Nini kinasababisha Mabasi ya Mikoani Siku hizi Kuchelewa kufika yaendako tofauti na zamani wakati Barabara za sasa ni Lami tupu?

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Apr 2, 2015
8,011
16,748
Nimeshangaa sana kusikia Mabasi yaendayo Mkoani Mwanza yakitoka Dar es Salaam Saa 12 Asubuhi yanafika Mwanza Saa 5 na hata Saa 6 za Usiku.

Mwaka 2006, 2007, 2008 na 2009 nimesafiri sana na Mabasi kutoka Dar es Salaam kwenda Mwanza ( tena wakati huo Barabara ilikuwa na Matatizo baadhi ya maeneo ) ila tulikuwa tunafika Nyegezi Kituoni Mwanza Saa 1 za Usiku na wapo ambao walikuwa wakifika hata Saa 12 za Jioni.

Nilidhani kwa sasa baada ya Barabara nyingi za Tanzania kuwa Mkeka ( Lami tupu ) Asante kwa Hayati Rais Dkt. Magufuli kwa Kuzijenga vyema alipokuwa Waziri chini ya Rais Mstaafu Jakaya Kikwete basi Mabasi yaendayo Mikoani yatakuwa yanawahi Kufika badala yake sasa ndiyo yanachelewa hadi Kero.

Napenda mno Mabasi yaendayo Kasi ( Spidi ) huko Mikoani au yakija Dar es Salaam na ndiyo maana nikiwa nisafiri nikienda kukata Tiketi Kwanza huwa nayaulizia Mabasi yaendayo haraka na yenye Madereva Mabandidu na Masela au yale ambayo huwa yanawakosakosa sana Ng'ombe, Mbuzi, Punda, Kuku na hata Watu ( Waendesha Baiskeli au Pikipiki ) au wale wanaopenda Kuvuka Kiholela ( Kizembe ) na nikiyapata ndiyo huwa nayapanda.
 
Ujinga mwingi sana na hizi sheria zetu za kipuuzi ni moja ya sababu kubwa! Gari inatoka Dsm kwenda Mbeya na imefungwa VTS (King’amuzi) ili kudhibiti mwendo! Cha ajabu hiyo gari inatakiwa tena kufuata ratiba za vituo mfano unao nikera gari za mbeya ikifika mpaka wa mbeya na njombe saa kumi kamili haitaruhusiwa hadi saa kumi na moja kasoro robo hivyo mnajikuta mnapoteza muda pale getuni pasi sababu ilihali huko njiani mwendo wa dereva ni kawaida na mzuri kabisa! Mhfyuu
 
Ujinga mwingi sana na hizi sheria zetu za kipuuzi ni moja ya sababu kubwa! Gari inatoka Dsm kwenda Mbeya na imefungwa VTS (King’amuzi) ili kudhibiti mwendo! Cha ajabu hiyo gari inatakiwa tena kufuata ratiba za vituo mfano unao nikera gari za mbeya ikifika mpaka wa mbeya na njombe saa kumi kamili haitaruhusiwa hadi saa kumi na moja kasoro robo hivyo mnajikuta mnapoteza muda pale getuni pasi sababu ilihali huko njiani mwendo wa dereva ni kawaida na mzuri kabisa! Mhfyuu
Igumbilo mnasimama,
Makambako mnasimama tena
Mpakani pale mnasimama tena. Ni kero sana kwakweli
 
Nimeshangaa sana kusikia Mabasi yaendayo Mkoani Mwanza yakitoka Dar es Salaam Saa 12 Asubuhi yanafika Mwanza Saa 5 na hata Saa 6 za Usiku.

Mwaka 2006, 2007, 2008 na 2009 nimesafiri sana na Mabasi kutoka Dar es Salaam kwenda Mwanza ( tena wakati huo Barabara ilikuwa na Matatizo baadhi ya maeneo ) ila tulikuwa tunafika Nyegezi Kituoni Mwanza Saa 1 za Usiku na wapo ambao walikuwa wakifika hata Saa 12 za Jioni.

Nilidhani kwa sasa baada ya Barabara nyingi za Tanzania kuwa Mkeka ( Lami tupu ) Asante kwa Hayati Rais Dkt. Magufuli kwa Kuzijenga vyema alipokuwa Waziri chini ya Rais Mstaafu Jakaya Kikwete basi Mabasi yaendayo Mikoani yatakuwa yanawahi Kufika badala yake sasa ndiyo yanachelewa hadi Kero.

Napenda mno Mabasi yaendayo Kasi ( Spidi ) huko Mikoani au yakija Dar es Salaam na ndiyo maana nikiwa nisafiri nikienda kukata Tiketi Kwanza huwa nayaulizia Mabasi yaendayo haraka na yenye Madereva Mabandidu na Masela au yale ambayo huwa yanawakosakosa sana Ng'ombe, Mbuzi, Punda, Kuku na hata Watu ( Waendesha Baiskeli au Pikipiki ) au wale wanaopenda Kuvuka Kiholela ( Kizembe ) na nikiyapata ndiyo huwa nayapanda.
Swali nzuri la kujiuliza pia vipi ukilinganisha rate ya ajali za mabasi kwa miaka hiyo na sasa hivi?
 
wamedhibitiwa sanaaa kiasi kwamba wakiona wamewahi kuliko muda wa wanaotakiwa kuingia mji flani wapo radhi wapack gari sehemu hata kwa dakika 30 ndio waendelee na safari.

ila kwa upande flani imedhibiti ajali maana miaka hiyo ni tabu
 
Kuna siku tumetoka dar saa kumi na mbili saa nne na nusu tuko dodoma lile basi likiitwa Champion
 
Sababu kuu mbili zinazochangia mabasi kuchelewa;

1. Miundombinu ya barabara haitoshelezi Mahitaji halisi ya wingi wa Vyombo vya Usafiri. Kwa mfano kipande cha Chalinze Dsm kinakuwa overloaded na magari ya abaria, mizigo nk nk mwishowe tunatumia muda mwiiiingi kwa kipande hicho. Kipande cha Chamwino ' Dodoma pia ni kero.

Inafikia hatua unatoka Mlandizi Mpaka Kibaha hupati nafasi ya kufanya overtaking bali foleni imefunga pande zote mbili.

Kwa ujumla masaa 4 yanapotea Dar - Moro wakati kiuhalisi ilitaliwa yatumike masaa 2 na hii inatokana na barabara kuelemewa na matumizi.

2. Sheria kandamizi zisizo enda na wakati yaaani kama wadau walivyoeleza hapo juu kwamba ukitoka Kigoma kuja Dsm hutakiwi kuvuka Gairo mpaka ifike saa 12:00 jioni, so hata ukifika pale saa 10 utakaa masaa 2 ili muda wa ratiba yako ufike. Hii pia inaenda sambamba na udumbufu ya Yange yange mikono kibaoooo.
 
Back
Top Bottom