obvious to all, even if we made mistakes - and when one tries anything new and uncharted there are bound to be mistakes.
The Arusha Declaration and our democratic single-party system, together with our national language, Kiswahili, and a highly politicized and disciplined national army, transformed more than 126 different tribes into a cohesive and stable nation.
However, despite this achievement, they say we failed in Tanzania, that we floundered. But did we? We must say no. We can't deny everything we accomplished. There are some of my friends who we did not allow to get rich; now they are getting rich and they say `See, we are getting rich now, so you were wrong'. But what kind of answer is that?
The floundering of socialism has been global. This is what needs an explanation, not just the Tanzanian part of it. George Bernard Shaw, who was an atheist, said, `You cannot say Christianity has failed because it has never been tried.' It is the same with socialism: you cannot say it has failed because it has never been tried.
 
Mie namkumbuka kama kiongozi aliyekuwa na mapenzi ya kweli kwa Watanzania na Tanzania. Aliona umuhimu mkubwa wa kuwa na lugha moja ya Tanzania ili kuleta umoja miongoni mwetu. Aliona umuhimu wa njia kuu za uchumi kuwa mikononi mwa Watanzania badala ya wageni. Alijua Watanzania wengi walikuwa ni maskini hivyo wengi wasingeweza kumudu gharama za shule kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu, hivyo kuifanya elimu ya Tanzania kuwa bure kuanzia msingi mpaka chuo kikuu. Maamuzi mengi aliyoyafanya yaliweka mbele maslahi ya Watanzania. Kwa mfano pale alipokataa shinikizo toka IMF na WB la kushusha thamani ya shilingi ili kupata misaada. Mwalimu alitumia lugha nyepesi ya walala hoi ili kuwafahamisha Watanzania ni kwanini alikataa kushusha thamani ya shilingi.

Mwalimu alikuwa na kumbukumbu za hali ya juu na mkarimu sana. Watu mbali mbali ambao walishiriki katika harakati za uhuru enzi za TANU na alikuwa hajawaona miaka chungu nzima alikuwa anawakumbuka mara moja mpaka majina, kila alipopata bahati ya kukutana nao katika shughuli zake kama kiongozi wa nchi. Na mara nyingi aliwakaribisha Ikulu na kutaka kujua maisha yao yakoje. Wale ambao walikuwa na hali ngumu aliwasaidia sana hata kuwajengea nyumba au kuwapa mitaji ya kufanya biashara kama walivyoomba wenyewe au kufanyiwa mambo mengine ambayo waliyataka.

Nilihudhuria mkutano wa kutangaza vita dhidi ya nduli Idd Amin pale Diamond Jubilee kama sikosei mwaka 1978. Hotuba aliyoitoa pale ilikuwa ni moja ya hotuba nzuri sana za Mwalimu za kuwahamasisha Watanzania katika vita ile. Alisema nduli kaingia nchi mwetu. Kauwa Watanzania wenzetu na kuiba mali zao. Hatuwezi kuvumilia tena vitendo vya nduli. Sababu tunazo, nguvu tunazo na uwezo tunao.

Mwalimu kama binadamu yeyote hakuwa perfect, lakini alikuwa na mapenzi ya kweli kwa Watanzania na Tanzania, hakuwa fisadi wala mroho wa kujilimbikizia mali.


Mwenyezi amlaze mahali pema peponi~AMIN
 
Ilikuwa Mei Mosi 1985, iliyofanyika Kitaifa Mkoani Tanga na kuhudhuriwa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya Madola Bw. Sherdath Ramphal (or similar sounding name). Siku ya pili yake mvua kubwa ilinyesha mjini Tanga na kufanya barabara kubwa za lami zisipitike hasa kutokea Old Nguvumali, Kisosora, Chumbageni n.k Ikabidi Mwalimu na msafara wake wapite "Uswahilini". Ndipo nilipopata kuona Mwalimu alivyokuwa mtu wa watu... mimi na ndugu zangu tukawa tumejipanga kwenye geti la nyumbani (tulikuwa na kakibanda kakuuza machungwa toka Muheza) basi jua likiwa limeanza kupiga, na akiwa amechelewa kwenda uwanja wa ndege, msafara wake ulipita taratibu katika barabara hiyo ya mashimo (kwani haikuandaliwa kwa ajili ya msafara!) basi tu yeye kageuka upande mmoja tu anapungua watu, ndipo binamu yangu wa kike alipopiga kelele "Na huku!" Mwalimu akitabasamu akageuka na kutupungia... Ilikuwa ni siku ya furaha kwamba na sisi "tumesikiwa"... Since then, I have made it my mission... to be heard by our leaders!!
 
mie namkumbuka kwa uwezo wake wa kutoa speech na kukataza watu kuangalia tv huku yeye akiangalia na kufanya kama anaforetell mambo yatakayotokea baadae ! how interesting na mengine mengi mazuri aliyoyafanya !
 
Watanzania bwana, mnaongelea ya kumkumbuka mwalimu tu, ongeleeni mmefanya nini kumuenzi mwalimu? Sisi wote kwa kisi kikubwa ni wasaliti wa yale aliyotufundisha Mwalimu.

Sioni hata sababu ya kufurahia siku ya kifo chake, mimi huwa
ni siku ambayo ninaona aibu kwamba siwezi kuyatimiza yale yote niliyokuwa naimba nikiwa kijana, nikiwa chipukizi wa Nyerere, na badala yake naona wote sasa tumejaa ubinafsi tu.

Labda leo mtamkumbuka vizuri Mwalimu kwa kutoa sehemu ya ulicho nacho na kuwasaidia Watanzania wenzetu, ndugu zetu na majirani zetu ambao ni hoi kuliko sisi.

Nakaeribisha mashambulizi.
 
Namkumbuka pale alipotaifisha mashamba na mali mbali mbali ya binafsi ya waTZ kama shamba na mali ya Mwamwindi, nk. Akiwa na maana Ujamaa ni 'Poverty' na lazima kuishi maisha duni kama bila TV, etc wakati anajua fika yeye na mawaziri wake hawawezi ishi hivyo.
Namkumbuka alivyofanikiwa kutuweka sawa kwa hotuba kemkem lakini namkumbuka na kumheshimu sana na sana kwa kutuelea uhuru, kukubali makosa ktk siasa zake na kisha kuachia uraisi.
 
Swali kubwa kwetu sisi ni hili, mwalimu kama kiongozi alituachia umoja wa kitaifa, lugha ya kitaifa, amani na mshikamano kama taifa, baada ya hapo sisi tumefanya nini? Mwinyi atakumbukwa kwa lipi? Mkapa atakumbukwa kwa lipi, JK atakumbukwa kwa lipi? Jiulize mpaka leo, CCM inashinda kwa kutumia mafanikio ya mwalimu personally maana kama yangekuwa na chama basi tungeyaona hata mengine maana chama ni kile kile, lakini wapi.

Anyway................tuzidi kudai mabadiliko, tutafika.
 
Watanzania bwana, mnaongelea ya kumkumbuka mwalimu tu, ongeleeni mmefanya nini kumuenzi mwalimu? Sisi wote kwa kisi kikubwa ni wasaliti wa yale aliyotufundisha Mwalimu.

Sioni hata sababu ya kufurahia siku ya kifo chake, mimi huwa
ni siku ambayo ninaona aibu kwamba siwezi kuyatimiza yale yote niliyokuwa naimba nikiwa kijana, nikiwa chipukizi wa Nyerere, na badala yake naona wote sasa tumejaa ubinafsi tu.

Labda leo mtamkumbuka vizuri Mwalimu kwa kutoa sehemu ya ulicho nacho na kuwasaidia Watanzania wenzetu, ndugu zetu na majirani zetu ambao ni hoi kuliko sisi.

Nakaeribisha mashambulizi.

Anzisha thread yako mwenyewe itakayokuwa mahsusi kwa kumuenzi......
 
Swali kubwa kwetu sisi ni hili, mwalimu kama kiongozi alituachia umoja wa kitaifa, lugha ya kitaifa, amani na mshikamano kama taifa, baada ya hapo sisi tumefanya nini? Mwinyi atakumbukwa kwa lipi? Mkapa atakumbukwa kwa lipi, JK atakumbukwa kwa lipi? Jiulize mpaka leo, CCM inashinda kwa kutumia mafanikio ya mwalimu personally maana kama yangekuwa na chama basi tungeyaona hata mengine maana chama ni kile kile, lakini wapi.

Anyway................tuzidi kudai mabadiliko, tutafika.


As much as Mwalimu alikuwa mchapakazi mzuri na pan Africanist nilikuwa sikubaliani na sera zake za kiuchumi ambazo ziliturudisha nyuma miaka 50, Vita na Uganda havikustahili damu ya Mtanzania yoyote yule,alitakiwa awaunganishe watu wa dini zote lakini mwishowe alikufa huku nchi ilikiwa iko divided kidini kuliko wakati mwingine wowote ule, japo alikuwa nawangangania wenzake wahamie Dodoma lakini yeye hakuhamia huko, Kodi zetu zilitumika kumjengea nyumba kwenye jiwe huko kijijini kwake lakini baada ya miezi michache aliamua kurudi Msasani.

Mwisho naweza kusema kitu pekee ambacho kilichonitia kuhusu Mwalimu, hakuwa MWIZI kama watawala waliomfuata lakini hiyo haiondoi ukweli kuwa alikuwa ni DIVISIVE figure na haswa baada ya kuwa kumbatia wadini ambao walimpotosha sana
 
Nyani,

Kumbe kila mtu anaanzisha thread yake mwenyewe?

Nilifikiri kila thread inayoanzishwa kila mtu yuko free kuchangia?

Uko huru kuchangia lakini baki kwenye mada..
Unapoanza kuzungumzia mambo yaliyo nje ya mada ni bora uanze thread mpya la sivyo topiki nzima itachukua detour na kupoteza lengo na mwelekeo kabisa
 
Jamani kama kweli Mwalimu alikuwa mdini na divisive, basi nimenyoosha mikono. Tanzania shall never get kiongozi asiye mdini! Yaani huyu mzee mnasema alikuwa divisive? Anyway lakini kama wahenga walivyosema, huwezi pendwa na wote. kila mtu ana mapungufu yake.
 


As much as Mwalimu alikuwa mchapakazi mzuri na pan Africanist nilikuwa sikubaliani na sera zake za kiuchumi ambazo ziliturudisha nyuma miaka 50, Vita na Uganda havikustahili damu ya Mtanzania yoyote yule,alitakiwa awaunganishe watu wa dini zote lakini mwishowe alikufa huku nchi ilikiwa iko divided kidini kuliko wakati mwingine wowote ule, japo alikuwa nawangangania wenzake wahamie Dodoma lakini yeye hakuhamia huko, Kodi zetu zilitumika kumjengea nyumba kwenye jiwe huko kijijini kwake lakini baada ya miezi michache aliamua kurudi Msasani.

Mwisho naweza kusema kitu pekee ambacho kilichonitia kuhusu Mwalimu, hakuwa MWIZI kama watawala waliomfuata lakini hiyo haiondoi ukweli kuwa alikuwa ni DIVISIVE figure na haswa baada ya kuwa kumbatia wadini ambao walimpotosha sana

Ulilipa kodi kiasi gani kumjengea mwalimu hiyo nyumba, au umeamua kuleta uzushi tu?
 
Masanja,
Hizi ni mbegu zilizopandikizwa na baadhi viongozi alokuwa akiwazungumzia ktk mahojiano yake na Ikaweba Bunting. Kwa kiasi kidogo sana wamefanikiwa na kamwe wasingeweza kuyasema haya akiwa hai.

Game Theory,
Mjomba kusema Nyerere aliturudisha nyuma miaka 50 hizi ni habari za Uongo. Tanzania kama yalivyokuwa mataifa mengine tulikuwa mbele miaka 10 kutokana na ujenzi wa miundombinu mipya. Hakuna nchi ktk Afrika ilojenga miundombinu mipya kama Tanzania, wengine wote waliyakuta mengi yamewekwa na Mkoloni. Sema Ujamaa ulikuwa mrengo ambao hauwezi kufanikiwa ktk mazingira ya kibiadamu.
Alichokifanya Nyerere ni kujenga msingi wa maendeleo ya Mtanzania sema tu Ame/tumeshindwa mbinu za kutuendeleza mbele zaidi.
Mimi husema Ubepari ni sawa na Ngono. Pamoja na hatari zake zote za HIV, kisonono, kaswende na kadhalika kamwe hatuwezi kuepuka. Ni wajibu wetu hata ktk dini. Bila Ubepari hakuna biashara, hakuna biashara hakuna Uchumi, mawasiliano mazuri kati ya jamii na kadhalika.
Ni maisha ambayo kila mmoja wetu ni wajibu wake kutafuta riziki zake kupitia hatua hii isipokuwa Mwl. Nyerere ambaye alikuwa Mkatoliki aliamini kuwa kila mtu anaweza kuwa Padre.. Ngono ni haramu hadi pale utakapo fikia umri fulani.
Na huo Umri ktk uchumi wetu alidhani Tanzania inakuja fikia umri wa kujitosheleza wenyewe (KUJITEGEMEA) hivyo kutakuwepo na level ground ya Ubepari baina yetu na nchi tajiri. This was Impossible!...
Mwisho kuna jamaa mmoja toka kwa Michuzi blog ameweza kuandika mengi mazito ya kumbumbuka mwl. JKN hasa ktk ELIMU. Ni vitu ambavyo wengi wetu hatukuviona kama ni big deal lakini duh! Yes mchonga alikuwa KIONGOZI.
Mungu amzidishie pepo!
 
Masanja,
Hizi ni mbegu zilizopandikizwa na baadhi viongozi alokuwa akiwazungumzia ktk mahojiano yake na Ikaweba Bunting. Kwa kiasi kidogo sana wamefanikiwa na kamwe wasingeweza kuyasema haya akiwa hai.

Game Theory,
Mjomba kusema Nyerere aliturudishja nyuma miaka 50 hizi ni habari za Uongo. Tanzania kama yalivyokuwa mataifa mengine tulikuwa mbele miaka 10 kutokana na ujenzi wa miundombinu mipya. Wengine wote waliyakuta mengi yamewekwa na Mkoloni, sema Ujamaa ulikuwa mrengo ambao hauwezi kufanikiwa ktk mazingira ya kibiadamu.
Mimi husema Ubepari ni sawa na Ngono. Pamoja na hatari zake zote za HIV, kisonono, kaswende na kadhalika kamwe hatuwezi kuepuka. Ni wajibu wetu hata ktk dini. Bila Ubepari hakuna biashara, hakuna biashara hakuna Uchumi, mawasiliano mazuri kati ya jamii na kadhalika.
Ni maisha ambayo kila mmoja wetu ni wajibu wake kutafuta riziki zake kupitia hatua hii isipokuwa Mwl. Nyerere ambaye alikuwa Mkatoliki aliamini kuwa kila mtu anaweza kuwa Padre.. Ngono ni haramu hadi pale utakapo fikia umri fulani.
Na huo Umri ktk uchumi wetu alidhani Tanzania inakuja fikia umri wa kujitosheleza wenyewe (KUJITEGEMEA) hivyo kutakuwepo na level ground ya Ubepari baina yetu na nchi tajiri. This was Impossible!...
Mwisho kuna jamaa mmoja toka kwa michuzi ameweza kuandika mengi mazito ya kumbumbuka mwl. JKN hasa ktk ELIMU. Ni vitu ambavyo wengi wetu hatukuviona kama ni big deal lakini duh! Yes mchonga alikuwa KIONGOZI.
Mungu amzidishie pepo!


kwa hiyo unabisha kuwa economic policies alizozipursue Nyerer haziturudisha nyuma au siyo?

Unakubaliana na mamabo kama Azimio la Arusha na Operesheni vijiji?

Mjomba nakumbuka mwaka jana tulizunguzia kwa kinaga ubaga haya mamabo ya Nyerere na Legacy yake mpaka waliokuwa wakichomwa na data waliomba thread ihamishwe

ngoja nikuchekie kama bado waheshimiwa hawakuzifuta moja kwa moja
 
Ilikuwa Mei Mosi 1985, iliyofanyika Kitaifa Mkoani Tanga na kuhudhuriwa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya Madola Bw. Sherdath Ramphal (or similar sounding name). Siku ya pili yake mvua kubwa ilinyesha mjini Tanga na kufanya barabara kubwa za lami zisipitike hasa kutokea Old Nguvumali, Kisosora, Chumbageni n.k Ikabidi Mwalimu na msafara wake wapite "Uswahilini". Ndipo nilipopata kuona Mwalimu alivyokuwa mtu wa watu... mimi na ndugu zangu tukawa tumejipanga kwenye geti la nyumbani (tulikuwa na kakibanda kakuuza machungwa toka Muheza) basi jua likiwa limeanza kupiga, na akiwa amechelewa kwenda uwanja wa ndege, msafara wake ulipita taratibu katika barabara hiyo ya mashimo (kwani haikuandaliwa kwa ajili ya msafara!) basi tu yeye kageuka upande mmoja tu anapungua watu, ndipo binamu yangu wa kike alipopiga kelele "Na huku!" Mwalimu akitabasamu akageuka na kutupungia... Ilikuwa ni siku ya furaha kwamba na sisi "tumesikiwa"... Since then, I have made it my mission... to be heard by our leaders!!


kumbe wewe ni mtu wa Tanga, hivyo umeogea sana iliki ama *(joke.

namkumbuka mwalimu kwenye maandiko yake na haswa kitabu cha uongozi wetu na hatima ya Tanzania.

Nmkumbuka kama mtu aliyekuwa na msimamo binafsi na asiyeweza kuyumbishwa yumbishwa na wala rushwa.

Nakumbuka 1995 kule DODOMA alipomwambia Lowassa aseme utajiri wake kaupata wapi,wakati ni kijana sana .

Namkumbuka wakati anahutubia wanafunzi wa chuo kikuu cha monrovia kule Liberia ,aliposema kuwa jukumu la kuleta maendeleo ya africa ni ya waafrika wenyewe, intelectuals need society.

Namkumbuka mkapa alivyolia na kusema atatimiza yale yote aliyomfundisha ili kumuenzi, je alimfundisha pia kutumia ofisis za ikulu kibiashara ama alilia uongo.
 
Nakumbuka sana ule wimbo wa KABURU MATATA HIYA!!!!!! naanza kuona maana ya makabwela na matajiri.....
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom