Nini kinakuogopesha kufungua au kufanya biashara?

Extrovert

JF-Expert Member
Feb 29, 2016
67,029
173,693
Watu wengi wanatamani kufanya biashara wengine wana mitaji kabisa sababu unakuta yeye ni mtumishi hela sio swala la kuuliza ila when it comes to starting a business anajikuta anasita sita au kupatwa na uoga na jakamoyo!

Ijapokuwa kujiajiri na biashara ndio kitu ambacho kinaaminika kuleta utajiri katika maisha ya raia. Ni kipi kinakufanya au kilikufanya uogope kufungua biashara?

1619424900422.png

 
Biashara inahitaji usimamizi. Na hicho ndicho kinacho tufanya wafanyakazi wengi kuogopa. Lakini pia wengi tunakosa wazo bora la biashara.

Na badala yake tunaigana igana tu! Jambo hili huchangia sana kushindwa na kukata tamaa mapema.
 
Watu wengi wanatamani kufanya biashara wengine wana mitaji kabisa sababu unakuta yeye ni mtumishi hela sio swala la kuuliza ila when it comes to starting a business anajikuta anasita sita au kupatwa na uoga na jakamoyo!

Ijapokuwa kujiajiri na biashara ndio kitu ambacho kinaaminika kuleta utajiri katika maisha ya raia. Ni kipi kinakufanya au kilikufanya uogope kufungua biashara?

NDUGU YANGU NDUGU Wangari Maathai NJOO HUKU UPATE MWONGOZO!!!

 
Biashara inahitaji usimamizi. Na hicho ndicho kinacho tufanya wafanyakazi wengi kuogopa. Lakini pia wengi tunakosa wazo bora la biashara.

Na badala yake tunaigana igana tu! Jambo hili huchangia sana kushindwa na kukata tamaa mapema.
Nilichokuja kugundua biashara za makampuni ndio nzuri kuliko hizi za uchuuzi! Hasa kwa nyie ambao mna pa kujishikiza
 
Watu wengi wanatamani kufanya biashara wengine wana mitaji kabisa sababu unakuta yeye ni mtumishi hela sio swala la kuuliza ila when it comes to starting a business anajikuta anasita sita au kupatwa na uoga na jakamoyo!

Ijapokuwa kujiajiri na biashara ndio kitu ambacho kinaaminika kuleta utajiri katika maisha ya raia. Ni kipi kinakufanya au kilikufanya uogope kufungua biashara?
Binafsi mtazamo wangu kwa ujumla ninavyoona, uko hivi:

- Kwanza kuanzisha biashara ni kitu ambacho kitakupa jukumu zima la kufikiri wewe mwenyewe asilimia 100. Wakati ajira ukishapewa majukumu yako, umemaliza. Kampuni haipati faida, imepigwa fine, TRA wamefunga account wewe hujui hilo, unachotaka ni mshahara wako.

When it comes to business kufikiria solutions kunakuhusu. Na hakuna asiyejua namna kufikiria ilivyo kazi nzito.

- Kitu kingine ni ukosefu wa subra ( patience ).

Biashara mara nyingi siyo kitu unachoweza kuanzisha leo tu kesho ukawa Fred Vunjabei.

It takes lots of time, learning, failures, experience, trial and errors, mara njia hii, kesho ile.

Kuna vitu unaweza kuvisikia tu, lakini ukivifanya unakuta hali ni tofauti. Sasa ni either utafute njia yako upya au ukate tamaa.

- Jambo jingine ni uelewa wa watu kuhusu biashara, uwekezaji na uchumi bado uko chini sana.

Binafsi naamini hata mfanyakazi bado ni mfanyabiasha kwasababu anauza muda wake kwa masaa 8 kwa siku possibly na masaa mengine ya OT. Kwahiyo hapa ni suala la skills na negotiation if at all unajua kampuni unayofanyia kazi inakutegemea unaweza kuwapangia wakulipe vipi ( hili lipo sana kwa wachezaji wakiwa kwenye peak )

- Kitu kingine ni risk taking. Kuna watu wakipoteza hata laki tu, wanalia mpaka kamasi zinatoka. Ni ngumu sana kusema atafanya biashara anayohisi atapoteza. Hivyo ataendelea tu kusubiria biashara isiyo na risk miaka yote au kumbe hata haipo.

- Lastly, ni tamaa, ubinafsi, Kukosa uaminifu, na SifaMagu. Aisee nadhani mtu aliyefanikiwa kuwaroga wabongo kwenye mambo haya ALIFANIKIWA ASILIMIA 100.
Alituweza kikamilifu.

Siku zote mafanikio huwa hayakai mbali na ushirikiano ndio maana hakuna kitu kigumu mnooo kukifanya kama ushirikiano.

Kwetu sisi ukiwa na kimtaji chako unakomaa mwenyewe miaka nenda rudi hakikui, ukisema umpe mtu aunganishe mkuze mtaji anapotea na pesa yako. Mkisema kukopa wabongo hawaheshimu kabisa mikataba na makubaliano.

- Wengine hawako tayari kufanya biashara halali na kusubiri. Wanatafuta mafanikio ya haraka. Na hawa ndio wahanga wakubwa wa pyramid schemes.
Kwahiyo hizi ndio challenge kubwa zinazofanya watu kwa ujumla wanashindwa kuanzisha biashara.
 
Mtumishi ajenge nyumba za wapangaji ale kodi ndio biashara simple kwake
Yes ndio biashara ya wavivu wa kufikiri hio always wanakimbilia kujenga nyumba za kupangisha raia!

Its a good business tho na haina hasara kama utaweka strong and strict management ila inapendeza uifanye on a prime area lasivyo payback period yake inachukua muda mrefu sana! Kwangu hii naiona ni biashara inayowafaa wenye hela ndefu ambaye anaweza akasimamisha floor hata 7-10 kwenda hewani! Ni sehemu ya kutunzia hela ambayo huihitaji kwa haraka!

Ila uzuri wake mwengine ni kuwa inaanza kukupa kodi straightaway ukiingiza mpangaji tu! Hiki ndio watu wanapenda
 
Watu wengi wanatamani kufanya biashara wengine wana mitaji kabisa sababu unakuta yeye ni mtumishi hela sio swala la kuuliza ila when it comes to starting a business anajikuta anasita sita au kupatwa na uoga na jakamoyo!

Ijapokuwa kujiajiri na biashara ndio kitu ambacho kinaaminika kuleta utajiri katika maisha ya raia. Ni kipi kinakufanya au kilikufanya uogope kufungua biashara?
Mambo ya TRA yanaongoza kuzingua.
 
Binafsi mtazamo wangu kwa ujumla ninavyoona, uko hivi:

- Kwanza kuanzisha biashara ni kitu ambacho kitakupa jukumu zima la kufikiri wewe mwenyewe asilimia 100. Wakati ajira ukishapewa majukumu yako, umemaliza. Kampuni haipati faida, imepigwa fine, TRA wamefunga account wewe hujui hilo, unachotaka ni mshahara wako.

When it comes to business kufikiria solutions kunakuhusu. Na hakuna asiyejua namna kufikiria ilivyo kazi nzito.

- Kitu kingine ni ukosefu wa subra ( patience ).

Biashara mara nyingi siyo kitu unachoweza kuanzisha leo tu kesho ukawa Fred Vunjabei.

It takes lots of time, learning, failures, experience, trial and errors, mara njia hii, kesho ile.

Kuna vitu unaweza kuvisikia tu, lakini ukivifanya unakuta hali ni tofauti. Sasa ni either utafute njia yako upya au ukate tamaa.

- Jambo jingine ni uelewa wa watu kuhusu biashara, uwekezaji na uchumi bado uko chini sana.

Binafsi naamini hata mfanyakazi bado ni mfanyabiasha kwasababu anauza muda wake kwa masaa 8 kwa siku possibly na masaa mengine ya OT. Kwahiyo hapa ni suala la skills na negotiation if at all unajua kampuni unayofanyia kazi inakutegemea unaweza kuwapangia wakulipe vipi ( hili lipo sana kwa wachezaji wakiwa kwenye peak )

- Kitu kingine ni risk taking. Kuna watu wakipoteza hata laki tu, wanalia mpaka kamasi zinatoka. Ni ngumu sana kusema atafanya biashara anayohisi atapoteza. Hivyo ataendelea tu kusubiria biashara isiyo na risk miaka yote au kumbe hata haipo.

- Lastly, ni tamaa, ubinafsi, Kukosa uaminifu, na SifaMagu. Aisee nadhani mtu aliyefanikiwa kuwaroga wabongo kwenye mambo haya ALIFANIKIWA ASILIMIA 100.
Alituweza kikamilifu.

Siku zote mafanikio huwa hayakai mbali na ushirikiano ndio maana hakuna kitu kigumu mnooo kukifanya kama ushirikiano.

Kwetu sisi ukiwa na kimtaji chako unakomaa mwenyewe miaka nenda rudi hakikui, ukisema umpe mtu aunganishe mkuze mtaji anapotea na pesa yako. Mkisema kukopa wabongo hawaheshimu kabisa mikataba na makubaliano.

- Wengine hawako tayari kufanya biashara halali na kusubiri. Wanatafuta mafanikio ya haraka. Na hawa ndio wahanga wakubwa wa pyramid schemes.
Kwahiyo hizi ndio challenge kubwa zinazofanya watu kwa ujumla wanashindwa kuanzisha biashara.
Umeongea deep sana, ila hapo kwenye trial and error ndio pamenigusa zaidi! Panahitaji uvumilivu mno na huwezi tumia hela ya mtu kwa kufanya hizo trial and erros!

Hapo ndipo swala la income binafsi linapo kick in! Nikiwa na 5M nikaamua kui risk nikafanikiwa kuwin inakuwa heri ila nikizengua pia sawa sina lawama na mtu! Ila ikiwa ya mkopo au ya ndugu ni round moja tu ukizingua lawama zote zako!
 
Yes ndio biashara ya wavivu wa kufikiri hio always wanakimbilia kujenga nyumba za kupangisha raia!

Its a good business tho na haina hasara kama utaweka strong and strict management ila inapendeza uifanye on a prime area lasivyo payback period yake inachukua muda mrefu sana! Kwangu hii naiona ni biashara inayowafaa wenye hela ndefu ambaye anaweza akasimamisha floor hata 7-10 kwenda hewani! Ni sehemu ya kutunzia hela ambayo huihitaji kwa haraka!

Ila uzuri wake mwengine ni kuwa inaanza kukupa kodi straightaway ukiingiza mpangaji tu! Hiki ndio watu wanapenda
"ndio biashara ya wavivu wa kufikiri" at the same time "inawafaa wenye hela ndefu"
Kwani wenye hela ndefu ni wavivu kufikiri?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
"ndio biashara ya wavivu wa kufikiri" at the same time "inawafaa wenye hela ndefu"
Kwani wenye hela ndefu ni wavivu kufikiri?

Sent using Jamii Forums mobile app
Real Estate sio biashara ya mtu anaelipwa laki 8 Gross mjomba! Ni biashara ya watu walio stabilize kiuchumi likely billionaires!

Tuelezane ukweli tu la sivyo utawalisha sana watoto matembele bila sababu! Sisi wavivu wa kufikiria jinsi ya kuextend vyanzo vya mapato ndio tunaokimbilia less risky businesses kama kujenga tunyumba twa kupanga kwa mikopo ya kuunga unga ambako payback period ni miaka ya mtoto kuzaliwa mpaka kumaliza form 4!

Unakopa 100M unajenga nyumba mbili za kukupa laki 6 kila mwezi! Mwenzako hela hio hio ananunulia mtambo wa kufanyia kazi za printing na kutengeneza mabango. Akichukua tender kadhaa za makampuni yanayojielewa ndani ya miez 6 hela imerudi! Wewe kila mwaka ndio upate 7.2M mpaka ifike 100M ni lini?

Unajenga nyumba kwa kuacha maskio wakati mwenzio anapandisha floor 10 hewani huku ananunua apartments zingine Mikocheni na hayumbi!
 
Real Estate sio biashara ya mtu anaelipwa laki 8 Gross mjomba! Ni biashara ya watu walio stabilize kiuchumi likely billionaires!

Tuelezane ukweli tu la sivyo utawalisha sana watoto matembele bila sababu! Sisi wavivu wa kufikiria jinsi ya kuextend vyanzo vya mapato ndio tunaokimbilia less risky businesses kama kujenga tunyumba twa kupanga kwa mikopo ya kuunga unga ambako payback period ni miaka ya mtoto kuzaliwa mpaka kumaliza form 4!

Unakopa 100M unajenga nyumba mbili za kukupa laki 6 kila mwezi! Mwenzako hela hio hio ananunulia mtambo wa kufanyia kazi za printing na kutengeneza mabango. Akichukua tender kadhaa za makampuni yanayojielewa ndani ya miez 6 hela imerudi! Wewe kila mwaka ndio upate 7.2M mpaka ifike 100M ni lini?

Unajenga nyumba kwa kuacha maskio wakati mwenzio anapandisha floor 10 hewani huku ananunua apartments zingine Mikocheni na hayumbi!
Sawa tufanye itachukua miaka 15, au hata 20!

Lakini usikatae ndio investment inayowafaa zaidi watumishi.

Naona una'oversimplify' mambo.. Hizo tenda zinapatikana kirahisi hivyo?

Ukweli ni huu : kama ni muajiriwa inakuwia ngumu mno kufanya biashara zinazotaka muda na ambazo ni very risky. The safe investment na ya muda mrefu kwa waajiriwa inabaki kuwa real estate!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom